BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
Amesema, Kamati ya Bunge imejulishwa kuwa Ujazo wa Maji umefikia Kina cha Mita 167 kutoka usawa wa Bahari, kiasi kinachoruhusu kuanza Uzalishaji wa Umeme na Mtambo wa Kwanza utawashwa Februari 16, 2024, wa Pili utawashwa Machi 2024 ambapo Megawati 470 zitaingizwa kwenye Gridi ya Taifa.
Kuhusu hali ya Umeme hadi kufikia Desemba 2024, uwezo wa Mitambo ya Kufua Umeme kutoka Vyanzo mbalimbali ulikuwa Megawati 1,889.84 ikiwa ni ongezeko la Megawati 195.29 kutoka Megawati 1,694.55 zilizokuwepo mwaka 2022.
Hata hivyo, Uzalishaji wa Umeme nchini bado ulikuwa chini ya Wastani wa Megawati 1,200 wakati Mahitaji ya Umeme ni Wastani wa Megawati 1,482.80, hali inayosababisha upungufu wa Nishati hiyo nchini kote kwa Megawati 283.