Nadhani ushauri mzuri kwa sasa ni kupeleka suala hilo katika baraza la ardhi au mahakama ya ardhi kwa usuluhishi. JF haiwezi kumpa haki huyo mjane wala wewe mwenyewe.sitafuti public sympathy mzee,hili swala linajulikana marangu nzima,iyo lease nitaiweka apa
sitafuti public sympathy mzee,hili swala linajulikana marangu nzima,iyo lease nitaiweka apa
Kwaiyo wewe ndo msemaji mkuu wa huyo mama.?
Unaonekana ni mwenye kuongea kwa ushabiki ukiomba public sympathy bila kujali kwamba unaweza kugundulika.
Uzoefu unanionesha kwamba wengi wa wanaoitwa wajane si watu wa kuwasikiliza upande mmoja na kufanya maamuzi. Ikiwa unahusika kwa kiasi hicho na hilo shauri, bila shaka ungetuwekea Lease ya hilo shamba (sio Liz) ili tujionee na si kuropoka km mama wa kiswahili.
Benteke kama unaijua hii habari mbona unaongea uwongo?mmoja wa mawakala nini ndugu yangu,Iyo shule ya marangu enyewe sio ya katoliki kiasili chunguza tuu,msitake tumwage kweli maana tutalidhalilisha kabisa hapa
Kanisa katoliki jimbo kuu la Moshi pamoja na shule yake ya sekondari Marangu bila aibu wala hofu ya Mungu wamuhubiriaye maana hi ni taasisi ya kidini wamemnyang'anya mjane shamba aliloachiwa na marehemu doctor Geovan Balletto.
Shamba hilo ambalo lina liz lipo jirani kabisa na shule ya Marangu inayomilikiwa na kanisa Katoliki, limekuwa likikaliwa na marehemu na familia yake na baada ya kifo chake mnamo 1972 alimuacha hapo mjane na mtoto wao.
Ndani ya shamba hilo kulikuwa na hospitali ambapo doctor huyo aliyekuwa mzungu raia wa Italy alikuwa akiwatibu na kuwasaidia sana wanakijiji wa Marangu na vijiji vya karibu akisaidiana na mjane huyu ambaye alikuwa nesi.
Pia kulikuwa na mazao pamoja na miti mingi na nyumba kubwa ya kuishi ambayo mpaka leo familia inaishi hapo,bila haya kanisa na taasisi yake bila ruhusa ya mjane huyo waliingiingia kwa nguvu kwenye shamba hilo na kukata miti mingi tuu na kujenga kisima.
Waliharibu mazao na kutandaza mabomba ya kupeleka maji shuleni kwao,kana kwamba hiyo haitoshi kanisa lilijitwalia eneo la ekari tatu hivi na kuanza ujenzi,mjane huyo alipouliza aliwekwa ndani kituo cha polisi HIMO.
Imekuwa kawaida kila hila na uonevu dhidi ya mama huyu mjane kutumika kwa polisi wa himo{RUSHWA KANISANI?}.
Hivi sasa kanisa linatumia nguvu kubwa ya fedha {sadaka} na hila ili wataifishe shamba hili ambalo lina liz na uhalali wote uliochwa na marehemu kwa familia yake,kanisa linafanya haya kupitia mawakala wake wakuu askofu mkuu Moshi pamoja na mwalimu mkuu Marangu sekondari ambaye kila kikicha anamtishia mama huyu maisha.
Je ni lini kanisa katoliki litaacha kuonea walalahoi na kwa kutumia sadaka zetu wenyewe?
Kupitia hapa tunaamini mama huyu atapata msaada kutoka kwa serikali,wanasheria,wanaharakati na watu mbalimbali hii ikiwa ni pamoja na ushahuri.
Benteke labda kwa mazoea tu ya jamii flani wakimuona mzungu wanaamini ni padre,ila huyu dr pamoja na mama mjane hawajawahi kuwa ivyo usemavyo,
Unafanya kampeni kanisa hili lifutwe kabisa serikali?una uhakika utafanikwa?anya mambo ya maana baba.
Benteke labda kwa mazoea tu ya jamii flani wakimuona mzungu wanaamini ni padre,ila huyu dr pamoja na mama mjane hawajawahi kuwa ivyo usemavyo,
Mama mjane anayo lease, na kama kanisa nalo linaamini wanayo lease yao hiyo ni double allocation.
Before the eyes of law wote tunajua the justice should be done and seen to be done.
Wote tunaelewa samaki mkubwa huwa anaamini kuwa anayo haki ya kummeza samaki mdogo ila kwa huyu mama hatuna budi kufatilia mashauri husika kwa karibu ili kuiweka wazi jamii ya wale wenye kujali haki,utu na ubinadamu wajue jinsi kanisa husika kama linatenda haki ama halitendi haki kwa mama husika.
Itakuwa ni aibu sana kama mabavu yatatumika ila naamini vyombo husika kuanzia land tribunal hadi mahakama vitazingatia haki ya huyu mama na pia vitazingatia kuwa kesi hii inatazamwa na level ya dunia na sio kijiji tena kama walidhani ni siri basi nawasihi tu wajue kuwa kesi hii itakwenda kuliabisha kanisa kama ubabe na outlaw acts zinazofanywa na kanisa zitaendelea dhidi ya mama huyu.