Kapt. Mkuchika na Maagizo yake!

Waziri Mkuchika amesema kuwa, waandishi wa habari wa tz, wanatakiwa wawe wametathimiwa ili tupate waandishi wazuri, tusipate watu wasio na elimu ya uandishi wa habari. hii itapunguza kupata habari manung'ayembe. hili suala limezungumziwa sana na nchi ze jirani, kuwa tz hakuna waandishi wa habari.

Chukua mfano, MTU ANAEITWA JERI MURO wa ITV, yule jamaa hana hata akili ya uandishi wa habari, halafu ni mkorofi kishenzi. kuna siku nilimshuhudia akipigana na mgambo walipotaka kumchukulia kipazasauti na mikamera yao...ni mtu mwenye jazba sana mimi namshauri kama anataka kuendelea na uandishi wa habari, aende shule zaidi(tulisoma nae pale udsm).

ukikumbuka siku ile gorofa lilipodondoka kule mnazimmoja, utaona namna alivyokuwa anahoji yule injinia, huwezi amini kama ni mwandishi aliyeenda shule, becuase he does not ask maswali yenye point, anauliza vile yeye anavyofikiri ndivyo bila hata kutafuta uhakika wake. Tatizo,yeye kama mfano wa waandishi wengine, anahoji kwa kuhukumu kila mtu anaemkuta kwenye eneo bila kujua kama ni mhusika au la, matokeo yake anamwaibisha mtu asiyehusika. ndo maana utaona waliokamatwa na polisi ni wengine, yule ambaye JERI MURO alimtuhumu kama ni mzemba hakuhusika. mwisho, yule jamaa alipata jazba halafu akashindwa kumjibu vizuri, ....

Nilimsikia Jeri muro kwa masikio yangu akitamka maneno haya" Aloo, wewe usinijibu hivi, wananchi watakuua sasahivi ukifanya mchezo", kutokana na hilo, yaani kauli ya kichochezi kama hiyo, wananchi waliokuwa wamemzunguka pale, walianza kutaka kumvamia yule jamaa hadi polisi walipomchukua na kumweka kwenye gari yao kama vila wanamwokoa. lakini sio kwamba aliwekwa mle kwasababu alikuwa na kosa.

You are making my point kuwa mtu anaweza "kusoma" na asiwe muandishi mzuri, na "asiyesoma" akawa muandishi mzuri.

Sasa huyu bwana kasoma UDSM, pale ndipo sehemu inaposadikika kutoka "elimu darasa" ya juu kabisa Tanzania, sasa wewe unataka aende kusoma wapi tena? Kama hawa graduates wa UDSM wanakuwa primitive hivi huoni kwamba tatizo si elimu tu, bali hali nzima ya maisha yetu, utamaduni wa kusoma, kutaka kujua mambo, kutaka kuvumbua, kuchunguza unadani wa vitu na si kuchukua vitu juu juu tu kama vinavyoletwa, kuleta vitu vipya na kadhalika.Hivi ni vitu ambavyo havifundishiki darasani, inabidi mtu avifanyie kazi yeye mwenyewe.

Sasa kama na wewe msomi wa UDSM unaweza kuja na a self defeating argument bila kujijua, huku ukimnyooshea kidole mwenzako, this leaves a lot to be desired about the quality of education at the epitomy of our educational institutions, namely UDSM.

Mimi naamini kuwapeleka watu wengine UDSM ni kuwalemaza permanently, labda tukitia mkazo kwenye kuwa na maktaba nyingi zaidi katika kila kitingoji tunaweza kupalilia usomi bila hii monopoly mbaya ya stashahada na shahada za vyuo.
 
You are making my point kuwa mtu anaweza "kusoma" na asiwe muandishi mzuri, na "asiyesoma" akawa muandishi mzuri.

Sasa huyu bwana kasoma UDSM, pale ndipo sehemu inaposadikika kutoka "elimu darasa" ya juu kabisa Tanzania, sasa wewe unataka aende kusoma wapi tena? Kama hawa graduates wa UDSM wanakuwa primitive hivi huoni kwamba tatizo si elimu tu, bali hali nzima ya maisha yetu, utamaduni wa kusoma, kutaka kujua mambo, kutaka kuvumbua, kuchunguza unadani wa vitu na si kuchukua vitu juu juu tu kama vinavyoletwa, kuleta vitu vipya na kadhalika.Hivi ni vitu ambavyo havifundishiki darasani, inabidi mtu avifanyie kazi yeye mwenyewe.

