Swash Bizo
Senior Member
- Jan 29, 2011
- 141
- 93
Kila jambo na mwisho wake....
Kipengele a ndio kinahusika, kwani kamAti za Bunge zinaundwa kwa mujibu wa kanuni na huwa zinaundwa upya kila baada ya miaka miwili na nusu ya uhai wa Bunge, so zilipaswa kuundwa upya , ila la kuifuta kamati ya POAC hoja ya spika leo ilikuwa hakuna bunge lolote duniani ambalo lina kamati kama hiyo, ila kamati ya hesabu za serikali ndio ipo na inakagua pamoja na mashirika ya umma kwani ni sehemu ya serikali hayo mashirika.
Ila kiuhalisia Spika amevunja kanuni kwani kamati ya POAC imeundwa kwa mujibu wa kanuni, yaani imetajwa na kanuni kuwa itakuwepo, hivyo alipaswa kuleta hoja ya kurekebisha kanuni kwanza ili Bunge liamue ndipo aweze kuifuta hiyo kamati , na sio kama alivyofanya.
Kamati nyingine hazijatajwa kwenye kanuni kama zilivyo za POAC, PAC NA LAAC , ndio maana Spika amepewa uhuru wa kuunda kamati kadiri atakavyoona inafaa kwa mujibu wa kanuni.
Zitto atapata wapi jukwaa la kueneza uongo wake
Taarifa zako ni za zamani sana , soma kanuni ya 113 , ujue kuwa mawaziri na manaibu sio wajumbe wa kamati za Bunge, hivyo Simbachawene na Kairuki sio wajumbe.
Pili , ukisoma hiyo kanuni utajua nani mwenye mamlaka ya kuunda , kamati kazi yake ni kumshauri na sio kuunda , mamlaka ya kuunda ni ya Spika.
Aidha , ukisoma kanuni hiyo ya 113 kifungu cha 11 utaona kuwa kamati zilizotajwa kwa majina kwenye kanuni ni tatu nyingine anapanga Spika kadiri atakavyoona inafaa..........
mkuu,
Nimekupata.
Hebu tujaribu kupambanua hili neno KUMSHAURI. Hudhani hata kuunda kamati hizi lazima kuna ushauri aliopata kutoka kwa hawa wajumbe wa kamati ya kanuni. Na kama sivyo, kwa nini hajitokezi hata mjumbe mmoja katika kamati hiyo na kutoa dukuduku lake kuhusiana na hilo.
Ushauri unaweza kupokelewa ama kukataliwa.....
Naomba uweke hiyo kanuni ya 113 yote kama ilivyo li kusaidia kupanua wigo wa mjadala...
EMT, bahati mbaya device ninayotumia kwa sasa haiwezi kukopy na kupaste, ila naomba mwenye kanuni za Bunge aweke kanuni yote ya 113 , itasaidia sana wengi kupata mwanga , hada wale ambao wana nia ya kujifunza.
Pili, POAC ilikuwa kamati ya kudumu ila maisha yake ni miaka miwili na nusu na inaundwa upya kama zilivyo kamati nyingine, ila ninachosema ni kuwa kamati tatu za mahesabu zimeundwa kwa kutajwa majina na kanuni, sasa kuziondoa ni lazima ufute kwenye kanuni kwanza, pili hata kifungu cha sheria ulichonakili hapo ndio ambacho kimefutwa leo na kubadilishwa, hivyo serikali na Spika walishakubaliana kuifuta POAC ndio maana kifungu kipya hakikutaja tena hizo kamati, so huu ni mkakati wa serikali kwa kushirikiana n Spika.
Wabunge wanapaswa kumbana huyu mama hapo, kuwa sheria ilitangulia na yeye baadae kaja kutamka tuu...
wa ccm ni 9+2cuf dhidi ya 3 upinzani sasa matokeo yake unategemea nini?
Liandikwalo, ndilo liwalo!. No one can stop, destiny!.Mimi nakuelewa kwani una hasira kuwa Kamati ya mtu wako imevunjwa na kupunguziwa mamlaka ya kujua nini kinaendelea kwenye masuala ya ulinzi na usalama, .....
Nimekupata Mkuu. I hope atakayekuwa na hizo kanuni ataziweka hapa though umeshafafanua vya kutosha.
Kama kifungu cha 38(1) cha Public Audit Act 2008 kimefutwa, inaonyesha wazi kuwa kulikuwa na "conspiracy" kati ya serikali na sehemu fulani ya bunge kuitumbukiza POAC baharini.
Inaonyesha wazi kabisa kuwa maamuzi ya kuifuta POAC yamefanywa na serikali na siyo kamati ya Kanuni. Kamati imetumika kama tuu rubber stamp ya maamuzi yaliyokwishafanywa na serikali kuitokomeza POAC.
Lakini nimeshangaa sana kwamba wakati wabunge hasa wa upinzani na wale walioko POAC wanapitia Mswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Mwaka 2013, kweli kabisa hawakuona na kuhoji kwa nini POAC inaondolewa kama moja ya Parliamentary Oversight Committees under the Public Audit Act 2008?
Kweli tuna wabunge.
mkuu,
Nimekupata.
Hebu tujaribu kupambanua hili neno KUMSHAURI. Hudhani hata kuunda kamati hizi lazima kuna ushauri aliopata kutoka kwa hawa wajumbe wa kamati ya kanuni. Na kama sivyo, kwa nini hajitokezi hata mjumbe mmoja katika kamati hiyo na kutoa dukuduku lake kuhusiana na hilo.
Kwanza kifungu kinasema chochote kuhusu koramu?
Kushauri kama kawaida ya sheria zetu nyingine, spika ndiye atakuwa na maamuzi ya mwisho au discretion.
Ushauri unaweza kupokelewa ama kukataliwa.....
Naomba uweke hiyo kanuni ya 113 yote kama ilivyo li kusaidia kupanua wigo wa mjadala...
Koramu imetajwa kwenye kanuni nyongeza ya nane , nyongeza hii iwekwe yote then mjadala utakuwa guided vizuri.....
Kanuni zenyewe ndizo hizi hapa au zimeshakuwa updated? https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...jukumu-yake-muongozo-wake-na-muundo-wake.html