CCM ina wenyeweKUNA KITU HAKIENDI SAWA NDANI YA CCM NA HASA KATIKA SEKRETARIAT YAKE. TAZAMA HAYA:
-Chenge, Mramba, Blandes, wako mahakamani na wote tayari wameambiwa kuna kesi ya kujibu
-Mwakalebela anaondolewa kwa sababu ya kuwa mahakamani?!
-Mfanyakazi wa serikali akifunguliwa tu mashtaka anakuwa nje ya kazi mpaka kesi iishe
-Bashe anaondolewa kwa sababu za uraia, lakini mkoa mzima wa Tabora ukiondoa Samweli Sitta, umechukuliwa
na wasomali.
Muda umefika kwa CCM kuwa na independent body ya kuchuja wagombea, siyo hii NEC na CC ambao pia ni wagombea wanaowachuja wagombea wenzao.
KUNA KITU HAKIENDI SAWA NDANI YA CCM NA HASA KATIKA SEKRETARIAT YAKE. TAZAMA HAYA:
-Chenge, Mramba, Blandes, wako mahakamani na wote tayari wameambiwa kuna kesi ya kujibu
-Mwakalebela anaondolewa kwa sababu ya kuwa mahakamani?!
-Mfanyakazi wa serikali akifunguliwa tu mashtaka anakuwa nje ya kazi mpaka kesi iishe
-Bashe anaondolewa kwa sababu za uraia, lakini mkoa mzima wa Tabora ukiondoa Samweli Sitta, umechukuliwa na wasomali.
Muda umefika kwa CCM kuwa na independent body ya kuchuja wagombea, siyo hii NEC na CC ambao pia ni wagombea wanaowachuja wagombea wenzao.
========Kazi kweli kweli, hata kama ni ubaguzi huu wako umezidi. Kama ni watanzania lakini wana nasaba za kisomali haiwaondolei u Tanzania wao. Na wana haki kama watanzania wengine , kama ya kugombea nafasi kama Ubunge.
Lakini Kapuya, Nkumba, Mfutakamba, na Kingwangala ni wasomali?.
Muzee, ukifikisha miaka 18 unatakiwa uukane uraia mmoja, hakuna uraia by default kwa wageni.Nadhani sheria zingine inatakiwa ziwe za kimataifa, Mtu kazaliwa Tanzania, leo unakuja kumwambia si raia wa hii nchi~sasa sijui yeye ni raia wa sayari gani, Mars?. Ni bora hawa CCM wangemtengenezea zengwe lingine lakini kwa hili la uraia mmhh...It doesn't make any sense to me!.
Wajameni, kwa nini hatutaki ku argue kwa kutafisiri sheria za uraia zilizopo uhamiaji? kwangu mimi haingii akilini kuhoji uraia wa Manji, RA na wengine bila kuwa na taarifa zaidi hii inatupotezea umakini wetu na kushusha hadhi ya jukwaa. Tujadili tukiwa na data siyo bifu na wivu binafsi.
Hawa nao wanawazuga watu tu.. hivi Chiligati akiulizwa Rostam alizaliwa wapi na lini anaweza kutoa jibu?