Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Ili tuweze kuwachukulia serious watawala wetu na hasa wabunge wetu kwenye suala la rada wakati umefika kwa Wabunge wote kukubaliana kuunda Kamati Teule ya Bunge ambayo itafanya uchunguzi wa wazi na huru kuhusu nini kilitokea. Hii itakuwa ni hatua ya kwanza ya kutufanya tuamini kuwa serikali yetu kweli iko makini na imeguswa. Hadi hivi sasa walioonekana kufuatilia ni Waingereza tu. Kamati Teule iundwe mara moja kabla ya kuendelea na kudai fedha zaidi.
Kamati Teule ikishaundwa na kupewa TOR za kueleweka tutakuwa tayari sisi wengine kuwasaidia ushahidi utakaowasaidia. Tutatoa ushirikiano kama kwenye Kamati Teule ya Richmond. Tunajua mengi kweli. Hatuitaji mjadala wa Rada uwe hivi hivi, mjadala utakuwa na maana kama kutoka hapo itaundwa kamati teule.
Kamati Teule ikishaundwa na kupewa TOR za kueleweka tutakuwa tayari sisi wengine kuwasaidia ushahidi utakaowasaidia. Tutatoa ushirikiano kama kwenye Kamati Teule ya Richmond. Tunajua mengi kweli. Hatuitaji mjadala wa Rada uwe hivi hivi, mjadala utakuwa na maana kama kutoka hapo itaundwa kamati teule.