Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,697
- 164,972
Hapo Zitto ndio wamemmaliza!
Pili, maamuzi haya ya spika - ya kupora mamlaka toka kwa wananchi - yamekuja sambamba na hoja iliyowasilishwa na serikali ya kunyang'nganya (tena) watanzania - kupitia kwa wabunge wao - mamlaka ya kupokea na kuchambua taarifa za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali!
Jana akitoa lecture at Harvard Kennedy School CAG wa India rebutted criticism that the official auditor was exceeding its mandate.
Akasema maintaining that the auditing of government and public entities has a positive impact on trust in society: "It focuses the minds of the custodians of the public purse to use resources effectively."
Read more at:I am no rubber stamp, CAG Vinod Rai warns UPA during Harvard speech : North, News - India Today
Sisi tunaenda completely the opposite.
Hiki kikao cha bunge mwezi huu kimeisogeza CCM mbali kabisa na wananchi. Bunge limegeuzwa kuwa rubber stamp, kanuni zimekiukwa, hoja za msingi zinakataliwa, na funga kazi AG anakuja na marekebisho ya sheria ambayo itasambaratisha taifa! Crisis!
kwa kweli sijui ila kama sikosei yeye ndiye alivunja kamati ya nishati, kitabu changu cha kanuni za bunge sinacho hapa
Mkuu hizi kamati ni mzigo kwa nchi kwani wajumbe wa hizi kamati wengi wao ni watupu kichwani
hapo bado sijapata mantiki.
Tunahitaji nyama zaidi kwenye hii thread ili kujiridhisha na maoni yetu, hasa sababu za kufutwa ziwekwe wazi hapa ili tujadili bila hisia
Ninadhani hii transparency wanayoificha, kuna kitu wanataka kukifanya ninahisi wanataka kuchota pesa za kampeni toka kwenye Mashirika ya umma kama NSSF, LAPF, GEPF,PSPF, PPF na NHIF!! ili wasije kuulizwa peso hiyo imekwenda wapi!! Watch out Tanzanians!!
Mikael,
Kwa mfumo tulio nao sasa, wananchi wanaisimamia serikali kupitia kwa wawakilishi wao, yaani wabunge. Kamati za bunge zinafanya kazi kwa niaba ya wananchi ikiwa ni pamoja na kuidhinisha mapato na matumizi ya fedha, na kukagua mwenendo wa matumizi hayo.
Alichokifanya spika (kuvunja kamati inayosimamia mashirika ya umma), ni kunyang'anya wananchi mamlaka ya kuisimamia serikali kupitia bunge. Huu ni uhaini. Hili ni moja.
Pili, maamuzi haya ya spika - ya kupora mamlaka toka kwa wananchi - yamekuja sambamba na hoja iliyowasilishwa na serikali ya kunyang'nganya (tena) watanzania - kupitia kwa wabunge wao - mamlaka ya kupokea na kuchambua taarifa za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali!
Nini tafrisiri yake?
Serikali haitaki kabisa 'usumbufu'. Hawataki kuulizwa wala kufuatiliwa kwenye utendaji wake ikiwa ni pamoja na kukaguliwa kwa matumizi ya kodi ya watanzania. Kwa sasa watanzania kujua matumizi ya kodi yao itakuwa ni 'fadhila' toka kwa rais.
Na huu ni mkakati wa kamati mpya wa kamati ya CCM chini ya Mangula, Kinana na Dr Asha Migiro, wa kuondoa 'transparency' kwenye governance system Tanzania. Kelele tulizozikia kule Addis Ababa, kwamba Tanzania imefanya vizuri kwenye utawala bora, ilikuwa ni ujenzi wa uzio ili wakifanya huu uharamia dunia isijue! Na hapa ndipo watanzania wanatakiwa kuwa macho zaidi.
lli kuokoa hii nchi na balaa linaloinyemelea basi 2015 ni vema bunge lisiwe dominated tena na wale wale walioruhusu 'uporwaji' huu wa haki ya wananchi kuisimamia serikali.
Kuhusu bunge
Kwa sasa hivi Tanzania hatuna bunge. hatuna! Tuna idara ya serikali inayokaa Dodoma -mara kadhaa kwa mwaka- ambapo wabunge toka vyama vingine wanaruhusiwa kuingia lakini kuongea inategemea mkalia kiti kaamka vipi siku hiyo. Hatuna bunge. Na kama kuna mtu amerudisha hii nchi nyuma, basi Makinda anaongoza. Makinda atakumbukwa kwa kuuwa Demokrasia Tanzania. Hili halina ubishi. Na huko tunakokwenda, ni mungu mwenyewe anaweza kuinusuru hii nchi na mabalaa yanayopaliliwa na huyu mama. Very unfortunate.
Kamati ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje, iliyokua inaongozwa na Edward Lowassa imevunjwa na kuundwa kamati mbili ya Ulinzi na Usalama na ingine ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma ya Zitto Kabwe, imefutwa kabisa.
Zaidi baadae
Yaaani sijaelewa hata kinachoendelea bungeni kupitia thread hii yaani ni matusi matupu kiasi kwamba haieleweki