Kamanda Kova asilaumiwe!

kweli huo ni utendaji wake wa kawaida na anajitahidi kusimamia anayoagizwa na amiri jeshi mkuu
 
Mimi nilipoteza imani na polisi pale walipoleta kichwa cha albino na kukiweka chooni kwa baba hapa kawe saa nane usiku then wanaenda kumuamsha kuja kukagua, hii ni baada ya mzee kukataa kuwaingiza kwenye payroll huku biashara yake ni halali. Cha kushangaza ambacho bado najiauliz ni je kichwa wametoa wapi? Wanakitunza kwanini? Hawa wana usalama kwa nini wanatumia miili ya watu kubambikia wengine kesi? Kwa kweli inatia aibu sana kwa jeshi la polisi, hivi polisi wote wamechanganyikiwa? Sina jibu
 
Mkuu mleta mada umemalizia kwa kumwambia aendelee na kazi yake unayoiita nzuri?unadhani kama anasoma hapa anaweza kuchambua na kuelewa unavyotaka aelewe?nimependa bandiko,ila huo utani wakati ishu ni hatari na maisha ya watu hatarini ni noma.Sasa hata kama tunataka kulifix jeshi la polisi,akiachwa aendelee ndo jambo la maana?Accountability is the key to the changes that we want.It is the begining...Kova amekosea and my opinion;he should resign!

Mkuu uandishi una namna nyingi, labda unajaribu kutuhabarisha pia kwamba Kova hana akili ya kutosha kuelewa hili bandiko
 
Mkuu uandishi una namna nyingi, labda unajaribu kutuhabarisha pia kwamba Kova hana akili ya kutosha kuelewa hili bandiko

Hawa watu ni kuwaeleza right on,wameshaonyesha dharau kubwa sana dhidi ya wananchi na kuinsult our inteligences.Kama ni kiazi sema kiazi,chepeo sema chepeo and so forth.Kuandika ameandika safi,except hapo mwisho.Kova,jeshi la polisi na serikali kwa ujumla wamekosea,that's the bottom line
 
Hivi ubalozi wa kenya wameshamtambua huyo 'MTEKAJI' kuwa ni kweli raia wao na wana records zake za uhalifu? manake naona kitambulisho cha uraia kimetolewa 2010, Umri bado mkanganyiko 21 au 31. Kama 21 ina maana kitambulisho kilitolewa akiwa na miaka 19 sheria za kenya za vitambulisho vya uraia inasemaje? kama ni 31 je muda wote alikuwa wapi kupata kitambulisho cha uraia.
 
Hivi kwa nini serikali ya Jk haimkamati mtuhumiwa wa kumtesa Dr Steven Ulimboka?kwa sababu Dr Ulimboka aliweza kumtambua pale alipofika wodi kutaka kumalizia kumuua Dr Ulimboka,hivi angekuwa ni mlalahoi ndo anatuhumiwa si angekuwa ameisha kamatwa na kufunguliwa mashitaka.Hivi huyu Ahmed Msangi anakinga ya kutokamatwa au analindwa na vigogo wenzake wa jeshi la pilisi na wa usalama wa taifa?au ni kutokana na udhaifu wa serikali ya mr Dhaifu?
 
Ipo siku atakuja kukamatwa tu. Wanamageuzi wakija chukua nchi atanyea debe. Serikali isidhani kuwa kufumbia macho udhalimu kutawaepusha na mkono wa sheria! wao wayakoroge tu siku zinakuja.
 
Wakimkamata itabidi aseme alikuwa na nani na alitumwa na nani etc? Hapa ndio penye tatizo kubwa. Nahisi wakishindwa kabisa watamstaafisha tu lakini si zaidi ya hapo.
 
Hivi ubalozi wa kenya wameshamtambua huyo 'MTEKAJI' kuwa ni kweli raia wao na wana records zake za uhalifu? manake naona kitambulisho cha uraia kimetolewa 2010, Umri bado mkanganyiko 21 au 31. Kama 21 ina maana kitambulisho kilitolewa akiwa na miaka 19 sheria za kenya za vitambulisho vya uraia inasemaje? kama ni 31 je muda wote alikuwa wapi kupata kitambulisho cha uraia.

Another important question
 
Hivi kwa nini serikali ya Jk haimkamati mtuhumiwa wa kumtesa Dr Steven Ulimboka?kwa sababu Dr Ulimboka aliweza kumtambua pale alipofika wodi kutaka kumalizia kumuua Dr Ulimboka,hivi angekuwa ni mlalahoi ndo anatuhumiwa si angekuwa ameisha kamatwa na kufunguliwa mashitaka.Hivi huyu Ahmed Msangi anakinga ya kutokamatwa au analindwa na vigogo wenzake wa jeshi la pilisi na wa usalama wa taifa?au ni kutokana na udhaifu wa serikali ya mr Dhaifu?
Katika hali ya kawaida Polisi au Serikali ilipaswa isikilize kilio cha wale wanaohitaji tume huru ya kuchunguza kwa vile serikali na polisi ni mojawapo ya watuhumiwa. Katika hali hii ambapo serikali imekataa kusikiliza ushauri huo usio na madhara yoyote kwa upande wao (hasa kama ni kweli wanavyodai kuwa hawakuhusika) imani kama haki itatendeka ni ndogo sana. Kutaja kuwa ni mtuhumiwa mmoja tu hadi sasa amehojiwa na mtuhumiwa mwenyewe asiwe yule aliyempigia simu Ulimboka ambaye kwa vyovyote jeshi la Polisi linamfahamu, kunalifanya Jeshi la Polisi machoni pa raia kuwa haliko makini. Hata kama waliotajwa wanaweza wasiwe wamehusika kuwahoji kulikuwa ni kwa lazima maana ni watuhumiwa. Ikiwa mbunge Nasari alihojiwa na kuachiwa kwa nini huyo aliyetajwa na Ulimboka asihojiwe. Kwa mazingira kama haya Jeshi linawalazimisha watu waamini kuwa tukio hili lina mkono wa serikali. Huu ni utamaduni mpya ambao tusingependa kuushuhudia katika nchi yetu. Mungu ibariki Tanzania
 
Ukiangalia jinsi hii sinema ambayo kamanda Kova kaachiwa aicheze juu ya mgogoro wa madaktari kwa taarifa aliyotoa na maelezo ya Mch. Gwajima kama anaipenda hii nchi anatakiwa ajiuzulu kwa kweli maana amejishushia heshima sana mbele ya jamii hata sisi tuliokua tunamuunga mkono sana na sasa naanza kuwaunga mkono madaktari nikiamini pengine tunadanganywa sana na serikali katika hili swala jinsi mambo yanavyojitokeza sasa.
 
Hivi ukimtuma mwanao akaibe na ukaamriwa kumtafuta mwizi utampeleka mwanao akashitakiwe? Ndiyo maana watu hao zaidi ya watano watalindwa. Kama tunataka haki ni lazima nguvu ya umma itumike kwa watu hao pindi watakapofahamika wote. Hivi unajua ni kwa nini vibaka wakikamatwa wanachomwa moto au kuuawa mara moja? Umma ulishapoteza imani na vyombo vya ulinzi hasa polisi!!!
 
kama kweli ulimboka alipata kipigo mpaka kupelekwa nje angewezaje kutambua?
 
Rest in Peace Kova
grave.jpg
Kamanda-Kova.jpg
 
Hofu yangu ni ukanjanja,usanii,magumashi ya Kova yasije kuteletea matatizo ya Kidiplomasia na Kenya nchi jirani,kashawapakazia kwamba wana kundi hatari linajiita Gangstar
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom