Kanisa la TAG mbona kama limepoa?

Kanisa la TAG mbona kama limepoa?

Kipindi kile walikuwa wanasaka wateja sasa wamewapata wanakula posho tu mission completed
 
Tanzania Assemblies of God-T.A.G is even stronger than before:
1.Imekuwa na matawi nchi nzima, kila wilaya, kila kata.
2. T.A.G is the strongest Pentecostal denomination in the country. Askofu mkuu wa T.A.G ndiye Rais wa makanisa yote ya ki Assemblies ya Africa.
3.Ndiyo dhehebu pekee la kipentecost nchini lenye vyuo vya Biblia vinavyotoa diploma, degree hadi masters kwa kushirikiana na Global University ya USA
3.Ni dhehebu la kipentecost pekee nchini linalopeleka wamisionari nje ya Tanzania kama Rwanda, Burundi, Sudan kusini, DRC, na Magasca.
4.Linahubiri injili nchini kwa kasi zaidi kuliko huko nyuma.

Ukiangalia takwimu ya Nini T.A.G ilifanya huko nyuma na nini inafanya kwa sasa, na Neno linataka kanisa liweje utagundua kuwa ndiyo lina peak kwa viwango vikubwa.
Ubarikiwe mkuu
 
Makanisa ya watu binafsi nayoyakubali ni mawili tu, lile la Kakobe na la Gwajima hawa jamaa wanapinga sana watu wanao jiita mitume na manabii karne hii ya 21
Hamna kitu hapo...!!!

Kama huamini maneno yangu subiri Gwajima au Kakobe watangulie mbele za haki uone kama hivyo vikundi utavisikia....!!
 
Ya kale..""" ? Kale ya muda gani...??? Makanisa ya Kipentekoste yote ni juzi juzi tuu....Ni makanisa ambayo hayana msingi....akifa mchungaji na kanisa linaporomoka

Ya Kale kwa maana ya "Classical Pentecostalism". Hayo makanisa niliyoorodhesha yapo kwa zaidi ya miaka 70. Tatizo lenu mnadhani kila anayehubiri uponyaji na Roho Mtakatifu ana " practice classical Pentecostalism".. Nimekuorodheshea hayo makanisa kufanya utafiti wako utaona tofauti kubwa na makanisa hayo mbadala.
 
Kwa ufahamu wangu haya makanisa ya TAG nguvu ilianza kupungua tangu kipindi kile cha KULOLA kuanzisha EAGT. Lakini wakajitahidi sana kukaa ktk mstari wa unyoofu hapa na maanisha kuhubiri na kuishi sawa sawa na NENO la Mungu yaani utakatifu. Kilichikuja kuharibu ni usasa hasa baada ya kuanza ile mikutano ya jagwani na kwingineko kwa kushirikiana na foreign ministries hasa za USA. Wale walipoingia wakaleta usasa taratibu wanawake wakaanza kuvaa suruali na kujiremba kanisani na kila aina ya mapambo. Hapa wakapunguza nguvh ya Mungu. Shetani akaanza kuingia taratibu ktk hayo makanisa uzinzi ktk kwaya ukawa kawaida...wachungaji kufumaniwa ikawa kawaida. Wakaibuka waimbaji binafsi ndani ya makanisa ikazidisha mgongano was kimaslai among singers. Mara wachungaji binafsi wakapata kibali kujenga makanisa yako lna kuyaendesha ilimradi tuu yako affiliated na TAG ie
mlima wa moto .
Tatizo likawa kubwa zaidi watu wakaanza kutafuta maslai na si injili tena. Ule umoto wao wa injili miaka ya 2000 kurudi nyuma umepotea kwa kazi lkubwa sana. Na sasa kuibuka kwa makanisa mengi ya kibinafsi yanayohubiri miujuza ujiza ya kitapeli mara maji chumvi mafuta ya upako sijui utapata gari nyumba mke mume utaenda ulaya yamekuwa changamoto kweli kwa TAG. TAG washajua ni wapi wamekosea ila wanaogopa gharama za kurudi ktk mstari wao kuhubiri utakatifu kwa wachungaji wavaa suruali wanawake au wanaume waziznzi ni gharama kubwa. Kuanza kuwaambia watu waache mapambo na vimini ibadani ni gharama kubwa sana kwao koz watakosa sadaka zao na kwenda kwingine. Hapa ndo ilitakiwa wampate anaza KULOLA kuwanyoisha siyo hiyo mijitu ina phd ya theolojia haina chchote. However wapo wachungaji ndan EAGT na TAG kam KATUNZI wanajua wanafanya nini
 