Sasa kama na wewe msomi wa UDSM unaweza kuja na a self defeating argument bila kujijua, huku ukimnyooshea kidole mwenzako, this leaves a lot to be desired about the quality of education at the epitomy of our educational institutions, namely UDSM.

Mimi naamini kuwapeleka watu wengine UDSM ni kuwalemaza permanently, labda tukitia mkazo kwenye kuwa na maktaba nyingi zaidi katika kila kitingoji tunaweza kupalilia usomi bila hii monopoly mbaya ya stashahada na shahada za vyuo.


No comment!
 
Uandishi wa habari na utangazaji uwe wa redio au televisheni ni kipaji na mtu anahitaji kukuza kipaji hicho.

Mathalan, mtu unaweza kuwa na taaluma yako ingine kabisa tuseme ya IT au Computing (BSc hons) lakini ukawa na kipaji na ukaenda kusomea PG Diploma in Mass Communications au MA in Business Computing kabisa. Baaada ya hapo ukatafuta ajira na ukatengeneza kipindi kuhusu Gadgets au Click with TBC.

Unakuwa unachakarika na majarida mbalimbali kuandaa vipindi vyako, kuhoji wataalam tena wengine kutoka palepale Mlimani au kwenda kutembelea makampuni mbalimbali yanayojihusisha na technology.

Sasa barrier kubwa ni lugha na ubunifu ndio vinatushinda sisi waafrika na kila wakati kufikiria kumlaumu mtu mwingine.
 
Nilisikia yote hayo kwa masikio yangu, na Jeri muro wa ITV namfahamu kwa njia ya tv tu. ila, huwa namshangaa hata mimi kusema ukweli, kwasababu anapohoji huwa anakuwa ni mtu wa jazba kama mtu wa mtaani/uswahilini vile. anajaji kabla ya kusikiliza maelezo. yaani, tz hatuna waandishi wazuri. tujifunze toka kwa wenzetu, kama mtu anatangaza mambo ya uchumi, inabidi awe mwandishi aliyesoma journalism halafu akasoma na degree ya uchumi, so it to every sector of journalism. sio kumchukua mtu aliyesoma kachuo fulani hivi pale buguruni au ilala. ndo maana watu wanawafanya kuwa matageti hivyohivyo.

Jeri alitoa kauli ya kichochezi siku ile. yeye alipofika pale kwenye jengo, tayari alikuwa ameweka kwenye mawazo yake kuwa mainjinia wa pale wote wabaya na wanatakiwa kufungwa bila kujua nani wenye makosa. ndo maana yule injinia alipofika kuhojiwa, jeri alikuwa anauliza maswali ya kumweka kifungoni na kama vile anamwamrisha, yaani kama vile yeye jeri na digrii yake moja, kama vile anamwamrisha vile, kumbe yule bosi. na kumwamrisha kwenyewe, alikuwa anamfokea na kuonyesha kuwa yule jamaa ni mzembe.

sijui kama hiyo ndo taaluma ya uandishi wa habari. kama humu ndani kuna waandishi wa habari wanaweza kulieleza hili. pia alitoa kauli ya kichochezi kusema kuwa jamaa atapigwa na wananch, apigwe kwasababu gani? je, hivi unafikiri kama ningekuwa mimi, umeniaibisha kwenye media kama vile halafu sina kosa, nitakuachaa? sikuachi, lazima nikutafute unaishi wapi nikufanyie. Mimi ni mwanasheria by profession, najua tu sheria zinazowahusu majonolisti, ila mengine siyajui. kama tunataka uandishi wa habari hapa tiz uungwe mkono na kila mtu, waandishi wa habari wanatakiwa wasiwe biased wanapofanya kazi zao.

you should not be biased whe you are asking questions, kwa njia hiyo, twaweza kupata ukweli halisi. being a mwandishi, sio mfalme, mtafungwa wengi sana kama hamtakuwa makini, na kama mtatoa habari msizokuwa na uhakika, mtayafilisi makampuni yenu, hamuoni SUMAYE ameshakula mill.100 kwa defamation yenu...hahaha, sisi wanasheria tunachekelea tu, tunataka watuletee watu ili tuwawakilishe tule hela za uwakilishi, hatuna shida.

