Kanisa la TAG mbona kama limepoa?

Kanisa la TAG mbona kama limepoa?

Jamani vipi kanisa la CCF lililokuwa na makao makuu yao pale sinza kumekucha mbona halisikiki tena,walikuwa wanandaa mkesha mkubwa pale uwanja wa taifa anayejua habari yake atujuze plz.
walukuwa na mzozo na huo ukumbi wao na watoto wa mzee aliyetoa sadaka huo ukumbi utumike kama nyumba ya ya ibada
 
mija kati y a ujinga wenye msaada alionifundisha mchungaji wangu wa TAG ni kuwa nisipende kujibu hoja ambayo iandhamiria kulikebehi kanisa na wala sio kufikia muafaka wa muulizaji kupata uelewa.
daima ukweli utasemwa hata na mawe.
 
Vp na haya makanisa yanayovuma kwa jina la mtu mmoja mmoja kwa mfano Lusekelo au Malisa, hayo makanisa yako chini ya mwamvuli gani? Wajuvi ufafanuzi tafadhali
hizo ni huduma zao wenyewe na ndiyo maana wengi wao wako sehemu moja tu
 
Kwanza nikupongeze kwa kuileta mada hii hata hivyo niseme tu kwamba wewe hauabudu huko TAG hivyo basi hata ufahamu wako kuhusu TAG inavyojiendesha si mpana kivile. Niseme tu kwamba TAG ilianza kuyumba wakati ule wa mgogoro kati ya Askofu Lazaro na Mwinjilisti Moses kulola (Hayati) ambao hatimaye uliamuliwa na mahakama na kufanya TAG igawanyike kuzaa EAGT iliyokuwa chini ya Moses kulola. Kwa bahati mbaya sana TAG wameendeleza na ule ugomvi hadi leo kwa kuendelea kuwaita EAGT waasi (Roho mtakatifu hawezi kufanya kazi mahali pasipo na msamaha wa kweli). Jambo moja lipo wazi kwamba TAG wamekosa mbadala wa Moses kulola wa kusimamia ile idara ya uinjilisti kitaifa ingawa baadhi ya nyakati wamekuwa wakifanya kazi na Egon Folk na kumwalika Rev Reinhard Bonkey na Daniel Kolenda (wa Christ for all Nations) mwaka jana. Nadhani pia pia uendeshwaji wa TAG (Central Administration) ni changamoto ambapo kama sikosei watumishi/huduma wanawezeshwa kimaisha na Headquarter bila kujali idadi ya washirika mtumishi anaosimamia LAKINI pia Wachungaji wengi umri umesogea sana na hivyo kushindwa kuendana (Mahubiri + Ushuhudiaji) na hali ya kizazi cha sasa.

NB: Nipo tayari kukosolewa
dhambi ya kuwakebehi EAGT na wale wapentekoste wenzao inawala.Ilifikia hatua mpaka wakatenga wanafunzi wao mashuleni CASFETA .Wale waluotengwa akina EAGT,FPCT and like wise ndiyo ukawa mwanzo wa kuanzishwa Umoja wao mashuleni wa TAYOMI.Hawa ndugu ni bora wakaona dhambi zao na kuzitubu ili kuleta neema na uwepo wa nguvu za Mungu kwenye Taasisi yao Mungu atawarehemu
 
TAG ilikuwa na nguvu tangu 19970's mpaka miaka ya kati ya 1980. Waliposhindwa kusolve tatizo mpaka ikapelekea kanisa kupasuka na ikazaliwa EAGT mwaka 1989....likawa anguko la TAG. Limebaki kanisa la wachungaji kushinda kusoma falsafa za dini yao ya assemblies tu na kupelekana marekani kusoma. Kuhubiri injili si issue tena kwao.....Hiyo miaka ya 2000 unayoisema sijui ni TAG gani unayoizungumzia.
mkuu mimi ndo nilianza kuifwatilia kidogo enz hizo
By the way TAG ya 2000 na sasa bado zina tofauti kubwa
 
Kaka kanisa hili la TAG mbona lipo vyema mpaka sasa tena linampango mkakati kabambe wa kuivuna Tanzania yote kwa Yesu mpango huo upewa jina la miaka 10 ya mavuno.Pia wametengeneza mpango wa kujenga vyuo vya kufundisha Theologia kila jimbo la makanisa yao.
Hakika wanafanya vyema zaidi ni kuwaombea ili wafanye vyema na wawe na uamsho wa kiroho katka nguvu kubwa.
Ni kanisa pekee la Kipendecost lenye mipango na maono makubwa ya kumtangaza Yesu likifatiwa na EAGT,FPTC,KLPT,P Holiness etc
NAkushauri uokoke na wewe ili urudishe huo moto uliopotea ambao Mungu amekuonyesha.
Barikiwa sana
 
