Kamanda Kova asilaumiwe!

Unajua huyu Msangi ni kama keshakufa.
Maneno yetu watanzania na sala zetu zishamuua mara zaidi ya mia.
Kabaki kama zombie tu
 
Mimi nilipoteza imani na polisi pale walipoleta kichwa cha albino na kukiweka chooni kwa baba hapa kawe saa nane usiku then wanaenda kumuamsha kuja kukagua, hii ni baada ya mzee kukataa kuwaingiza kwenye payroll huku biashara yake ni halali. Cha kushangaza ambacho bado najiauliz ni je kichwa wametoa wapi? Wanakitunza kwanini? Hawa wana usalama kwa nini wanatumia miili ya watu kubambikia wengine kesi? Kwa kweli inatia aibu sana kwa jeshi la polisi, hivi polisi wote wamechanganyikiwa? Sina jibu
mkuu ndo lile sakata la James Isame?Usishangae ndiyo maana polisi wengi wakishastaafu maisha yao huwa yanakuwa ya dhiki sana sababu ya laana mbalimbali wanazokuwa wamekusanya
 
Ngoja Dr Ulimboka arudi,kwanza alitakiwa atoe taarifa kwa mwanasheria wake kushinikiza mtuhumiwa aliyetambuliwa akamatwe.However sidhani kama it will be possible,labda kama ccm itaondolewa madarakani.
 
Mkamateni ahmed msangi-Ngwajima
Mkenya hawezi kuja kutubu kwangu kwa nini asiende kwenye kanisa lake- Ngwajima
 
Mimi nilipoteza imani na polisi pale walipoleta kichwa cha albino na kukiweka chooni kwa baba hapa kawe saa nane usiku then wanaenda kumuamsha kuja kukagua, hii ni baada ya mzee kukataa kuwaingiza kwenye payroll huku biashara yake ni halali. Cha kushangaza ambacho bado najiauliz ni je kichwa wametoa wapi? Wanakitunza kwanini? Hawa wana usalama kwa nini wanatumia miili ya watu kubambikia wengine kesi? Kwa kweli inatia aibu sana kwa jeshi la polisi, hivi polisi wote wamechanganyikiwa? Sina jibu


Duuuuuu!, Poleni saana kwa mtendwa. Too bad
 
Rest in Peace Kova
grave.jpg
Kamanda-Kova.jpg

Mhhhhhh! ivi huyo Kova ni yule aliyepigia saluti mwili wa marehemu Kanumba ambaye ni mrangi wa hapa Kondoa
 
Hivi ubalozi wa kenya wameshamtambua huyo 'MTEKAJI' kuwa ni kweli raia wao na wana records zake za uhalifu? manake naona kitambulisho cha uraia kimetolewa 2010, Umri bado mkanganyiko 21 au 31. Kama 21 ina maana kitambulisho kilitolewa akiwa na miaka 19 sheria za kenya za vitambulisho vya uraia inasemaje? kama ni 31 je muda wote alikuwa wapi kupata kitambulisho cha uraia.

wametudanganya na wanajua kwamba wametudanganya, haina haja ya kujiuliza yote hayo
 
Nchi za wenzetu baada ya tukio wangechukua DNA ambazo zilikuwepo kwenye nguo za Dr. na alama za vidole ambazo zingesaidia kubaini kama Joshua alihusika. Sasa kwa vile hatuna utaalamu huo, tutabaki na labda!
 
Pia na mimi nakumbuka wameshawahi kunikuta mtaani, wakadai ni mzurulaji, waliniomba rushwa nikakataa, wakasema twende kituoni, kwa kuwa nilijiamini sikuwa na tatizo lolote nikawambia twendeni, kama hatua mia moja kufika kituoni wakaniambia haya shika bangi yako, nikashtuka!, ikabidi niwape tu buku 10 ili nisije swekwa rumande, na tatizo kubwa ni kwamba jamhuri inadai polisi haongopi, tafakari sasa ni watanzania wangapi wanaobambikiwa kesi kwa kukataa kuwapatia kitu kidogo.
 
Mimi nilipoteza imani na polisi pale walipoleta kichwa cha albino na kukiweka chooni kwa baba hapa kawe saa nane usiku then wanaenda kumuamsha kuja kukagua, hii ni baada ya mzee kukataa kuwaingiza kwenye payroll huku biashara yake ni halali. Cha kushangaza ambacho bado najiauliz ni je kichwa wametoa wapi? Wanakitunza kwanini? Hawa wana usalama kwa nini wanatumia miili ya watu kubambikia wengine kesi? Kwa kweli inatia aibu sana kwa jeshi la polisi, hivi polisi wote wamechanganyikiwa? Sina jibu

Jakubumba,

Ni kweli polisi wa Tanzania wana Tabia ya kuwataka watu wawapelekee ushahidi and this can only happen in Tanzania. Akina Kova wamwkulia kule Police lines pale Moshi. Ni matunda ya polisi kurithisha kazi watoto wao.

Elimu Yao wengi ni ya kuungaunga. Most have IQ below normal.

Kuhusu kuweka kichwa kwenye guest house ya Baba yako hiyo ni Vandetta! Chacha ana Tabia ya mazishi huwa halipi watu kwenye deals au wanazokubaliana na watu kwa hiyo imefanyika ili kumtesa. Itabidi wapeni polisi rushwa ya kutosha watawaambia nani kasuka hilo Dili.
 