Hapo juu kwenye higlights ndio kwenye hoja NZITO..Hata wenzetu ndio hivyo wanafanya...Mtu unakuwa mchumi kweli kama unaripoti issue ya uchumi..Kadhalika kwa siasa,michezo na hata issue za kijeshi.

Ila naona waanze kwanza kwa kuithamini taaluma ya waandishi na malipo yao yaongezwe.
Hapo watu wanahakikisha ceridibility ya habari kwani sasa hivi ni rahisi tu kusema...AAH..WAANDISHI UCHWARA NK.
 
Vyeti, vyeti, vyeti! Tanzania tunapenda vyeti kama tunavyopenda ulabu na uloda as if it really matters!

Nimelifikiria tamko la Mkuchika kwa upande mwingine si wa kisiasa bali ni wa kielimu.

Nitaanzia hapa ndani uwanja wa fujo. Kila mmoja wetu ana utaalamu wa kuongea, lakini ukiangalia uandishi wa hoja na dataz, unagundua haraka haraka kuwa mtoa hoja, hajafundishika katika suala la uandishi. iwe ni insha au majibu ya kitu, kuna kuchanganya vituo, matumizi mabaya ya herufi kubwa na ndogo, mkazo na maandishi yasiyolingana alimradi mtu kaamua kujiongelea na kutoa maoni.

Sasa kama hapa JF tunatapia hizo hatutumii kanuni tulizofunsishwa tangu shule ya msingi hata kuangalia kuwa maneno tuliyoandika tunayapitia kuyasoma tuyaelewe kwanza sisi wenyewe kabla ya kumpa mtu wa nne ayasome, tunafikiriaje Waandishi wa habari Tanzania watakuwa na tofauti na sisi?

Si sisi wana JF tunaojivuna vifua mbele kuwa tumesoma, tunajua mambo mengi, sasa kama kanuni rahisi za uandishi (writing) zinatushinda, je hao wa Tanzania watakuwaje, wawe wamesoma TSJ Buguruni au UDSM?

Matatizo ya magazeti na Televisheni kuonekana kuwa ni vihiyo si kosa la aliyeajiriwa kama mwandishi, ni makosa ya mwenye mali na mhariri wa idara na mhariri mkuu.

Kama Mkuchika lengo la kutoa kauli yake ni kuhusu uhakiki wa habari kupitia wahariri na wahariri wakuu, ndipo basi kuna haja ya kuwa na waliosomea Taaluma ya Uandishi na wanajua umuhimu wa habari kufanyiwa tahariri na hata wale wanaoajiriwa kama waandishi wa makala, utangazaji au habari kwa ujumla.

Kwa hili la uhakiki na uhariri, nitamuunga mkono Mkuchika, lakini mnalosema wengine hapa kuwa kuandika makala au kutangaza n ilazima uwe na cheti cha TSj, nafikiri huko ni kujidanganya!
 
Maadishi HOVYO ya kimcharazo na hata yasiyosomeka ya DAKTARI hayamaanishi kuwa yeye ni mjinga.

Pointi hapa ni kuboresha taaluma ya uandishi na si mashindano ya kuandika jf...Hapa ni kijiweni na ndio maana kuna wakati hata wachungaji hutowa lugha chafu.

Tubaki kwenye hoja...Kwamba kama mwandishi anaripoti kuhusu uchumi...Basi awe anajuwa anachokifuatilia ili ripoti yake iwe ni ya kumwelimisha mwananchi na si BORA LIENDE.
 
Tanzania bado haijaondokana na mfumo wa Chama Kimoja na songombingo za Ki-Lenin, Mao au Stalin!

CCM wanaogopa sana Independent thinkers! Domancy (possibly not even a word but fits to display rotten minds of CCM!) ya CCM inawatoa jasho. Wana Mwenyekiti Kilaza ambaye kakiri kuogelea na mawimbi hayawezi, hivyo kila siku wakisoma chambuzi kuonyesha uozo wao, wanatafuta sheria mbali mbali kudumisha utawala na udhaifu wao.

Ngoja nimalize kusahihisha "Waraka wa Mchungaji" nitauchapa kwenye Magazeti yote ya binafsi waongeze chachu ya kunitafuta kisha nitawatwanga na "Mwanitafuta ni mimi" na kumalizia na Screw Muungwana!

Rev. Kishoka,

Huwezi kufanya mpango na kuchapisha vijarida vidogo vya kusambaza nchi nzima BURE, ili uwafikie walio wengi? Manake nadhani watu wengi vijijini huku hawanunui magazeti. Asante.
 
