Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,650
- 218,105
Ikiwa kama umechoshwa na unyama unaotendwa dhidi ya binadamu nchini Tanzania ( RIP Lwajabe , pole Lissu ) , na ikiwa kama unakerwa na dhuluma dhidi ya wakulima , ikiwa unakerwa na rushwa na ikiwa kweli wewe ni mcha Mungu basi wakati wako wa kutenda kwa kadri ya maandiko Matakatifu umefika , pinga umasikini kwa kuikataa ccm na kuichagua Chadema , jiwekee akiba mbinguni kwa kuwakataa watekaji na wabambika kesi , kataa uonevu dhidi ya wananchi wa Tanzania .
Mungu anakuona unavyoteseka na amekuona ulivyo na Subira , sasa amekuletea Chadema na washirika wake ili ukombolewe dhidi ya Maisha ya kishetani ambayo ccm imejiapiza kuwapa wananchi , muda ni huu acha kulia lia , kura ni siri yako , ipige vizuri ili kumtukuza Mungu kwa " Ufufuo " wa Tundu Lissu ubarikiwe .
Nchi hii imebakisha wiki chache sana ili kuondokana na utumwa , dhiki , uonevu , ukosefu wa ajira , mishahara duni , ufisadi , utekaji , makanisa na misikiti kutumika , hofu , mateso , dharau , matusi , wizi , ada ya kuzaa , elimu duni , uonevu wa Masheikh wa Uamsho pamoja na mambo yote mabaya yaliyofichwa , mwenye maamuzi ni wewe , ikatae ccm ili tujue waliko waliopotea , ikatae ccm ili tuwajue watekaji , ikatae ccm ili chini ya mwezi mmoja tuyajue majina ya waliomshambulia Lissu na waliowatuma .
CHAGUA CHADEMA KWA UHURU , HAKI NA MAENDELEO YA WATU.