Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

Mauwaji aliyoyafanya ni ya kisiasa,na kwahiyo majibu yake pia ni ya kisiasa.

Hata asipojiuzulu,kuna wakati atajibu tuhuma hizi za mauwaji.Nchi za wenzetu kashfa kama hii wala asingethubutu kupanua mdomo,maana angekuwa keshajiuzulu na angeogopa maneno yake yasitumike dhidi yake wakati wa mashtaka.Kwa mfano kauli kuwa watu wakikusanyika kufunguwa tawi basi wauwawe kwasababu wamevunja sheria.Kauli kwamba walifanya maandamano ni ya kisiasa,kwasababu mwanzoni alisema ni mikutano haitakiwi kwasababu ya sensa,lakini cha ajabu ccm ilikuwa na mikutano,na pia kulikuwepo na fiesta.

Only in Tanzania haya ndo yanaonekana kuwa ni ya kawaida.

Huyu jamaa uwezo wake wa kufikiri ni mdogo sana,yaani pamoja na kusimamia mauwaji ya kizembe yanayolalamikiwa na ulimwengu mzima bado haoneshi ata chembe ya kujutia. Kama wasiotii sheria bila shuruti hukumu yao ni kuuawa mbona hawakuua walioandamana bila kibali kushinikiza kuachiwa waliogomea sensa au waliokata uzio uliowekwa na polisi pale kidongo chekundu? Kama polisi walikuwa wanatekeleza majukumu yao halali kwa nini mtuhumiwa amepelekwa mahakamani? Sishangai sana lkn maana ata raisi wetu ana fikra kama za Kamuhanda ndio maana akuona umuhimu wa kutoa japo pole ya mdomo tu kwa wafiwa.
 
Mimi nilifikiri siku ile ya tukio alikuwa amelewa ulanzi kwa jinsi alivyokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari kabla ya mauaji yenyewe, kumbe ndivyo alivyo muda wote!!!! Ninakubaliana na wadau walaiotangulia kwamba huyu ni mshitakiwa namba moja. Ndiyo, hatafikishwa mahakamani leo lakini iko siku atakabiliana uso kwa uso na Pilato kama si Dar basi ni the Hague! Hana hata ubinadamu wa kusema kwamba ile ilikuwa ni bahati mbaya.
 
Ndo madhara ya kuwa na dead conscience (dhamiri ilokufa)
 
JUMAMOSI, SEPTEMBA 22, 2012 08:48 NA ELIZABETH MJATTA

KAMANDA wa Polisi, Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, ameibuka na kusema hawezi kujiuzulu kutokana na kifo cha aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel ten, Daud Mwangosi, aliyeuawa hivi karibuni mkoani Iringa.

Kamanda Kamuhanda alitoa msimamo huo jana alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Radio cha Radio One wakati wa kipindi cha Kumepambazuka.

“Ninachofahamu mimi ni kwamba, kesi ya msingi iko mahakamani na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ameshaunda kamati ambayo inachunguza mwenendo mzima wa tukio hili na baadaye itatoa taarifa.

“Kwa hiyo, siwezi kujiuzulu kwa sababu tukio hilo la kifo lilitokea wakati wa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti,” alisema Kamanda Kamuhanda.

Alipoulizwa kuhusiana na kuwajibika kutokana na mauaji hayo alisema, hawezi kuwajibika kwa sababu hana makosa.

“Niwajibike kwa kosa lipi?, kuna kosa mtu anaweza akawajibika, lakini kama huna kosa huwezi kuwajibika, haiwezekani watu waliofanya makosa wenyewe kwa kuandamana bila uhalali wasiwajibike halafu mimi niwajibike, haiwezekani.

“Sisi tunapokuwa kazini, tunalinda raia na mali zao na ndiyo tulilofanya na mara zote tunasisitiza utii wa sheria bila kushurutishwa.