Vyeti, vyeti, vyeti! Tanzania tunapenda vyeti kama tunavyopenda ulabu na uloda as if it really matters!

Nimelifikiria tamko la Mkuchika kwa upande mwingine si wa kisiasa bali ni wa kielimu.

Nitaanzia hapa ndani uwanja wa fujo. Kila mmoja wetu ana utaalamu wa kuongea, lakini ukiangalia uandishi wa hoja na dataz, unagundua haraka haraka kuwa mtoa hoja, hajafundishika katika suala la uandishi. iwe ni insha au majibu ya kitu, kuna kuchanganya vituo, matumizi mabaya ya herufi kubwa na ndogo, mkazo na maandishi yasiyolingana alimradi mtu kaamua kujiongelea na kutoa maoni.

Sasa kama hapa JF tunatapia hizo hatutumii kanuni tulizofunsishwa tangu shule ya msingi hata kuangalia kuwa maneno tuliyoandika tunayapitia kuyasoma tuyaelewe kwanza sisi wenyewe kabla ya kumpa mtu wa nne ayasome, tunafikiriaje Waandishi wa habari Tanzania watakuwa na tofauti na sisi?

Si sisi wana JF tunaojivuna vifua mbele kuwa tumesoma, tunajua mambo mengi, sasa kama kanuni rahisi za uandishi (writing) zinatushinda, je hao wa Tanzania watakuwaje, wawe wamesoma TSJ Buguruni au UDSM?

Matatizo ya magazeti na Televisheni kuonekana kuwa ni vihiyo si kosa la aliyeajiriwa kama mwandishi, ni makosa ya mwenye mali na mhariri wa idara na mhariri mkuu.

Kama Mkuchika lengo la kutoa kauli yake ni kuhusu uhakiki wa habari kupitia wahariri na wahariri wakuu, ndipo basi kuna haja ya kuwa na waliosomea Taaluma ya Uandishi na wanajua umuhimu wa habari kufanyiwa tahariri na hata wale wanaoajiriwa kama waandishi wa makala, utangazaji au habari kwa ujumla.

Kwa hili la uhakiki na uhariri, nitamuunga mkono Mkuchika, lakini mnalosema wengine hapa kuwa kuandika makala au kutangaza n ilazima uwe na cheti cha TSj, nafikiri huko ni kujidanganya!


Rev. Umesomea uandishi lakini?

Watakuja mpaka humu na kusema ili kuandika JF inabidi uwe na degree ya Journalism, this is an online forum after all.
 
" Aloo, wewe usinijibu hivi, wananchi watakuua sasahivi ukifanya mchezo" - Jerry Muro

ah... hapa naona siyo tu swala la taaluma ila uelewa wa mtu binafsi pia maana huwezi kwa akili zako kumwuliza mwenzako mbele ya hadhara maswali ya aina hiyo kama kweli una maadili, pia ni hatari katika hali ile. Kimsingi huyo jamaa atakuwa hana maadili kwa ujumla, sio tu maadili ya uana-habari, hana adabu kabisa. Kiburi chake ndicho kilichomsahaulisha kwamba alienda pale kujua na kuwahabarisha wananchi kilichotokea, sio kwenda kumkaba engineer... Sasa kama alishajua engineer ndio mwenye makosa alienda kufanya nini? kwanini hakutupa taarifa moja kwa moja kwamba engineer ndio mkosaji tumpige mawe...???
 
Vyeti, vyeti, vyeti! Tanzania tunapenda vyeti kama tunavyopenda ulabu na uloda as if it really matters!

Nimelifikiria tamko la Mkuchika kwa upande mwingine si wa kisiasa bali ni wa kielimu.

Nitaanzia hapa ndani uwanja wa fujo. Kila mmoja wetu ana utaalamu wa kuongea, lakini ukiangalia uandishi wa hoja na dataz, unagundua haraka haraka kuwa mtoa hoja, hajafundishika katika suala la uandishi. iwe ni insha au majibu ya kitu, kuna kuchanganya vituo, matumizi mabaya ya herufi kubwa na ndogo, mkazo na maandishi yasiyolingana alimradi mtu kaamua kujiongelea na kutoa maoni.

