Kanisa katoliki nchini Malta labariki Ushoga

Kanisa katoliki nchini Malta labariki Ushoga

Kwani ukiristo ni nini, si kufuata mafundisho ya Yesu Kristo?

Wao ndio wametuletea ukiristo, tunapaswa kukubali maana kama walichomekea kuhusu mke mmoja sasa kwa nini wasije na wanaume kuoana. Kipindi wanaleta dini walijua sio rahisi kuwashawishi waafrika wakubaliane na ndoa zaa mashoga ila kwanza tuwachomekee mke mmoja, tumeingia kingi sasa wanakamilisha mkakati wao.
Ww acha kukariri Ukristo ulikuwepo Africa hata kabla ya Africanos jemedari wa kirumi hajapigana na Ethiopia Last millennium kama ulikua hujui ndiyo jina Africa ndipo lilipopatikana.Nenda Ethiopia kuna makanisa yanazaidi ya miaka 600 na kuendelea hivyo hivyo na Elitrea wazungu Africa wameanza kuja miaka ya 1600's na 1700's kabla yao wa fanya biashara wa Asia na waarabu.
 
Sijaona sehemu inayosema kanisa limekubali ushoga hapo., its one thing kutopingana na kitu na ni kitu kingine kabisa kukubaliana na kitu hicho
 
Kuna tatizo la lugha hapo, mleta mada kusema 'labariki ushoga' wakati alichoongea bishop ni tofauti inaonyesha kiingereza kilikuwa ni tatizo. Kuna tofauti kati ya mashoga na ushoga. Pia kuna tofauti kati ya kuwa shoga na kufunga ndoa ya jinsia moja.
 
Kanisa hili linalongozwa na papa Fransis au nilingine, misimamo ya kanisa iko waz, huyo askofu atakua ni Muasi
 
ushonga na kanisa katolik na ulaya ni vitu simultaneous....
 
Huyu ataisikia habari ya Papa mda sio mrefu
Atafukuzwa kama mbu
Upuuzi huu katu kanisa katoliki hautaukubali milele
 
Unaposema ufuska unafanyika kanisa katoliki unaji expose ulivo na akili ndogo. Ufuska ni dhambi ni katazo katika amri za Mungu lakini binadamu wote wanaanguka kwenye dhambi na kanisa katoliki linakemea mno ufuska mifano miwili
1. Ukiwa na kijana wako anaishi na mke au mume bila ndoa (kanisa linachukulia kuwa huo ni uzinzi) wewe mzazi huruhusiwi kushiriki sakrament hadi wanao wafunge ndoa
2. Ukizaa mtoto nje ya ndoa (ndani ya uzinzi) habatizwi hadi ufunge ndoa. Sijawahi kuona kanisa lolote la Kristu linalolinda ufuska labda haya makanisa yenu ya kishetani

Mkuu;
Pole sana sana. Hivi bado kuna watu wanaongozwa na sheria za kibinadamu?? Tena unaona furaha kabisa kujivunia?? Ni amri ya ngapi Mungu alisema kama mwanao, mtu mzima, amezini ati weye usishiriki sakrament?? Hivi inakuja akilini kweli?? Kwako mtu anakuwa mtoto hadi lini?? Weye bado unakula kwa mama?? Utoke kwetu Tarime, uende kufanya kazi Mtwara, huko ukutane na Mmakonde mchukuane huko mkazae watoto wenyu, mimi babako huku Tarime mninyime kushiriki sakramenti, hii inakuja??
Haya, kwako weye dhambi ni uzinzi tu baasi?? Wezi wa mali ya umma! Matapeli na waongo! Wasengenyaji na wanaotoa mimba! Jamani, Jilindeni nafsi zenu. Soma biblia ambayo ndiyo dira yako ya kukuongoza ile njia ya kwenda kwa Baba.
Ati ukizaa mtoto nje ya ndoa habatizwi. Huyo mtoto kosa lake ni kuzaliwa na huyo mzinzi au?? Weye ulichagua kuzaliwa?? Nadhani, wengi huko mnazini tu bila hata kujua. Unafungiwa ndoa na mtu asiye na mke bado unaamini kuwa kakufungia ndoa?? Yeye anaijua ndoa?? Atakufundisha nini kuhusu ndoa??
Naomba tuache haya maneno kwani yanaleta kichefuchefu
 
Haya basi tufanye hivi, weka hapa uthibitisho kuwa kanisa katoliki ni mafuska au mapunga, kama huwezi basi kauli zako hazima mashiko sepa tu

Mkuu;
Tumefika mahali pa kubishana bila sababu?? Mleta uzi amekuambia kuwa kanisa Katoliki kule nchini Malta limehalalisha ushoga. Amekuwekea na Picha za hayo Mapunga. Nimekuambia kuwa Kardinali Mtunza fedha (Treasurer) wa Roman Cotholic kule Vatican yaani makao makuu ya dini hiyo ameamriwa kurudi kwao Australia aende kujibu tuhuma za kuwalawiti watoto wa kiume na hapa sio mmoja bali wengi kule kwao. Kesi zinanguruma mahakamani hivi unapobishana huku JF. Unataka nini?? Jitahidi kupata habari mbali mbali zitakusaidia.
 
Malta Archbishop Charles Scicluna told a church community recently: "We are not against gays... But we do not need to change the way in which God created marriage to enable us to say that two men or two women can get married."
 
Sio kweli hizo ni propaganda za kuangusha ukatoliki

Nakumbuka kwenye mkutano wa juzi hapa wa makadinali wa Rc hilo suala halikupita na maaskofu walikataa kulizungumzia kwa msimamo kuwa ndoa kwa mujibu wa bible ni ya mwanaume na mwanamke tu...period
 
Mbona nackia kwenye nchi wanazooa wake wengi ndo wanapenda sana mchezo wa kudukua wanaume wenzao?
Kwa misheria ya kule wangekuwa wameisha kwa kuchinjwa wa kule wanatangazwa sana tu lakini kuna nchi vinara na ruksa Holland ,Denmark, Luxemborg, UK, USA na hazitangazwi kwa kuwa kwao si issue ya discussion !
Sasa humo ilipo insinuate kwa kuwa kuna marufuku ya thamani ya roho yako basi akitokea baradhuli anakuwa baradhuli wa kweli kweli si mchezo na lazima atatangazwa kwa kuwa kule nu kinyume na mila desturi na sheria ya nchi na imani zao!
 
Ni dini lao mnalamika nini?! Hata wakisema waabudu matako kwani kuna ubaya gani?! Ni dini yao..
 
Unaposema ufuska unafanyika kanisa katoliki unaji expose ulivo na akili ndogo. Ufuska ni dhambi ni katazo katika amri za Mungu lakini binadamu wote wanaanguka kwenye dhambi na kanisa katoliki linakemea mno ufuska mifano miwili
1. Ukiwa na kijana wako anaishi na mke au mume bila ndoa (kanisa linachukulia kuwa huo ni uzinzi) wewe mzazi huruhusiwi kushiriki sakrament hadi wanao wafunge ndoa
2. Ukizaa mtoto nje ya ndoa (ndani ya uzinzi) habatizwi hadi ufunge ndoa. Sijawahi kuona kanisa lolote la Kristu linalolinda ufuska labda haya makanisa yenu ya kishetani
Acha uongo we ndugu. Hakuna ukweli wowote kwenye hayo uliyosema.
 
Back
Top Bottom