Hivi kwa nini serikali ya Jk haimkamati mtuhumiwa wa kumtesa Dr Steven Ulimboka?kwa sababu Dr Ulimboka aliweza kumtambua pale alipofika wodi kutaka kumalizia kumuua Dr Ulimboka,hivi angekuwa ni mlalahoi ndo anatuhumiwa si angekuwa ameisha kamatwa na kufunguliwa mashitaka.Hivi huyu Ahmed Msangi anakinga ya kutokamatwa au analindwa na vigogo wenzake wa jeshi la pilisi na wa usalama wa taifa?au ni kutokana na udhaifu wa serikali ya mr Dhaifu?
Napenda kujua maendeleo ya kamanda kova kwa sasa, yuko wapi na anafanya nini? Na daktari ulimboka yuko wapi? Msaada wa taarifa hizi ili tuweke historia vema.ukiwa na busara huwezi endelea fanya kazi za kuwaua ama kuwaumiza wengine, kova analaumiwa kwa sababu anjua anachofanya kuwa si sahihi sasa kwa busara ilimpasa kuachana na kazi hiyo maana inamjengea maadui na kumvunjia heshima kama vile pinda.
labda tukubaliane kuwa hana busara na njaa ndio inayomsumbua ndio maana anaendelea kufanya anayoyafanya.
maana kuchagua pesa kuliko utu ni uchache wa busara
ndio maana mfalme suleiman katika biblia hakumuomba mungu utajiri au hela au nguvu aliomba busara.