Huyu KOVA, MWIGULU, CHILIGATI n.k wanatoka mahala kumoja.........sitaki kuamini kuwa watu wote wa huko wako hivi
 
Sisi watanzania tunakosea kumhukumu Kova kwa swala hili la Joshua Mkenya kuhusika na tukio la Ulimboka. Tunamuonea Kova

1. Ni utamaduni wa serikali hii kupika uongo na kudanganya wananchi kuhusu mambo mbalimbali. Hata Bunge hudanganywa
2. Ni utamaduni wa Polisi kubambika watu kesi za mauaji na uharamia.
3. Kova amekuwa mara kwa mara akiitisha mikutano na waandishi aw habari kutangaza habari za uongo za kukamatwa majambazi "sugu waliokuwa wanatafutwa muda mrefu" Anachukua silaha za ujambazi uliofanyika zamani anaonesha kana kwamba ndo kazikamata. Ili aonekane anafanya kazi yake kwa umahiri. Ujambazi unaongezeka hadi wananchi wamezoea hawalalamiki tena
4. Jeshi la Polisi kwa ujumla halipelelezi kesi bila mlalamikaji kutoa pesa na nyenzo nyingine. Nani ataliwezesha jeshi la Polisi kupeleleza tukio la Ulimboka? Je, jeshi la Polisi lina ujuzi wa kupeleleza au kutesa watu wakiri makosa?
5. Jeshi la Polisi linatuhumiwa kuhusika na tukio la Ulimboka, mnatarajia Kova anaweza kupeleleza Msangi kama ndiye aliyemtuma Msangi?


Kwa maelezo hayo hapo juu, namsifu sana Kova kwa ubunifu aliofanya wa kutupatia mtuhumiwa Mkenya na kulihusisha kanisa. Nahisi Kova aliumoza kichwa sana na amejitahidi kutafuta namna ya kulinausua jeshi la Polisi na serikali.

Kwanini tuhangaike kutafuta kujiuliza kam Kenya kuna watu wenye tabia ya uharamia na mauaji wakati tunajua hivyo tayari, Mungiki, Mauaji baada ya Uchaguzi etc

Kwa nini tuhangaike kuhoji uadilifu wa viongozi wa dini? Kwa nini kiongozi huyo wa dini asifurahi kwamba serikali imemshukuru kwa kutoa ushirikiano?

Tunafanya makosa kumtuhumu Kova kudanganya leo wakati ndiyo utendaji wa kazi aw kawaida siku zote, penda usipende

Endelea Kamanda Kova, I salute you!

BIG SHAME!!!!! Hiki ni kituko na ni aibu kwa waliompa madaraka Kamanda Kova. Inakuwaje ishu tete kama hii unathubutu kukurupuka na kutoa maelezo ambayo hayana utafiti wa kuaminika?

Sioni sababu inayosababisha kamanda kova apate usongo wa tatizo hili kiasi hiki, wanaweza kutokea watu kumi waliohongwa ili kudhoofisha upelelezi na kudai kuwa ni wahusika wa tukio je atakubaliana nao tu bila kujua undani wa taarifa wanazotoa?

Watu wa aina ya kova ndiyo wanaosababisha serikali ionekane ina tatizo, katika karne hii yenye watu wenye elimu na uelewa wa kutosha ukimkuta mtu mzima anadhani anaweza kuwahadaa watu hivihivi hicho ni kichekesho!!! kwa hali ya kawaida tu kama kweli mtu aliyejitambulisha kuwa ni mmojawao wa waliomshambulia Dk Ulimboka amekamatwa, shahidi wengine wa uhakika ni kanisa la Ufufuo je kamanda Kova nao amewaunganisha kwenye watu muhimu wa kutoa ushahidi?
 
mkuu mleta mada umemalizia kwa kumwambia aendelee na kazi yake unayoiita nzuri?unadhani kama anasoma hapa anaweza kuchambua na kuelewa unavyotaka aelewe?nimependa bandiko,ila huo utani wakati ishu ni hatari na maisha ya watu hatarini ni noma.sasa hata kama tunataka kulifix jeshi la polisi,akiachwa aendelee ndo jambo la maana?accountability is the key to the changes that we want.it is the begining...kova amekosea and my opinion;he should resign!

tuko pamoja mkuu. Sidhani kama kova amefanya analysis ya kutosha juu ya athali ya kauli yake. Yaani kuhusisha utekaji wa ulimboka na huyo mkenya na pia kanisa kwa upande mwingine. Kwangu mimi naona kuna implication mbaya kwani katika harakati tunazoendelea nazo za ushirikiano-eac- naona kama ni tatizo kubwa. Kwani kova anataka tuanze kuwaona makenya ni watu hatari na wasiofaa kuwanao katika jamii. Kwa mtu makini na aliyeenda shule huhitaji nusu saa kujua kuwa alichokisema kova ni uongo. Nilikuwa sifahamu upeo wa kufikiri wa kova pengine na watalaam wengine wa jeshi letu la polisi, sasa nimefahamu kuwa hatuna polisi makini. Alichokifanya kova na waandamizi wake kinadhalilisha jeshi zima la polisi kuwa ni watu ambao pengine wanafikiri kwa kutumia maka...kwangu mimi naona hapo ndo walikaa na kuona wakisema hivyo watanzania wataamini. Duuuuu...maskini kova sijui karogwa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom