Kanisa katoliki wamwibia mjane

Kanisa katoliki wamwibia mjane

Ushabiki wa kidini unawapeleka vibaya sana humu. Yaani mnaambiwa huyo mama ana lease halali ya serikali juu ya umiliki wa eneo hilo bado mnasema eti aliapewa na kanisa akae kwa muda tu? Kanisa lilikuwa wapi wakati huyo mama na huyo mumewe mtaliano wakati wanapewa hiyo hati ya umiliki wa ardhi hiyo?
 
sitafuti public sympathy mzee,hili swala linajulikana marangu nzima,iyo lease nitaiweka apa
Nadhani ushauri mzuri kwa sasa ni kupeleka suala hilo katika baraza la ardhi au mahakama ya ardhi kwa usuluhishi. JF haiwezi kumpa haki huyo mjane wala wewe mwenyewe.
 
Unaonekana ni mwenye kuongea kwa ushabiki ukiomba public sympathy bila kujali kwamba unaweza kugundulika.

Uzoefu unanionesha kwamba wengi wa wanaoitwa wajane si watu wa kuwasikiliza upande mmoja na kufanya maamuzi. Ikiwa unahusika kwa kiasi hicho na hilo shauri, bila shaka ungetuwekea Lease ya hilo shamba (sio Liz) ili tujionee na si kuropoka km mama wa kiswahili.

Mkuu hii story ya kina Balleto naijua...huyu mama alikuaga mtawa na huyu mzungu alikua anafanya kazi kwenye hiyo hospital ya kanisa.....huyu mama kipindi hicho alikua hapo kwenye hospitali ya kanisa kama nesi na mtawa...lakini aliasi utawa akatembea na huyo mzungu akapata ujauzito akazaa mtoto. anayeitwa John Barreto..jamaa mmoja alikuaga machachari sana kipindi cha nyumba kwa kutembea na mabinti wa Arusha. Ukienda Arusha huyu jamaa anajulikana sana. Kwa kifupi hilo shamba na hospitali ilikua mali ya kanisa na huyo mama alikuaga hapo kama mtawa muhudumu akaja akaasi akatembea na huyo mzungu.
 
Kanisa Katoliki linatoa ardhi haliibi ardhi....Ni taasisi kubwa duniani inayomiliki ardhi ya dunia kwa asilimia kubwa...

Huyo mjane ndo kalibia kanisa ardhi
 
Benteke kama unaijua hii habari mbona unaongea uwongo?mmoja wa mawakala nini ndugu yangu,Iyo shule ya marangu enyewe sio ya katoliki kiasili chunguza tuu,msitake tumwage kweli maana tutalidhalilisha kabisa hapa
 
Benteke kama unaijua hii habari mbona unaongea uwongo?mmoja wa mawakala nini ndugu yangu,Iyo shule ya marangu enyewe sio ya katoliki kiasili chunguza tuu,msitake tumwage kweli maana tutalidhalilisha kabisa hapa

Muulize ndugu yako John Barreto anayeishi Arusha ni mtoto. wa nani? na pia muulize huyo mama alimzaa John na nani? na kipindi cha nyuma huyo mama alikuaga nani? mkuu mimi huko ndio kwetu na nimekulia huko.
 
Ni kama nafahamu hili eneo, ni mashamba makubwa sana yalikuwa yanamilikiwa na maburuda,
Na pia walikuwa hawaendelezi haya mashamba kwa hiyo miaka ya nyuma walikuwa wanagawa kwa mtu yeyote mwenye kutaka kulima unalima lakini ujue kuwa eneo siyo lako.

Kwa miaka hii kama ukishindwa kuendeleza eneo huwa linachukuliwa, hasa sehemu zenye ufinyu wa ardhi kama huko marangu.

La maana kama kanisa wasimdhulumu mama mjane,
wakae naye mezani ili wanunue hilo eneo; itasaidia nini kujenga hekalu kwenye ardhi uliyodhulumu? Je ni Mungu yupi unayemuabudu? Kama ni Mungu ambaye ni MUME WA WAJANE ni lazima wamlipe mjane wa watu.
 
kanisa katoliki ni zaidi ya ulijuavyo wewe....!!
Kanisa katoliki jimbo kuu la Moshi pamoja na shule yake ya sekondari Marangu bila aibu wala hofu ya Mungu wamuhubiriaye maana hi ni taasisi ya kidini wamemnyang'anya mjane shamba aliloachiwa na marehemu doctor Geovan Balletto.

Shamba hilo ambalo lina liz lipo jirani kabisa na shule ya Marangu inayomilikiwa na kanisa Katoliki, limekuwa likikaliwa na marehemu na familia yake na baada ya kifo chake mnamo 1972 alimuacha hapo mjane na mtoto wao.

Ndani ya shamba hilo kulikuwa na hospitali ambapo doctor huyo aliyekuwa mzungu raia wa Italy alikuwa akiwatibu na kuwasaidia sana wanakijiji wa Marangu na vijiji vya karibu akisaidiana na mjane huyu ambaye alikuwa nesi.

Pia kulikuwa na mazao pamoja na miti mingi na nyumba kubwa ya kuishi ambayo mpaka leo familia inaishi hapo,bila haya kanisa na taasisi yake bila ruhusa ya mjane huyo waliingiingia kwa nguvu kwenye shamba hilo na kukata miti mingi tuu na kujenga kisima.

Waliharibu mazao na kutandaza mabomba ya kupeleka maji shuleni kwao,kana kwamba hiyo haitoshi kanisa lilijitwalia eneo la ekari tatu hivi na kuanza ujenzi,mjane huyo alipouliza aliwekwa ndani kituo cha polisi HIMO.

Imekuwa kawaida kila hila na uonevu dhidi ya mama huyu mjane kutumika kwa polisi wa himo{RUSHWA KANISANI?}.

Hivi sasa kanisa linatumia nguvu kubwa ya fedha {sadaka} na hila ili wataifishe shamba hili ambalo lina liz na uhalali wote uliochwa na marehemu kwa familia yake,kanisa linafanya haya kupitia mawakala wake wakuu askofu mkuu Moshi pamoja na mwalimu mkuu Marangu sekondari ambaye kila kikicha anamtishia mama huyu maisha.

Je ni lini kanisa katoliki litaacha kuonea walalahoi na kwa kutumia sadaka zetu wenyewe?

Kupitia hapa tunaamini mama huyu atapata msaada kutoka kwa serikali,wanasheria,wanaharakati na watu mbalimbali hii ikiwa ni pamoja na ushahuri.
 
Benteke labda kwa mazoea tu ya jamii flani wakimuona mzungu wanaamini ni padre,ila huyu dr pamoja na mama mjane hawajawahi kuwa ivyo usemavyo,
 
Benteke labda kwa mazoea tu ya jamii flani wakimuona mzungu wanaamini ni padre,ila huyu dr pamoja na mama mjane hawajawahi kuwa ivyo usemavyo,

Mzungu hakuwa padre ila mama alikua mtawa
 
Sizani kama nikanisa kweli lawezafanya kit hicho.Ila kutokana na ubinadamu kupungua pia lawezekana kwa maslahi ya wachache.Moshi kuna chama cha wanasheria watoao masaada wakisheria,msaidie kuwakutanisha nae
 
Unafanya kampeni kanisa hili lifutwe kabisa serikali?una uhakika utafanikwa?anya mambo ya maana baba.

Hata kama kampeni zake za kutaka kanisa la Rc lifutwe hatofanikiwa lakini atakuwa amefanikiwa kutujuza sisi uchafu unao fanywa na viongozi wa kanisa husika.
Kulawitiwa wtt wadogo na viongozi wa kiroho ni jambo chafu sana na la kishenzi kupita kiasi.
Mm nafikiri kama kweli unataka utetezi wa bw Yesu basi na ww huna budi kuungana na kahtan kulaani vitendo hivyo ili upate kuwa jirani na bw yesu.
 
Benteke labda kwa mazoea tu ya jamii flani wakimuona mzungu wanaamini ni padre,ila huyu dr pamoja na mama mjane hawajawahi kuwa ivyo usemavyo,

Mkuu hilo eneo miaka yote wa2 wanajua ni mali ya kanisa istoshe mama john kama ana lease hawezi pokonywa hpo period,ila historia yake alikua mtawa
 
Mama mjane anayo lease, na kama kanisa nalo linaamini wanayo lease yao hiyo ni double allocation.
Before the eyes of law wote tunajua the justice should be done and seen to be done.
Wote tunaelewa samaki mkubwa huwa anaamini kuwa anayo haki ya kummeza samaki mdogo ila kwa huyu mama hatuna budi kufatilia mashauri husika kwa karibu ili kuiweka wazi jamii ya wale wenye kujali haki,utu na ubinadamu wajue jinsi kanisa husika kama linatenda haki ama halitendi haki kwa mama husika.
Itakuwa ni aibu sana kama mabavu yatatumika ila naamini vyombo husika kuanzia land tribunal hadi mahakama vitazingatia haki ya huyu mama na pia vitazingatia kuwa kesi hii inatazamwa na level ya dunia na sio kijiji tena kama walidhani ni siri basi nawasihi tu wajue kuwa kesi hii itakwenda kuliabisha kanisa kama ubabe na outlaw acts zinazofanywa na kanisa zitaendelea dhidi ya mama huyu.

acha hizo haki haidhulumiwi xo acha majungu
 
Mkuu benteke mbona hueleweki mara padre mara si padre, hujui usemalo rud upewe detail vizuri ww, mimi mwenyewe ni mkatoliki lakini hapa kanisa halitendi haki, wewe inaelekea labda tu una bifu na huyo john, maana hata kama ametembea na mabint, haihusian na mama yake kudhulumiwa
 
Huyo mjane naye ni Muitaliano?Ana watoto wangapi?Nao ni Waitaliano?Kwanini wasirudi kwao Italy wakaacha eneo litumike na jamii badala ya kuendelea kuishikilia eneo la Tanzania wakati wao si Watanzania?
 
Daaa Mungu ashukuriwe kama hii habari imefika hapa, hii habari naifahamu vizuri kwani mimi ni mzaliwa wa pale rauya jirani kabisa na shule pamoja na huyu mjane hua anaitwa mama John. Huyu mama ameliaga sana jamani, ni kweli kanusa na shule vimemtesa haswa. Siongei hivi kulichafua kanisa sababu hapa rauya wanakijiji asilimia 99 ni wakatoliki nikiwemo na mimi hata na huyo mjane, hapa tunasimamia ukweli kanisa limezidi uonevu hadi kwa waumini wake halijal, huyu mama ana lease halali na tulishamshauri aende kanisan kwa baba askofu lkn pia hawakumsaidia, kanisa katoliki tunakwenda wapi? Yule mzungu alikuepo hapa kabla hata shule haijajengwa na alikua na hospitali yake binafsi hapa na lile jengo la hosp bado lipo pale na pia alikua na nyumba aliyoishi na mkewe na hadi sasa yule mjane anaishi kwenye nyumba hiyo. Shule ya marangu mwanzoni haikua ikimilikiwa na kanisa ila baadae kanisa lilikabidhiwa shule ile na baada ya kanisa kuingia pale ndo matatizo yalianza wakawa wanalitaka lile eneo wampe pesa mama john awauzie, mama john hakuafiki hilo sababu alisema hiyo ni kumbukumbu ya mumewe na urithi wa mtoto wao john. Vitimbi vikaanza kwa nguvu shule iliingia pale karibu kabisa na nyumba wanayoishi likajenga kisima ambacho hadi leo kipo na waligombana sana na yule mjane mpaka mjane aliwekwa polisi himo, huwa wanakijiji tunahis kanisa na shule havikujua kua mama ana lease, baadae kanisa lilidai kua marehemu aliacha usia kua shamba ligawanywe nusu kwa nusu na mjakaz wao na marehem sababu ambayo haina mashiko kabisa cz haiwezekan mjakaz apewe sawa na familia, na wakadai mjakaz aliwauzia sehemu yake iliyopakan na shule, wanakijiji wenye upeo tunajiuliza je kwakua shule na kanisa ni wasomi kwanini walinunua shamba bila nyaraka? Inawezekanaje shamba ambalo lina lease liuzwe nusu yake, na baada ya kugundua kua lease ya yule mama ni valid tena ya miaka 99 walijaribu kumpa tena pesa je kama walikua na haki walikua wanampa pesa ya nini mjne, kwa nini kanisa linafanya nambo kienyeji? Hapa kanisa halichafuliwi bali tunajiuliza barua zote za kuhusiana na sakata hili zinasainiwaga na askofu mkuu wa moshi which means kanisa lipo busy kuchkua kipande hichi cha ardhi, nakiita kipande maana hili kanisa ni kubwa na linajitia aibu lenyewe na sisi waumin wake kwa jambo hili linalofanya. Mwalimu mkuu wa zamani ndg kisamo alimsumbuaga sana huyu mama kila mara polisi na vituko vingi lkn ilishindikana sababu ya hati ya shamba akamuacha, sasa huvu kuna mwalimu mkuh mpya ambaye ndo amelianzisha sakata upya, kwa mabavu aliingia na kuanza kujenga ukuta ktk hiyo sehemu ya nusu ya shamba, je huyu mwalimu ambaye ni mpya lazma atakua anapata maelekezo kutoka kwa mwajiri wake ambaye ni kanisa, na kama kanisa linadai kuuziwa huo upande ni kwa nini lilienda kujenga kisima kule karbu na nyunba ya mama john kama si uonevu? Mwl mkuu anamtishia mama jihn kua watamwamisha pale kabisa anapata wapi hii nguvu?? Kanisa acheni uonevu yule mama ana haki kabisa na wanakijiji wengi wanalitambua hilo
 
Back
Top Bottom