“Kwa hiyo, hicho ndicho kilichokuwa kinafanyika, kilichofanyika ndiyo utii wa sheria bila shuruti, wangetii sheria bila shuruti yote yasingetokea,” alisema.

Septemba 2 mwaka huu, Mwangosi aliuawa kwa kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu alipokuwa kazini katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa.

Baada ya kulipuliwa na kitu hicho, mwili wake ulisambaratika vipande vipande ingawa pia askari mmoja aliyekuwa jirani naye, pia alijeruhiwa mguu.

Baada ya tukio hilo, waandishi wa habari, wanaharakati na watu mbalimbali, walilaani tukio hilo na kutoa matamko yao wakitaka Kamanda Kamuhanda ajiuzulu, kutokana na mauaji hayo.

Septemba 12 mwaka huu, askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia mwenye namba G2573, Pasificus Simon,
alipandikizwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Iringa, kwa kosa mauaji ya marehemu Mwangosi.

Mtuhumiwa huyo alipofikishwa mahakamani hapo, hakutakiwa kujibu lolote kutokana na kosa linalomkabili haliwezi kusikilizwa katika mahakama hiyo. Hadi sasa mshitakiwa yuko mahabusu.


Viwanda vya uongo utavijuwa tu.
 
acheni kelele, kamanda kesha ongea, andamaneni tena tuwatwale mitwe.
Afterall mna uhakika gani kuwa bomu lililomuua mwangosi limetoka kwenye bunduki ya yule dogo. Inawezekana walikuja nalo ili wawalipue polisi kwa jazba na kumbe wameua mwandishi.
 
Atuambie Marehemu Mwangosi alivunja sheria ipi hata astahili adhabu ya kifo? Hakuwa hata na jiwe mkononi zaidi ya kamera yake tena chini ya polisi wasiopungua 8 wenye silaha. Hilo kosa hata Shetani atamhukumu.
 
acheni kelele, kamanda kesha ongea, andamaneni tena tuwatwale mitwe.
Afterall mna uhakika gani kuwa bomu lililomuua mwangosi limetoka kwenye bunduki ya yule dogo. Inawezekana walikuja nalo ili wawalipue polisi kwa jazba na kumbe wameua mwandishi.

Sidhani kama uko salama.
 
hajakurupuka serikali ndio inampa jeuri,viongozi wengi serikalini hawapendi chadema kiendelee kuwa hewani. Hivyo yoyote anaekihujumu chadema yupo upanda wao.!!
 
Sidhani kama uko salama.

Niko salama kabis, members wa cdm wengi wao ni wenye hulka ya hasira,jaziba na wasiokubali kuwa hata wasio kubaliana nao mawazo yao yanaweza kuwa sahihi.
Ni rahisi m2 wa aina hii kubeba bomu hata la tnt kwa madhumuni ya kuwaripua polisi ambao kwa cdm kwao ni kikwazo.
 
Niko salama kabis, members wa cdm wengi wao ni wenye hulka ya hasira,jaziba na wasiokubali kuwa hata wasio kubaliana nao mawazo yao yanaweza kuwa sahihi.
Ni rahisi m2 wa aina hii kubeba bomu hata la tnt kwa madhumuni ya kuwaripua polisi ambao kwa cdm kwao ni kikwazo.

Unaweza kuthibitisha hilo kuwa Mwangosi alikuwa na Bomu na je alipewa na nani? Mazingira na kauli ya Kamuhanda yanathibitisha polisi ndiyo waliomwua Mwangosi sasa sielewi kwanini unapinga kitu chenye ushahidi uliojitosheleza. Hata ubinadamu huna mkuu?
 
Anatia kichefuchefu sana huyu! Yani usipotii sheria bila shuruti adhabau yake ndo kifo? Halafu hawa waandishi wetu wa habari nae, utafikiri kama hawajui kuuliza maswali bana!
 
