KERO Kampuni Ya Mabasi ABC upper class Mnakera Sana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
hiz kampun kongwe huwa wanajikuta, mie nlishaacha kupanda kampun kongwe,, hizi mpya mpya zinajali sana wateja,,, nna basi langu pendwa , nawajua madereva wote, wahudumu wote,

nkitaka kusafiri napga simu tu, naekewa siti nzuri,, mastori kama kawa,, imefika hatua vimzigo vdogo vdogo nikitaka kulipia naambiwa kausha broO
 
Nina mpango wa kuwafungulia mashtaka. wamenikatia tiketi ya kieletronic nikatumiwa ujumbe kwenye simu kwa SMS bahati mbaya sikusoma SMS yote. Nimefika Dar napeleka madai kwa muhindi wangu ili anirudishie nauli yangu nakuta nauli imeandikwa TBR to Dar shs 100 (Mia moja) . Muhindi kagoma kunirudishia 50,000 niliyolipa akidai tiketi inaonyesha nimelipa sh 100.Nimeshaenda Latra wameniambia niende kesho. Shenzi sana hawa
 
Mmh naona siku yako ilikuwa mbaya.
Mbona haina matatizo kiasi hicho?

Nimesafiri nayo sana..sema kuna siku Dereva alisinzia akatupeleka porini
 
Wewe boya ndio utakuwa ni chawa wa ABC na ndio maaana umekuja kutetea kwa suala ambalo lipo wazi.
Kuwa na adabu kutukana tukana watu mtandaoni utakuja kumtukana kibenten wa mamaako.
 
kila la heri ipo siku na nauli utaambiwa kausha.
 
Mkuu ilinitokea nikadhani labda ni bahati mbaya, tulitakiwa kwenda Dodoma saa 4 mpaka saa 6 hatujaondoka, simu unapiga inaita tu bila kupokelewa. Ingawa mabasi yao yana ubora.
 
Mmh naona siku yako ilikuwa mbaya.
Mbona haina matatizo kiasi hicho?

Nimesafiri nayo sana..sema kuna siku Dereva alisinzia akatupeleka porini

Siku zote ambazo nimesafiri nao usiku, siku zilikuwa mbaya

Last week wametuweka manzese mpaka saa sita kasoro, wakati gari ilitakiwa kuondoka saa 4

Unafika moro hotelin saa nane, noo food no anything yet wanaenda kuweka mafuta tunakaa tena Pale 45mn
 

Biasha inayotoa Huduma ya usafiri ikikosea mwenye departure time, itatoka kwenye Biashara siku si nyingi,
 
Kuna siku nilienda kutuma mzigo kwenda iringa aisee nilijuta ABC kuna jamaa alonipokea alikuwa anajibu ovyo kama vile ule mzigo nilikuwa natuma bure for sure nilighairi palepale na baadae kuna mmoja wa staff wa pale akanambia yule ndiyo mtoto wa boss na ndiyo alivyo aisee jamaa anakera na kama ni kweli basi kuna uwezekano hata haya yanayoendelea ni sehem ya majukumu yake ila ilikuwa kampuni yangu pendwa sana.
 
Usipokuwa makini kwenye biashara yako, wakukuangusha au kufanikiwa ni waajiriwa. Lazima uwe makini sana sana
 
Unasafirishwaga bure? au huwa unashikiwa mtutu wa bunduki kupanda hayo Mabasi? Hivi huu ujinga wa uzezeta utatutoka lini?
 
Kuna siku nilimkatia mke wangu ticket kwenda dodoma kutoka dar es salaam, kwanza lilichelewa sana kuja cha pili gari halikuja lile nililokata(lilikua linaenda singida) na lilikua gari bovu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…