Nmeingia kwe kasherehe ka ndugu yangu nikaacha kamkweche kangu nje parking ya ukumbi mbali na Barabara.
Wamekuja vijana wa TANROAD hawasikii la muadhini wala nini, wanasema nimepaki kwenye hifadhi ya barabara faini laki 200, jamani tuoneane huruma, kweli kwa uchumi huu hii fedha ni ya kutafuta mwezi nzima.
Sheria zipi? Sikatai ila zisiwe sheria za kuumizana maana badala ya kufundisha zinaleta chuki tu kati ya wananchi na haya mashirika.
Naomba waliangalie hili na kutupa mwelekezo badala ya kutengenezeana mazingira ya kuumizana.