Sijui mtoa uzi anatumia kipimo gani na kuona kuwa kanisa la TAG limepoa. Hakuna hata kimoja kilichokuwepo miaka ya nyuma ambacho kimepotea au kupungua. Kinyume chake kila eneo la ukristo wa kweli limeonyesha kukua. Washirika wengi makanisani wameokoka na ndiyo sifa mama ya kuwa mshirika wa kanisa. Wengi zaidi wamejazwa na Roho Mtakatifu na kunena kwa lugha kuliko zamani. Wahubiri leo ni wengi zaidi kuliko mwanzo ambapo ni wachache tu waliokuwa wanahubiri. Kuna wainilisti wa kitaifa wengi zaidi leo kuliko zamani. Miujiza kanisani ndio mahali pake na hufanyika kila ibada. Tatizo tu ni kwamba kanisa halina Tv yake, kwa hiyo yanayofanyika huko huwa hayafahamiki kwa kasi na watu walio nje. Wagonjwa bado wanaombewa na kupona na ni kitu cha kawaida sana. Kanisa limekua sana. Ila kama unahitaji kuona mbwembwe kama za "mitume na manabii" hapo utasubiri sana. Kanisa la TAG halifanyi huduma kama maonyesho, huduma hufanyika kwa staha ya hali ya juu na kuzingatia maadili kwa hali ya juu. Hutasikia habari ya mafuta ya upako, wala maji ya upako wala chochote kinachofanana na hayo. Ila NENO huhubiriwa na kufundishwa kikamilifu na Roho Mtakatifu hulithibitisha kwa ishara na miujiza. Karibu katika kanisa lolote la TAG kwa msaada na ushauri zaidi. Lakini mwisho, unatakiwa uokoke binafsi ili uwe tayari kumlaki Yesu mara arudipo mawinguni. Mungu akubariki, binafsi nimeokoka na ninampenda sana Yesu. Nimeamua kuachana na dhambi. Ya kale yamepita, tazama yote yamekuwa mapya. Na wewe unaweza kuachana na maisha ya dhambi na haujachelewa bado.
 
Ni kweli uliloongea, uchaji wa Mungu umepungua miongoni mwa waumini jambo linalofanya yule roho mtakatifu kutofanya kazi kama mwanzo. Kingine sio TAG tu Bali kuna EAGT ambalo ni tawi la TAG lilitokea baada ya kugombana Askofu Lazaro na Marehemu Askofu Moses Kulola. Miaka ya 80's na 90's yalipata umaarufu na kuenea kwa kasi huku wakivuna waumini wengi kutoka madhehebu walioyaita wasioamini katika wokovu, ubatizo wa maji mengi na vipawa vya roho mtakatifu.
Sababu za kuporomoka ni hizi, wazazi waliokoka kweli lakini watoto waliozaliwa kwenye hayo makanisa ni waumini tu sio wamekata ushauri,jingine ni ministries zilizoanza zinavuna waumini sana kutoka hayo makanisa na bahati mbaya watu wanakimbilia muujiza wa mafanikio wa maisha na sio kuimarika kiroho, wachungaji wao baadhi wameingia katika kupenda fedha kuliko kufundisha neno la Mungu
 
Sikuzote ivumayo haidumu, shida hapo ni Elim, hii nikuazia wachungaji mpaka waumini.. Kwanini
Kukosa misingi mizuri ya kuweka mipango imara yenye kudum ndani ya kanisa. Najua wengi mtanipinga lkn ukweli utabaki palepale..
Labda nani anaejua mchungaji wa Tag ana degree?
Nimeshuhudia darasa la saba mtu akikabidhiwa kanisa na mojakwamoja kuitwa mchungaji.
Kuongoza jamii pia kunahitaji Elim sio kitu rahisi sana.
Pengine tujifunze kitu.. Kutoka makanisa ya Romani catholic, pendecoste, kkkt,Sabato.. Hawa wengi wao viongozi wana uwezo kielim.. Ni degree, phd nk.misingi yao hudum.
Na hawayumbi nawala hawana papara.
 
