Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,595
- 19,498
Kuna siku moja rafiki yangu mmoja alikwenda harusini akiwa amevalia vizuri sana tena alivyokuwa na pamba za uhakika kila mtu alisema kweli jamaa yule kapendeza sana. Halafu kumbe jamaa alikuwa na nafasi fulani kwenye ukoo wa maharusi, kwa hiyo alipata nafasi ya kutoa nasihi zake. Jamaa yule alitoa hotuba nzuri sana yenye maadili mazuri sana kwa maharusi na watu wtote waliokuwapo pale. Mojawapo ya maadili lilihusu maharusi kujiheshimu ili waweze kuheshimiwa na wengine.
Baada ya hotuba ile, jamaa akabugia pombe mpaka akajisadia kwenye nguo pale pale ukumbini na kulala chini akiwa hoi bin-taabani huku uharo wake ukiwa unasambaa hovyo hovyo hadi ikabidi sherehe ya harusi ifungwe.
Kesho yake gumzo lilikuwa jinsi jamaa huyo alivyojisadia kwenye nguo na kuzidiwa na pombe hadi akalala chini ukumbini huku akiwa na kinyesi kwenye nguo zake. Hakuna aliyekumbuka kuwa alikuwa jamaa alikuwa amevalia nguo nzuri na alikuwa ametoa maadili mazuri.
Inawezekana kweli Lowasa aliwahi kufanya mambo mazuri ikiwa ni pamoja na kukemea uuzwaji wa viwanja kiholela pale Dar, na kuhusu matumizi ya maji ya Ziwa Victoria. Hata hivyo, uharo wa rushwa aliolalia kwenye nguo ndio signature identity yake na wala hatutaisahau hata akijisafisha vipi. Kwa sasa hivi tunafahamu kuwa hata vile viwanja alivyokuwa akikemea uuzwaji pale Dar, baadaye vilikuwa uzwa na alipokea rushwa. Kila jambo afanyalo jamaa huyu huwa liko kalikulatedi kumpa ulaji fulani binasfi, siyo kwa maslahi ya taifa. Swala la maji ya Ziwa Victoria lilikuwa kalikulated kumfanya aonekane mchapa kazi ili aweze kuwania ama urais au nafasi kubwa zaidi serikalini.
Baada ya hotuba ile, jamaa akabugia pombe mpaka akajisadia kwenye nguo pale pale ukumbini na kulala chini akiwa hoi bin-taabani huku uharo wake ukiwa unasambaa hovyo hovyo hadi ikabidi sherehe ya harusi ifungwe.
Kesho yake gumzo lilikuwa jinsi jamaa huyo alivyojisadia kwenye nguo na kuzidiwa na pombe hadi akalala chini ukumbini huku akiwa na kinyesi kwenye nguo zake. Hakuna aliyekumbuka kuwa alikuwa jamaa alikuwa amevalia nguo nzuri na alikuwa ametoa maadili mazuri.
Inawezekana kweli Lowasa aliwahi kufanya mambo mazuri ikiwa ni pamoja na kukemea uuzwaji wa viwanja kiholela pale Dar, na kuhusu matumizi ya maji ya Ziwa Victoria. Hata hivyo, uharo wa rushwa aliolalia kwenye nguo ndio signature identity yake na wala hatutaisahau hata akijisafisha vipi. Kwa sasa hivi tunafahamu kuwa hata vile viwanja alivyokuwa akikemea uuzwaji pale Dar, baadaye vilikuwa uzwa na alipokea rushwa. Kila jambo afanyalo jamaa huyu huwa liko kalikulatedi kumpa ulaji fulani binasfi, siyo kwa maslahi ya taifa. Swala la maji ya Ziwa Victoria lilikuwa kalikulated kumfanya aonekane mchapa kazi ili aweze kuwania ama urais au nafasi kubwa zaidi serikalini.