Iringa: Kina cha Maji Bwawa la Mtera chapungua na kuathiri uzalishaji Umeme

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,120
1694318274340.png

Kina cha maji cha Bwawa la Mtera, Mkoani Iringa kimepungua na hivyo kupunguza Uzalishaji wa umeme kutoka megawati 80 mpaka 72.

Hayo yamebainika leo Septemba 9, 2023 baada ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kutembelea bwawa hilo ili kuona uzalishaji wa umeme.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Ussi Salum amesema uvumi kuwa baadhi ya watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kufungulia maji bila utaratibu na hivyo kusababisha upuugufu wa maji ya kuzalisha umeme sio wa kweli.

"Tumeridhika na uzalishaji wa umeme, kwa sasa kina cha maji kimepungua kwa sababu ni kipindi cha kiangazi, mvua ndio ambazo zinajaza Bwawa la Mtera na hivyo kusaidia uzalishaji Kidatu," amesema Salum.

Amesema lengo la ziara hiyo ni kujionea hali halisi ya uzalishaji umeme kwenye vyanzo vya maji vya Mtera, Kidatu, na Kihansi na kujipanga iwapo mvua za kiwango cha juu zitanyesha kama ilivyotangazwa na mamlaka ya hali ya hewa hivi karibuni.

Katika bwawa hilo, mashine zote mbili zina uwezo wa kuzalisha megawati 72 huku kila moja ikizalisha megawati 38.

Mkurugenzi wa Uzalishaji Umeme kutoka Tanesco, Pakaya Mtamakaya amesema mashine hizo zinauwezo wa kuzalisha mpaka megawati 80 kina cha maji kinapojaa.

Amesema watahakikisha umeme unaendelea kupatikana licha ya bwawa hilo kupungua kiwango chake cha maji kutokana na uhaba wa mvua.

"Kawaida huwa tunapata mvua mara mbili kwa msimu na iwapo msimu ukichelewa husababisha uhaba wa maji, lakini hauathiri upatikanaji wa umeme kwani kuna vyanzo mbadala vya uzalishaji," amesema.
 
Za chinichini zinasema maji ya Bwawa la Mtera yalifunguliwa kumwagika mwezi machi 2023 ili Bwawa lisibomoko, pamoja na ushauri wa wataalamu kuwa yasifunguliwe, inasemekana wakubwa walisisitiza yafunguliwe yamwagike. Je haya ni kweli? Kama ni kweli nini lengo la wahusika? Na kwanini wasishitakiwe Mahakamani kwa hujuma?
 
Za chinichini zinasema maji ya Bwawa la Mtera yalifunguliwa kumwagika mwezi machi 2023 ili Bwawa lisibomoko, pamoja na ushauri wa wataalamu kuwa yasifunguliwe, inasemekana wakubwa walisisitiza yafunguliwe yamwagike. Je haya ni kweli? Kama ni kweli nini lengo la wahusika? Na kwanini wasishitakiwe Mahakamani kwa hujuma?
Yalifunguliwa ili kisingizio kiwepo watu waingie mkataba nyonya damu
 
Mwenye majibu ya maswali haya naomba anisaidie
1) Ile GESI ya kutoka Mtwara kuja Kinyerezi Dar imeishia wapi? Si tuliambiwa kwamba sio tu itaondoa tatizo la umeme bali pia bei ya umeme itashuka?

2) Hivi unadhani viongozi wetu (Rais, Mawaziri, Makatibu wakuu, Wakuu wa Mikoa/Wilaya, Wakurugenzi wa mashirika na taasisi za umma, Wabunge, Mabalozi, n,k) wanaathirika na tatizo la umeme? Kwamba inawezekana kweli wakalala bila umeme kwenye makazi yao? Inawezekana kwelie asiyeathirika na tatizo husika akawa na moyo na utashi wa kutafuta utatuzi wa tatizo hilo? Yaani, mgao uwepo au usiwepo mimi kwangu sitakosa umeme, unadhani nitahangaika kutafuta ufumbuzi wa umeme?

3) Hii si mara ya kwanza wala ya pili, hata mwaka jana, mwaka juzi kusikia kwamba kuna upungufu wa uzalishaji wa umeme kutokana na kupungua kwa maji, kwanini tatizo hili linajirudia wakati viongozi wapo na ni wale wale? Waliopewa majukumu ya kutuongoza kweli wana maono na dira ya tunakukwenda?

Natafakari tu, lakini kama kuna mwenye majibu ya maswali haya nitashukuru kama atanisaidia
 
Sizani inawezekana hayamabwa yamejaa matope ndomanakinakinakua Kidogo nahakuna sevisikwenyemabwa
 
Mwenye majibu ya maswali haya naomba anisaidie
1) Ile GESI ya kutoka Mtwara kuja Kinyerezi Dar imeishia wapi? Si tuliambiwa kwamba sio tu itaondoa tatizo la umeme bali pia bei ya umeme itashuka?

2) Hivi unadhani viongozi wetu (Rais, Mawaziri, Makatibu wakuu, Wakuu wa Mikoa/Wilaya, Wakurugenzi wa mashirika na taasisi za umma, Wabunge, Mabalozi, n,k) wanaathirika na tatizo la umeme? Kwamba inawezekana kweli wakalala bila umeme kwenye makazi yao? Inawezekana kwelie asiyeathirika na tatizo husika akawa na moyo na utashi wa kutafuta utatuzi wa tatizo hilo? Yaani, mgao uwepo au usiwepo mimi kwangu sitakosa umeme, unadhani nitahangaika kutafuta ufumbuzi wa umeme?

3) Hii si mara ya kwanza wala ya pili, hata mwaka jana, mwaka juzi kusikia kwamba kuna upungufu wa uzalishaji wa umeme kutokana na kupungua kwa maji, kwanini tatizo hili linajirudia wakati viongozi wapo na ni wale wale? Waliopewa majukumu ya kutuongoza kweli wana maono na dira ya tunakukwenda?

Natafakari tu, lakini kama kuna mwenye majibu ya maswali haya nitashukuru kama atanisaidia
Tatizo la umeme limeanzia wapi,mbona liliisha awamu ya tano kuna nini tatizo kuanza mara baada ya January kuwepo pale. something wrong somewhere
 
Back
Top Bottom