Kwa ufahamu wangu haya makanisa ya TAG nguvu ilianza kupungua tangu kipindi kile cha KULOLA kuanzisha EAGT. Lakini wakajitahidi sana kukaa ktk mstari wa unyoofu hapa na maanisha kuhubiri na kuishi sawa sawa na NENO la Mungu yaani utakatifu. Kilichikuja kuharibu ni usasa hasa baada ya kuanza ile mikutano ya jagwani na kwingineko kwa kushirikiana na foreign ministries hasa za USA. Wale walipoingia wakaleta usasa taratibu wanawake wakaanza kuvaa suruali na kujiremba kanisani na kila aina ya mapambo. Hapa wakapunguza nguvh ya Mungu. Shetani akaanza kuingia taratibu ktk hayo makanisa uzinzi ktk kwaya ukawa kawaida...wachungaji kufumaniwa ikawa kawaida. Wakaibuka waimbaji binafsi ndani ya makanisa ikazidisha mgongano was kimaslai among singers. Mara wachungaji binafsi wakapata kibali kujenga makanisa yako lna kuyaendesha ilimradi tuu yako affiliated na TAG ie
mlima wa moto .
Tatizo likawa kubwa zaidi watu wakaanza kutafuta maslai na si injili tena. Ule umoto wao wa injili miaka ya 2000 kurudi nyuma umepotea kwa kazi lkubwa sana. Na sasa kuibuka kwa makanisa mengi ya kibinafsi yanayohubiri miujuza ujiza ya kitapeli mara maji chumvi mafuta ya upako sijui utapata gari nyumba mke mume utaenda ulaya yamekuwa changamoto kweli kwa TAG. TAG washajua ni wapi wamekosea ila wanaogopa gharama za kurudi ktk mstari wao kuhubiri utakatifu kwa wachungaji wavaa suruali wanawake au wanaume waziznzi ni gharama kubwa. Kuanza kuwaambia watu waache mapambo na vimini ibadani ni gharama kubwa sana kwao koz watakosa sadaka zao na kwenda kwingine. Hapa ndo ilitakiwa wampate anaza KULOLA kuwanyoisha siyo hiyo mijitu ina phd ya theolojia haina chchote. However wapo wachungaji ndan TAG kam KATUNZI anajua anafanya nini
Katunzi ni Mch.wa EAGT siyo TAG...
 
TAG imekwisha, Baada ya kuimarika kwa EAGT. Hata hivyo kanisa kutoshirikiana na muungano wa makanisa ya kipentekoste (PCT) imelifanya hili kanisa kutoeleweka na jamii.
 