Sikuzote ivumayo haidumu, shida hapo ni Elim, hii nikuazia wachungaji mpaka waumini.. Kwanini
Kukosa misingi mizuri ya kuweka mipango imara yenye kudum ndani ya kanisa. Najua wengi mtanipinga lkn ukweli utabaki palepale..
Labda nani anaejua mchungaji wa Tag ana degree?
Nimeshuhudia darasa la saba mtu akikabidhiwa kanisa na mojakwamoja kuitwa mchungaji.
Kuongoza jamii pia kunahitaji Elim sio kitu rahisi sana.
Pengine tujifunze kitu.. Kutoka makanisa ya Romani catholic, pendecoste, kkkt,Sabato.. Hawa wengi wao viongozi wana uwezo kielim.. Ni degree, phd nk.misingi yao hudum.
Na hawayumbi nawala hawana papara.
Askofu wao mkuu ana PHD anaitwa Barnabas Mtokambali ingia google uwacheck hao watu.Pia wanachuo chao kinaitwa CENTRAL BIBLE COLLEGE kipo Dodoma kinatoa hadi level ya Masters elimu Bibilia na Theologia pia wanachuo kikubwa Lindi,Mbeya,Arusha na Mwanza na wanajenga kingine kikubwa pia Tabora na kingine kipo pale opposite na Blue Pearl Hotel Ubungo kinaitwa Global Harvest kinatoa hadi Masters pia wamejiafiliate na chuo kipo Marekani kinaitwa Globa University .No research no right to speak.
 
KWELI KANISA HILI LIMEPOA SAAANA SABABU 1. WACHUNGAJI WAMEKUWA NA TAMAA YA KUPENDA PESA KULIKO MAELEZO, WACHUNGAJI WA KANISA LA T.A.G WANASHINDANA KWA MAISHA YA ANASA NA KUWALAZIMISHA WAUMINI WAO WAWACHANGIE PESA WANUNUE MAGARI MAZURI. MFANO KUNA KANISA LIKO MOSHI- SOWETO NI LA T.A.G LIMELAZIMISHA KILA MUUMMINI ATOE LAKI MOJA NA ZAIDI ILI KUMNUNULIA MCHUNGAJI GARI BILA KUJALI UWEZO WA KIUCHUMI WA WAUMINI WAO 2. UBAGUZI NDANI YA KANISA UMEKUWA MKUBWA SANA, WENYE PESA WANAPEWA KIPAUMBELE MASKINI HAWATHAMINIWI 3. UKABILA 4. VYEO VYA UPENDELEO NDANI YA KANISA 5. RUSHWA KATIKA CHAGUZI ZA MAASKOFU, MFANO UCHAGUZI UKIKARIBIA HUWA MAASKOFU WANATOA PIKIPIKI NA MAGARI KWA WACHUNGAJI NA WAANGALIZI, UCHAGUZI UKIISHA TU HAWAGAWI TENA. 6. KUKOSA KANISA KUBWA HALINA TV WALA REDIO ILA VIJANA WADOGO TU KINA MWAMPOSA/BULDOZA WANA REDIO NA TV. 7. KUTOTOA HUDUMA ZA KIJAMII, KANISA LINA MATAWI NCHI NZIMA ILA HALINA HATA HOSPITALI..WANA SHULE MBILI ZA SEKONDARI NAZO ZINZ MIUNDMBINU MIBOVU KULILKO HATA SHULE ZA KATA.8. KUKOSA UPENDO MIONGONI MWA WACHUNGAJI WAO KWA WAO, WACHUNGAJI WA MAKANISA YA MIJINI WANAISHI MAISHA YA HALI YA JUU SANA ILA WENZAO WA VIJIJINI WANA HALI MBAYA SANA NA WALA HAWASAIDIANI 9.TABIA YA KURITHISHANA MAKANISA KIUKOO NA KINDUGU MFANO BABA AKIZEEKA ANAMUACHIA MDOGO WAKE AU MTOTO WAKE HILI NALO NI TATIZO KUBWA MFANO CALVARY TEMPLE ARUSHA(T.A.G)
Kwa utafiti wangu wanawanashule tano za Sekondari ambazo ni Faraja,Siha,Ebeneza,nyingine ipo Singida ,nyingine ipo Sumbawanga.Pia wanachuo cha ualimu kipo Iringa Tanangozi.
Kwa upande wa Radio wanayo ipo jimbo la Mbeya mjini.
Hospitali wanayo katika chuo chao cha Dodoma na clinic ya kuzalishia wajawazito.
 
TAG Haijapoa kama unavyo fikiria kila zama na ukurasa wake TAG bado wako vizuri kumbuka kila kitu hakijabadrika ila huwafuatilii labda
 
TAG ilikuwa na nguvu tangu 19970's mpaka miaka ya kati ya 1980. Waliposhindwa kusolve tatizo mpaka ikapelekea kanisa kupasuka na ikazaliwa EAGT mwaka 1989....likawa anguko la TAG. Limebaki kanisa la wachungaji kushinda kusoma falsafa za dini yao ya assemblies tu na kupelekana marekani kusoma. Kuhubiri injili si issue tena kwao.....Hiyo miaka ya 2000 unayoisema sijui ni TAG gani unayoizungumzia.
 
mambo ya kiroho ni magumu kuyafasiri humu.Itabidi yajubiwe kimwili zaidi
 
Back
Top Bottom