Sasa kama hapa JF tunatapia hizo hatutumii kanuni tulizofunsishwa tangu shule ya msingi hata kuangalia kuwa maneno tuliyoandika tunayapitia kuyasoma tuyaelewe kwanza sisi wenyewe kabla ya kumpa mtu wa nne ayasome, tunafikiriaje Waandishi wa habari Tanzania watakuwa na tofauti na sisi?

Si sisi wana JF tunaojivuna vifua mbele kuwa tumesoma, tunajua mambo mengi, sasa kama kanuni rahisi za uandishi (writing) zinatushinda, je hao wa Tanzania watakuwaje, wawe wamesoma TSJ Buguruni au UDSM?

Matatizo ya magazeti na Televisheni kuonekana kuwa ni vihiyo si kosa la aliyeajiriwa kama mwandishi, ni makosa ya mwenye mali na mhariri wa idara na mhariri mkuu.

Kama Mkuchika lengo la kutoa kauli yake ni kuhusu uhakiki wa habari kupitia wahariri na wahariri wakuu, ndipo basi kuna haja ya kuwa na waliosomea Taaluma ya Uandishi na wanajua umuhimu wa habari kufanyiwa tahariri na hata wale wanaoajiriwa kama waandishi wa makala, utangazaji au habari kwa ujumla.

Kwa hili la uhakiki na uhariri, nitamuunga mkono Mkuchika, lakini mnalosema wengine hapa kuwa kuandika makala au kutangaza n ilazima uwe na cheti cha TSj, nafikiri huko ni kujidanganya!

Ninaomba kutofautiana na wewe hapa mkuu, hapa JF tupo wananchi wa namna mbali mbali na kutoka kwenye avenue nyingi na tofauti za maisha, kinachotukutanisha hapa ni uchungu wa taifa letu, na siamini kuwa ili kutoa hoja ikaeleweka ni lazima iwe katika form fulani ya uandishi, au uandishi uliotukuka au ulioenda shule,

Hii comment ninaiona kama ni an insult kwa wale tusioenda shule, au tusioweza kuandika kama unavyotaka wewe kwa maneno yako hapo juu, ninaamini kuwa wananchi wote wanaruhusiwa kuja hapa kutoa maoni yao, bila ya kujali shule zao au uwezo wao kuandika, kwa sababu tukifanya hivyo basi itabidi wengi hapa ambao hatukwenda shule tuondoke,

I mean sina uhakika na the point lakini naona kama you should have been a little bit sensitive na maneno yako hapo juu, sio wananchi wote waliosoma vizuri kama wewe na wengine mnaojua kuandika vizuri, kama ninakuelewa vizuri , waacheni wananchi hapa JF waandike watakavyo na wawezavyo, tukianza hizi hatuwezi kufika mbali maana huu utakuwa ni ubaguzi period, between waliosoma na wanoweza kuandika vizuri na wasioweza, JF tunapswa kuwa bigger than mawazo ya namna hii!
 
You are making my point kuwa mtu anaweza "kusoma" na asiwe muandishi mzuri, na "asiyesoma" akawa muandishi mzuri.

Sasa huyu bwana kasoma UDSM, pale ndipo sehemu inaposadikika kutoka "elimu darasa" ya juu kabisa Tanzania, sasa wewe unataka aende kusoma wapi tena? Kama hawa graduates wa UDSM wanakuwa primitive hivi huoni kwamba tatizo si elimu tu, bali hali nzima ya maisha yetu, utamaduni wa kusoma, kutaka kujua mambo, kutaka kuvumbua, kuchunguza unadani wa vitu na si kuchukua vitu juu juu tu kama vinavyoletwa, kuleta vitu vipya na kadhalika.Hivi ni vitu ambavyo havifundishiki darasani, inabidi mtu avifanyie kazi yeye mwenyewe.

Sasa kama na wewe msomi wa UDSM unaweza kuja na a self defeating argument bila kujijua, huku ukimnyooshea kidole mwenzako, this leaves a lot to be desired about the quality of education at the epitomy of our educational institutions, namely UDSM.

Mimi naamini kuwapeleka watu wengine UDSM ni kuwalemaza permanently, labda tukitia mkazo kwenye kuwa na maktaba nyingi zaidi katika kila kitingoji tunaweza kupalilia usomi bila hii monopoly mbaya ya stashahada na shahada za vyuo.