KWELI KANISA HILI LIMEPOA SAAANA SABABU 1. WACHUNGAJI WAMEKUWA NA TAMAA YA KUPENDA PESA KULIKO MAELEZO, WACHUNGAJI WA KANISA LA T.A.G WANASHINDANA KWA MAISHA YA ANASA NA KUWALAZIMISHA WAUMINI WAO WAWACHANGIE PESA WANUNUE MAGARI MAZURI. MFANO KUNA KANISA LIKO MOSHI- SOWETO NI LA T.A.G LIMELAZIMISHA KILA MUUMMINI ATOE LAKI MOJA NA ZAIDI ILI KUMNUNULIA MCHUNGAJI GARI BILA KUJALI UWEZO WA KIUCHUMI WA WAUMINI WAO 2. UBAGUZI NDANI YA KANISA UMEKUWA MKUBWA SANA, WENYE PESA WANAPEWA KIPAUMBELE MASKINI HAWATHAMINIWI 3. UKABILA 4. VYEO VYA UPENDELEO NDANI YA KANISA 5. RUSHWA KATIKA CHAGUZI ZA MAASKOFU, MFANO UCHAGUZI UKIKARIBIA HUWA MAASKOFU WANATOA PIKIPIKI NA MAGARI KWA WACHUNGAJI NA WAANGALIZI, UCHAGUZI UKIISHA TU HAWAGAWI TENA. 6. KUKOSA KANISA KUBWA HALINA TV WALA REDIO ILA VIJANA WADOGO TU KINA MWAMPOSA/BULDOZA WANA REDIO NA TV. 7. KUTOTOA HUDUMA ZA KIJAMII, KANISA LINA MATAWI NCHI NZIMA ILA HALINA HATA HOSPITALI..WANA SHULE MBILI ZA SEKONDARI NAZO ZINZ MIUNDMBINU MIBOVU KULILKO HATA SHULE ZA KATA.8. KUKOSA UPENDO MIONGONI MWA WACHUNGAJI WAO KWA WAO, WACHUNGAJI WA MAKANISA YA MIJINI WANAISHI MAISHA YA HALI YA JUU SANA ILA WENZAO WA VIJIJINI WANA HALI MBAYA SANA NA WALA HAWASAIDIANI 9.TABIA YA KURITHISHANA MAKANISA KIUKOO NA KINDUGU MFANO BABA AKIZEEKA ANAMUACHIA MDOGO WAKE AU MTOTO WAKE HILI NALO NI TATIZO KUBWA MFANO CALVARY TEMPLE ARUSHA(T.A.G)
 
Habari za muda huu waungwana?
Natumai mnaendelea vizuri hasa baada ya mihangaiko ya siku.

Niende moja kwa moja kwenye mada niliyokusudia kuianzisha leo.

Kwa wale wakristo mtakua mpo aware zaidi kuhusu ukristo ulivyo na ulivyo hapa nchini.

Miaka ya nyuma kidogo ukristo ulikua imeenea zaidi kwa makanisa ya Romani Catholic, Lutheran na Pentecoste. Miaka ilivyokwenda zaidi ndipo tulipo shuhudia idadi kubwa ya makanisa hapa nchini.

Nakumbuka miaka ya 2000 kanisa la TAG lilianza kuja kwa kasi sana. Kufikia miaka ya '03-0'5 walikua wanasikika sana kutokana na makongamano makubwa na mahubiri yao.
Hawa watu walikua wanaponda sana makanisa mengine hususan wakatoliki.Hapa ndipo walipopata waumini wengi kutoka makanisa kongwe niliyotaja hapo juu kutokana na miujiza waliyokua wanafanya makanisani mwao kama kutoa pepo na kuombea wagonjwa just little to mention.

Walikua kwa kasi sana na hapa matajiri wengi pia walihamia huko wakajenga makanisa nchi nzima na kukua kwa kasi kutokana na styl yao mpya ya kuabudu na mahubiri.

Ilikua changamoto sana kuoa binti wa kilokole enzi hizo.Ilifika mahali mtu akitoka katoliki,lutheran au pentecoste akajiunga TAG alikua anatengwa na familia na ndugu na aliitwa muasi.Ikafika mahali kukawa na kama ka uadui fulani kati madhehebu hayo.
Enzi hizo karibu kila mlokole alikua anaweza kutoa pepo na kuongea zile lugha zao.

Miaka ilivyo anza kwenda sasa;taratiiibu ile power yao ya ku preach na kufanya miujiza ikaanza kupotea na kufifia.
Hivi sasa wameshazoeleka na wapo very normal sana.
Hivi sasa wana intergrate na wakristo wengine vizuri sana tofauti na zamani.

Maswali yangu:

1:Kwanini TAG wamepoa sana na hawapo hot kama zamani?
2:Je mi kwa sababu waumini wamesha jaa hivyo basi hawana nia ya ku expand zaidi?
3:Au ni utandawazi unachangia?

Karibuni kwa mawazo
Kwanza nikutulize, Je wewe ni mshirika wa kanisa la TAG? Kama ndio, umefanya nini kulisaidia kanisa lisipoe? Au unafikiri hiyo ni kazi ya wachungaji na maaskofu peke yao?
Kama wewe sio mshirika (mtazamaji), unangoja nini kuokoka? Unapata wapi ujasiri wa kulikosoa kanisa ikiwa wewe sio mshirika na wala huhusika?
 
