Mkuu nimekupata.
kila kamati ina majukumu yake lakini maajukumu ya jumla ni haya,
4.0 MAJUKUMU YA MSINGI NA YA JUMLA YA KAMATI
4.1 Kwa mujibu wa mgawanyo wa Mamlaka kama ilivyoainishwa katika vifungu vilivyotangulia, Bunge na Kamati zake za Kudumu hufanya kazi za kusimamia Utendaji wa Serikali kwa niaba ya Wananchi.
Bunge na Kamati zake ndiyo darubini (Oversight or Watch-dog organ) ya kuhakikisha kwamba mambo yote ya uendeshaji wa kazi za Dolaunafanywa kwa kuzingatia Katiba, Sheria na Kanuni zilizowekwa.
Kwa hiyo, kuna majukumu ambayo hutekelezwa na Bunge lenyewe nabaadhi ya majukumu ambayo utekelezaji wake ni wa siku hadi siku yanashughulikiwa na Kamati za Kudumu.
7
4.2 Kila Kamati ya Kudumu ina majukumu ya msingi na inalo jukumu la jumla la kufuatilia utekelezaji wa Ahadi za Serikali zilizotolewa Bungeni ambazo zinagusa mambo yaliyo katika Mamlaka ya Kamati inayohusika. Aidha, Kamati inaweza kupendekeza kwa Spika nyongeza ya majukumu ambayo yatajitokeza katika kutekeleza majukumu ya msingi. Kwa upande mwingine, Spika anaweza kukabidhi jambo lingine lolote kwa Kamati yoyote kama atakavyoona inafaa, kwa ajili ya kushughulikiwa na Kamati hiyo, kwa mujibu wa
Kanuni za Kudumu za Bunge Kanuni ya 90(1) na (2).