Kampeni ya kuikataa Vodacom

Habari zenu wana wa nchi na poleni kwa majukumu mbali mbali ya ujenzi wa taifa.
Baada ya tafakuli ya kina juu ya tukio la kukamatwa Mwandishi Erick Kabendera jana na Kufungiwa huduma ya mawasiliano ya simu yake na Vodacom nimeoma kuna mambo kadhaa yana tia simanzi sana juu ya Usalama wa raia yeyote kwa sasa hapa nchini.

Mwandishi Erick Kabendera anasema alipoona Mawasiliano yake yamefungwa aliwapigia vodacom na kuwauliza kulikoni? Vodacom wakamjibu kuwa wameagizwa na TCRA wafunge mawasiliano yake. Lakini baadae TCRA ambao ndio wenye jukumu la usimamizi wa Mawasiliano wakakanusha kuwa hawahusiki na tukio hilo na wala sio kazi yao kufungia watu mawasiliano.

Majibu ya TCRA yanatupa maswali magumu juu ya Mtandao wa Vodacom kama ifuatavyo.

1. Kwa nini Vodacom wanawaficha wahusika halisi waliotoa amri ambayo kama waliona ni halali?
2. Lengo halisi la kufunga mawasiliano ya mwandishi ni nini? Ili akitekwa asipatikane hewani na kuwasiliana na ndugu zake?

3. Kama mtuhumiwa anatafutwa na chombo cha usalama SIMU yake ikiwa hewani husaidia chombo cha usalama kujua mahali alipo na kumkamata kirahisi. Sasa Hawa Vodacom kumzimia Simu mtuhumiwa anaye tafutwa wana LENGO gani?

4.Makosa anayotuhumiwa Kabendera hayahusiani na mambo ya Mawasiliano kwa nini Vodacom wamfungie huduma mteja wao ambaye amelipia huduma?

Maswali haya yanatuonesha Vodacom sio Mtandao salama tena kwetu watanzania. Unashirikiana na wahalifu, watekaji, wauaji, na watesaji hapa mchini.

Pili Vodacom wameonesha dharau kubwa sana kwetu watanzania. Kama wanaweza kukufungia Mawasiliano mtu ambaye huna hatia ili udhurike na watekaji watashindwa kuvujisha habari zako?

Je, Pesa zetu tunazo ziweka huko M.PE.SA ni salama tena? Huwezi amka ukaambiwa akaunti yako imefungwa na pesa zako zimechukuliwa kwa maagizo toka juu?

Kitendo hiki hakipaswi kufurahiwa. Vodacom wanapaswa kuchukuliwa hatua na sisi wenyewe wananchi ili kulinda usalama wetu na kuwaonesha kuwa tumefedheheshwa sana na tukio hili.

Hatua za kuchukua ni hizi wana bodi.
1. Kuacha kutumia mtandao wa Vodacom na mitandao mingine kama hiyo inayo shirikiana na waharifu kutesa raia wema.

Vodacom wamejidhihirisha pasi na shaka kuwa ni hatari kwa usalama wetu hima hima tuchukue hatua haraka.
Asanteni.
 
Eti Tuikatae voda wewe na nani
Na mtandao upi Utumie labda hama nchi
Ukafanye kinyume na utaratibu lakini Hakuna sehemu utakimbilia ukawa salama kama wewe ni mvunjifu wa sheria na taratibu wa Nchi
Wapumbavu hawatokaa waishe.. Sheria gani imevunjwa?? Vodacom ni lazima kuitumia?? acha kuwaza kupitia makalio dada!
 
Tunawahukumu Voda bure bila tafakuri... Mitandao yote inadakuliwa ni swala la muda tuu
 
 
Kumbe regime inapingwa hivi![emoji2][emoji2] Basi sawa. Kila heri mtetezi wa wanyonge.

Na wewe you should!

Mnyonge asie na nguvu anaonewa,anakua bullied sababu tu ni mwandishi wa habari lazima atetewe na wote!

Hata kama ni sheria,sheria most often times ni favourable kwa watawala na sio wanyonge!

Mtu unamnyima mnyonge kufanya kazi yake halali kutokana na weledi wa taaluma yake kuisaidia familia yake kama wewe na mimi na huyo mwenye madaraka!

Wanyonge ni lazima wawe centre of everything!Watumiwe kama yardstick ya ku-improve maisha na comfort kwa wanadamu wote!

Sio regime na watawala wenye priveledge ya kila kitu!
 
Ni kweli kampuni yoyote ya simu inayotoa mawasiliano ya mteja wake bila ridhaa yake ni kinyume cha sheria

Lakini kwa upande mwingine tujiulize ni sheria ngapi zimevunjwa toka utawala huu was awamu ya tano uingie madarakani??

Jibu ni nyingi, ambazo hazina hesabu

Huo ndiyo mwelekeo wa seeiakali yoyote yenye mwelekeo wa kiidikteta
 
Pumbavu! Hii nayo mtaishia patupu kama kipindi kile.

Sikia, watu hawatumii Voda sababu Lema au Msigwa au Mbowe kasema tumieni, Bali wa natumia voda sababu ya huduma zao,

Huduma zao ndio zitakazoamua uitmuie au laa!

Wakati mwingine tumieni akili.

Hujui lolote!

As we speak Tigo has overtaken Vodacom in every statistical category,go and check!

Na pia sio lazima wananchi wahame Vodacom manually kama unavyodhani!

Hapo ndio unapo-miss the whole point!

The aim ni chuki ya moyoni ya brand name Vodacom!

Brand name Vodacom tayari ishapata damage already!

Ishakua ni symbol of oppression tayari!Damage has already been done,permanently!

Vodacom brand ilikua ni symbol of excellence,integrity,simplicity,etc.Sasa hivi as we speak Tigo has taken all that!

Hakuna haja ya watu kuhama!Hiyo ndio unayotegemea which is wrong observation na kuicheck hii ishu kijuu juu kama kawaida yenu!

Vodacom=Oppression!

Ishapakwa mavi tayari!

Na kibaya zaidi wananchi hua hawasahau,2025 regime itakua haipo Voda itakuwepo na subscribers watakua hawaongezeki kama sio kupungua!

Na trust me,as we speak,new lines Vodacom zinazotoka kila siku zimepungua compared to jagganauts like Tigo!

New subscribers sahauni!

Vodacom is eating its own shit!
 
Kwani hujui kuwa mwenye shares nyingi Vodacom ni Rostam Aziz??

Kutokana na ukaribu alionao huyo jamaa kwa jiwe, tegemea chochote hapo
 
Bora uwambie, watz tuna shida sana, wanafikiri huko kwingine kuna usalama, mi sielewi watu wanawaza kitu gani.

Wakitaka chochote hamna cha voda, tigo ,airtel, halotel ,zantel ,ttcl kama kunanyingine mtaongeza. Watapata tuu Inategemea mlengwa yupo wapi (mtandao upi)
 
Hawa inabidi tuwaadhibu kwani "uwezo tunao, sanabu tunayo na nia tunayo" hakuna atakaye tulazimisha kutumia mtandao wao.

Hawa kwa mwezi nawachangia si chini ya laki 2, kwa nini wanatufanyia hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…