Kwanza nikutulize, Je wewe ni mshirika wa kanisa la TAG? Kama ndio, umefanya nini kulisaidia kanisa lisipoe? Au unafikiri hiyo ni kazi ya wachungaji na maaskofu peke yao?
Kama wewe sio mshirika (mtazamaji), unangoja nini kuokoka? Unapata wapi ujasiri wa kulikosoa kanisa ikiwa wewe sio mshirika na wala huhusika?
Punguza povu kijana,TAG sio kanisa ni kikundi cha wapiga dili kwani ukiangalia misingi yake inathibitisha hilo.
 
Kwanza nikutulize, Je wewe ni mshirika wa kanisa la TAG? Kama ndio, umefanya nini kulisaidia kanisa lisipoe? Au unafikiri hiyo ni kazi ya wachungaji na maaskofu peke yao?
Kama wewe sio mshirika (mtazamaji), unangoja nini kuokoka? Unapata wapi ujasiri wa kulikosoa kanisa ikiwa wewe sio mshirika na wala huhusika?
Unajua maana ya "KUOKOKA" wewe..????
 
hii thread naona watu wanatiririka sana na nimejifunza mengi ambayo nilikua siyajui.

Wapo wanao ipinga kwa hoja nyepesi na wapo wanaiopinga kwa FACTS.

Wapo wanakubaliana na mimi kwa maelezo mazuri tena kuliko mimi
 
Habari za muda huu waungwana?
Natumai mnaendelea vizuri hasa baada ya mihangaiko ya siku.

Niende moja kwa moja kwenye mada niliyokusudia kuianzisha leo.

Kwa wale wakristo mtakua mpo aware zaidi kuhusu ukristo ulivyo na ulivyo hapa nchini.

Miaka ya nyuma kidogo ukristo ulikua imeenea zaidi kwa makanisa ya Romani Catholic, Lutheran na Pentecoste. Miaka ilivyokwenda zaidi ndipo tulipo shuhudia idadi kubwa ya makanisa hapa nchini.

Nakumbuka miaka ya 2000 kanisa la TAG lilianza kuja kwa kasi sana. Kufikia miaka ya '03-0'5 walikua wanasikika sana kutokana na makongamano makubwa na mahubiri yao.
Hawa watu walikua wanaponda sana makanisa mengine hususan wakatoliki.Hapa ndipo walipopata waumini wengi kutoka makanisa kongwe niliyotaja hapo juu kutokana na miujiza waliyokua wanafanya makanisani mwao kama kutoa pepo na kuombea wagonjwa just little to mention.

Walikua kwa kasi sana na hapa matajiri wengi pia walihamia huko wakajenga makanisa nchi nzima na kukua kwa kasi kutokana na styl yao mpya ya kuabudu na mahubiri.

Ilikua changamoto sana kuoa binti wa kilokole enzi hizo.Ilifika mahali mtu akitoka katoliki,lutheran au pentecoste akajiunga TAG alikua anatengwa na familia na ndugu na aliitwa muasi.Ikafika mahali kukawa na kama ka uadui fulani kati madhehebu hayo.
Enzi hizo karibu kila mlokole alikua anaweza kutoa pepo na kuongea zile lugha zao.

Miaka ilivyo anza kwenda sasa;taratiiibu ile power yao ya ku preach na kufanya miujiza ikaanza kupotea na kufifia.
Hivi sasa wameshazoeleka na wapo very normal sana.
Hivi sasa wana intergrate na wakristo wengine vizuri sana tofauti na zamani.

Maswali yangu:

1:Kwanini TAG wamepoa sana na hawapo hot kama zamani?
2:Je mi kwa sababu waumini wamesha jaa hivyo basi hawana nia ya ku expand zaidi?
3:Au ni utandawazi unachangia?

Karibuni kwa mawazo
unatakiwa ujibiwe kimaandiko.Kifupi ni kwamba siku za mwisho upendo wa wengi utapoa
 
Back
Top Bottom