Pundit,nadhani huyu bwana ameshindwa kutanabaisha kuwa uandishi wa habari nayo ni taaluma,hivyo haifai kuvamiwa na watu wasio na taaluma hiyo japokuwa wapo wasio na taaluma hiyo ila wana vipaji ambavyo vingetakiwa kuendelezwa kupitia taaluma hiyo. Jeri Muro sidhani kama pale mlimani kasomea uandishi wa habari,sina hakika sana kwani main campus haitoi taaluma ya uandishi wa habari NA UTANGAZAJI isipokuwa IJMC.Watu kama JERI Muro wapo wengi sana,sema kinachotakiwa hapa hata kama sio mwanataaluma ya uandishi wa habari yaani una taaluma nyingine basi angalau go for certificate in journalism ili uzijue japo ABC,kuliko kusomea public administration halafu maisha yako yote unabakia kufanya kazi ya uandishi wa habari bila hata kuwa na ABC zake,hii ndio inayoitwa abuse of professional,kwani mtu aliyesomea uandishi ukikutana haye akakuelekeza kitu unaweza hata kumjibu ovyo kwa kuwa wote mnafanya kazi moja utajiuliza anakuzidi nini?ndio maana taaluma nyingine kama sheria zimeamua kulinda taaluma hiyo kwa sheria kabisa bila kuwa na digrii ya kwanza ya sheria(LLB) huwezi kuruhusiwa kupractice sheria,hata uwe na masters ya sheria,ila bachelors ni kitu kingine legal professional haikutambui kama mwanasheria.
 
Pundit,nadhani huyu bwana ameshindwa kutanabaisha kuwa uandishi wa habari nayo ni taaluma,hivyo haifai kuvamiwa na watu wasio na taaluma hiyo japokuwa wapo wasio na taaluma hiyo ila wana vipaji ambavyo vingetakiwa kuendelezwa kupitia taaluma hiyo.

Strong point!
 
Augustoons,

Kwa hiyo wanaosoma sheria Marekani, amabao inawabidi wasome bachelor somo lingine halafu degree ya sheria ni ya pili, hawawezi ku practise sheria bongo?

A bit off the track but of substantial interest to me nevertheless.
 
Namuunga mkono Mkuchika kwa waandika habari wa kitanzania kweli wanaboa sana habari huwa zinakuwa na maswali mengi hazijiteshelezi.kama ITV news zao ni zile za Mwenyekiti Mengi awahasa vijana...Kikwete afungua zahanati,Dr Shein azindua mradi wa maji,Karume atoa vyeti vya Madrasa Nuur.....zinaboa sana.....
 
Mimi naamini habari ni zaidi ya taaluma, it is the fourth estate.

Kwa hiyo, kwa kufuatisha uhuru wa vyombo vya habari na demokrasia, kila mtu awe na uwezo wa kuandika na kujieleza.

Juzi nilikuwa nasoma "The Economist" online edition, katika wachangiaji kuna bwana mmoja mwalimu wa art alikuwa analalamika kwamba zile article za uchumi ni nzuri sana lakini zinaandikwa kwa lugha iliyo technical sana na zinakuwa inaccessible.Labda haya ndiyo matokeo ya usomi mwingi, ndiyo sababu magazeti serious hayauzi sana.Labda tunahitaji waandishi wetu wawe respresentative ya population yetu, labda inabidi tuache kuwa condescend watu wasio na degree na stashahada kwani mfumo wetu wenyewe wa elimu ni sandakarawe amina, mwenye kupata apate, mwenye kukosa akose, kipapatikio cha kuku, kuna watu hawajafika chuo kikuu si kwa sababu hawana uwezo wa kishule au hawajafaulu, ila kwa sababu nafasi hamna.

Unaona hapo? Naelewa kuhusu standards na kwa kiasi fulani ninaweza kukubali hili when it comes kujenga madaraja, lakini kuhusu fourth estate this becomes a little bit too much.

It just sounds too much like Mkuchika using some clever guise to stifle freedom of the press.
 
Wataka waandishi wasomi wakati hata hao wanaowaita hawajasoma wakiwauliza maswali muhimu wanabaki kurushiana mpira.
 
ndiyo sababu magazeti serious hayauzi sana.
Unafikiri sababu kubwa ya magazeti serous hayauzi ni hiyo?.....jiulize kwanini vitabu vya kupanua mawazo haviuziki hapa Bongo kuliko vile vya hadithi za Shigongo? hata magazeti kama raia mwema haliuzi sana kama magazeti pendwa kama kasheshe na wenzake
 
Back
Top Bottom