Niko salama kabis, members wa cdm wengi wao ni wenye hulka ya hasira,jaziba na wasiokubali kuwa hata wasio kubaliana nao mawazo yao yanaweza kuwa sahihi.
Ni rahisi m2 wa aina hii kubeba bomu hata la tnt kwa madhumuni ya kuwaripua polisi ambao kwa cdm kwao ni kikwazo.

Kama hufikirii kwa kutumia masaburi, basi unatamani sana leo kutukanwa!
 
Mwandishi wa IPP! unategemea nini hapo zaidi ya white wash? Huyu kamanda ni ignorant good for nothing, nasijui hata kama ana elimu, mwenye cv yake na aiweke tumjadili zaidi inawezekana kabisa katika kupekua madaftari akajakukutwa na maradhi ya akili.

Anasema askari hawana kosa sasa yule aliepelekwa mahakamani kufanya nini? anasema kazi yao kulinda sheria bila shuruti sasa hajui hata kanuni za polisi zinazohimiza kwa nguvu ya sheria utumiaji wa propotinate force, sasa kama kuuwa sio dispropotinated use of force ni kitu gani? Ubaba wake utakuja kumsuta siku yake itafika, madhali kachangia pakubwa katika dhulma ya roho ya marehem na warithi wake ajue tu dunia hii iko siku itamsuta na atasimama mbele ya sharia kujibu tuhuma.

Huyu sifikiri kama hata anaelimu ya darasa la saba, mbali ya elimu hana hata akhlaki za kibinaadamu, chuki, jazba na upendeleo ndio uliomuathiri akili akawa ni sawa ni mgonjwa wa akili. Aibu kuwa ndio mkuu wa polisi wa mkoa, kila siku zinavyokwenda ndio kunaniwia vigumu kukitetea chama nilichokiamini. shame on you.
 
Wanasheria tutakufwata popote pale ulipo, uwe umevaa gwanda uwe umevua gwanda!
 
kwa nini waandishi wa habari huwa mnawaauliza hawa mnaowauliza maswali mwongozo? kwa nini usimuulize ni makosa gani ambayo yanapaswa mtu akawajibika kama alivyosema kuna makosa ya kuwajibika?

.
Njaa mbaya sana. Waandishi wengi Tanzania wanauliza maswali huku wakiwa wamechora picha ya bahasha ya kaki kichwani.
.
 
Kuna kila sababu kwa viongozi wetu kupatiwa mafunzo ya uwajibikaji. Mara nyingi utawasikia wakisema niwajibike kwa lipi wakati mimi sina kosa. Nijuavyo mimi, wengine watasahihisha kuwajibika siyo lazima ufanye kosa, unaweza kuwajibika kwa kupinga kilichotokea au kukerwa na kilichotokea au kinachoendelea katika utawala wako au uongozi wako. Kwa maana nyingi ni vyema viongozi wetu wakatambua kuwa kiongozi anayefanya makosa yeye hatakiwa kujiuzulu tu bali ni lazima ashitakiwe kwa kosa alilolifanya. Sasa wanaposema hawawezi kujiuzulu kwa kuwa hawana kosa wanashindwa kuelewa kuwa ukifanya kosa na ikabainika ni kosa unatakiwa kushitakiwa na kujibu tuhuma dhidi yako.

Kujiuzulu unaweza usiwe umefanya kosa lakini kwa kuwa wewe ni kiongozi na umeshindwa kudhibiti makosa chini ya usimamizi wako unashauriwa kujuuluzu ili kuacha hiyo nafasi kwa kuwa imekushinda au haumweshindwa kutimiza masharti ya kazi husika.

Kashule hako ni muhimi sana kwa viongozi wetu, ni aibu kuona kiongozi mkubwa kama Waziri, Mbuge, RC, RPC N.K anashindwa kutofautisha au kuelewa maana ya kuwajibika kwa kujiuzulu na kuwajibishwa kwa mustakabali wa sheria kutokana na kosa ulilofanya.

Nawasilisha
 
Back
Top Bottom