CAPO DELGADO
JF-Expert Member
- Aug 31, 2020
- 9,764
- 20,456
Afisa Habari wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe akamatwa usiku wa manane huko Tabora.
Chanzo cha Kukamatwa kwake ni kutoa Lugha chafu kwa viongozi wa Mkoa.
Ameshikiliwa kwa Mahojiano Maalum.
RPC Tabora amethibitisha
“Nathibitisha tunamshikilia Msemaji wa Yanga, Ali kamwe, tunamshutumu kwa kutoa kauli mbaya dhidi ya viongozi wa Serikali, tunaendelea na mahijiano nae na tutatoa taarifa,” Richard Abwao - Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora.
==================
Polisi Mkoani Tabora imethibitisha kumshikilia Afisa habari wa Yanga Ali Kamwe.
Kamanda wa Polisi Tabora Richard Abwao amethibitisha kushikiliwa kwa Ali Kamwe na Polisi huku tuhuma zake zikitajwa ni kutoa lugha chafu kwa viongozi wa Serikali.
Kamwe alikuwa na timu yake ya Yanga Tabora kwa mchezo dhidi ya Tabora United ambayo ilimalizika jana kwa Yanga kushinda mabao 3-0.
Kabla ya Mchezo Kamwe anatajwa kuzozana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh. Paul Matiko Chacha katika kile kilichotajwa kuwa alikuwa akijibu alichosema RC huyo kuwa Yanga wamekuja na kiherehere mkoani mwake.
Ali Kamwe kushoto akiwa na RC Tabora
Chanzo cha Kukamatwa kwake ni kutoa Lugha chafu kwa viongozi wa Mkoa.
Ameshikiliwa kwa Mahojiano Maalum.
RPC Tabora amethibitisha
“Nathibitisha tunamshikilia Msemaji wa Yanga, Ali kamwe, tunamshutumu kwa kutoa kauli mbaya dhidi ya viongozi wa Serikali, tunaendelea na mahijiano nae na tutatoa taarifa,” Richard Abwao - Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora.
==================
Polisi Mkoani Tabora imethibitisha kumshikilia Afisa habari wa Yanga Ali Kamwe.
Kamanda wa Polisi Tabora Richard Abwao amethibitisha kushikiliwa kwa Ali Kamwe na Polisi huku tuhuma zake zikitajwa ni kutoa lugha chafu kwa viongozi wa Serikali.
Kamwe alikuwa na timu yake ya Yanga Tabora kwa mchezo dhidi ya Tabora United ambayo ilimalizika jana kwa Yanga kushinda mabao 3-0.
Kabla ya Mchezo Kamwe anatajwa kuzozana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh. Paul Matiko Chacha katika kile kilichotajwa kuwa alikuwa akijibu alichosema RC huyo kuwa Yanga wamekuja na kiherehere mkoani mwake.
Ali Kamwe kushoto akiwa na RC Tabora