Wakuu,
Tumekuwa na mijadala na taarifa mbalimbali hapa JF na mitandao mingine kuhusu hatima ya ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya (EU). Ili kuweka mambo sawa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imetoa ufafanuzi rasmi kama inavyoonekana hapa:
Kwa wanaopata changamoto ya kuisoma taarifa hiyo kwa kina, nimekuleteeni muhtasari wa mambo ya msingi yaliyofafanuliwa na Serikali:
Nini maoni yako kuhusiana na tamko hili la Serikali ya Tanzania?
Tumekuwa na mijadala na taarifa mbalimbali hapa JF na mitandao mingine kuhusu hatima ya ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya (EU). Ili kuweka mambo sawa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imetoa ufafanuzi rasmi kama inavyoonekana hapa:
Kwa wanaopata changamoto ya kuisoma taarifa hiyo kwa kina, nimekuleteeni muhtasari wa mambo ya msingi yaliyofafanuliwa na Serikali:
1. Nini Hasa Kilitokea?
- Kamati ya Mambo ya Nje na Kamati ya Maendeleo za Bunge la Ulaya zimefanya kikao na kupiga kura kuhusu mapendekezo yanayohusiana na Mpango wa Ushirikiano wa Maendeleo wa mwaka 2025 kati ya Tanzania na EU.
- Katika kura hiyo ngazi ya kamati, mapendekezo yalipitishwa kwa kura 81 za kuunga mkono, kura 1 ya kupinga, na kura 4 za kutokuwa na msimamo.
2. Ufafanuzi wa Serikali (Mambo 3 ya Kuzingatia)
Ili kuepuka 'taharuki', Wizara imefafanua kuwa haya sio maamuzi ya mwisho, na mchakato uko hivi:- Ni Hatua ya Awali: Kura hii imepigwa na Kamati mbili tu na ni sehemu ya taratibu za ndani za Bunge la Ulaya za kufanya maamuzi.
- Mchakato Bado Haujakamilika: Mapendekezo haya lazima yapelekwe kwenye Kikao cha Bunge zima la Ulaya (lenye Wabunge zaidi ya 700) kwa ajili ya mjadala na uamuzi wa mwisho. Hivyo, kura ya kamati haiwakilishi msimamo wa mwisho wa Bunge zima la EU.
- Mamlaka ya Kiutendaji yako kwa 'Tume ya Ulaya': Kama ilivyo kwenye mifumo mingi ya kibunge, maazimio ya Bunge hupelekwa kwenye chombo cha utendaji. Kwa upande wa EU, uhusiano na nchi washirika huendeshwa na Tume ya Ulaya (European Commission). Hivyo, mapendekezo hayo hayapaswi kutafsiriwa kuwa ndiyo uamuzi wa moja kwa moja unaobainisha mustakabali wa mahusiano.
3. Hali ya Mahusiano ya Tanzania na EU kwa Sasa
- Serikali inatoa hakikisho kuwa uhusiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya unaendelea kuwa imara na unazidi kustawi.
- Ushirikiano huu umejengwa kwa muda mrefu kupitia mazungumzo na kuheshimiana, na Serikali ina dhamira ya dhati ya kuendelea kuimarisha ushirikiano huu kwa faida ya wananchi wa pande zote mbili.
Nini maoni yako kuhusiana na tamko hili la Serikali ya Tanzania?