Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

naombeni namba yake tafadhali....


RPC IRINGA
con_tel.png

+255 715009921
 
Hapa sio suala la kujiuzulu, na wala sisi hatuombi RPC Kamuhanda ajiuzulu. Akishajiuzulu so what? Ndio kanawa mikono au? TUNACHOTAKA NI RPC KAMUHANDA APANDISHWE KIZIMBANI KWA MAUAJI YA MWANGOSI (RIP).
 
JUMAMOSI, SEPTEMBA 22, 2012 08:48 NA ELIZABETH MJATTA

KAMANDA wa Polisi, Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, ameibuka na kusema hawezi kujiuzulu kutokana na kifo cha aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel ten, Daud Mwangosi, aliyeuawa hivi karibuni mkoani Iringa.

Kamanda Kamuhanda alitoa msimamo huo jana alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Radio cha Radio One wakati wa kipindi cha Kumepambazuka.

“Ninachofahamu mimi ni kwamba, kesi ya msingi iko mahakamani na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ameshaunda kamati ambayo inachunguza mwenendo mzima wa tukio hili na baadaye itatoa taarifa.

“Kwa hiyo, siwezi kujiuzulu kwa sababu tukio hilo la kifo lilitokea wakati wa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti,” alisema Kamanda Kamuhanda.

Alipoulizwa kuhusiana na kuwajibika kutokana na mauaji hayo alisema, hawezi kuwajibika kwa sababu hana makosa.

“Niwajibike kwa kosa lipi?, kuna kosa mtu anaweza akawajibika, lakini kama huna kosa huwezi kuwajibika, haiwezekani watu waliofanya makosa wenyewe kwa kuandamana bila uhalali wasiwajibike halafu mimi niwajibike, haiwezekani.

“Sisi tunapokuwa kazini, tunalinda raia na mali zao na ndiyo tulilofanya na mara zote tunasisitiza utii wa sheria bila kushurutishwa.

“Kwa hiyo, hicho ndicho kilichokuwa kinafanyika, kilichofanyika ndiyo utii wa sheria bila shuruti, wangetii sheria bila shuruti yote yasingetokea,” alisema.

Septemba 2 mwaka huu, Mwangosi aliuawa kwa kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu alipokuwa kazini katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa.

Baada ya kulipuliwa na kitu hicho, mwili wake ulisambaratika vipande vipande ingawa pia askari mmoja aliyekuwa jirani naye, pia alijeruhiwa mguu.

Baada ya tukio hilo, waandishi wa habari, wanaharakati na watu mbalimbali, walilaani tukio hilo na kutoa matamko yao wakitaka Kamanda Kamuhanda ajiuzulu, kutokana na mauaji hayo.

Septemba 12 mwaka huu, askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia mwenye namba G2573, Pasificus Simon, alipandikizwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Iringa, kwa kosa mauaji ya marehemu Mwangosi.

Mtuhumiwa huyo alipofikishwa mahakamani hapo, hakutakiwa kujibu lolote kutokana na kosa linalomkabili haliwezi kusikilizwa katika mahakama hiyo. Hadi sasa mshitakiwa yuko mahabusu.


Kosa halihalishi kosa. Suluhisho la kosa la kuto kutii sheria kwa hiari si kuua. Na kama hicho kitendo cha kuua ni halali kwa nini huyu askari wa cheo cha chini kafikishwa mahakamani?
 
Majibu yake yamenistua sana.

Hakika sheria si mali kitu kwa the keeper.

askari with an empty big head... ooh pumpkin between his shoulders, eti anasema kama wagetii sheria bila shuruti hayo yote yasingetokea. sasa kesi mahakamani, na kamati sijui tume ni za nini, huyu kamanda bure kabisa. mjinga sana huyu mzee. wakati utamuhukumu.
 
[h=2][/h]JUMAMOSI, SEPTEMBA 22, 2012 08:48 NA ELIZABETH MJATTA

KAMANDA wa Polisi, Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, ameibuka na kusema hawezi kujiuzulu kutokana na kifo cha aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel ten, Daud Mwangosi, aliyeuawa hivi karibuni mkoani Iringa.

Kamanda Kamuhanda alitoa msimamo huo jana alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Radio cha Radio One wakati wa kipindi cha Kumepambazuka.

Ninachofahamu mimi ni kwamba, kesi ya msingi iko mahakamani na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ameshaunda kamati ambayo inachunguza mwenendo mzima wa tukio hili na baadaye itatoa taarifa.

Kwa hiyo, siwezi kujiuzulu kwa sababu tukio hilo la kifo lilitokea wakati wa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti, alisema Kamanda Kamuhanda.

Alipoulizwa kuhusiana na kuwajibika kutokana na mauaji hayo alisema, hawezi kuwajibika kwa sababu hana makosa.

Niwajibike kwa kosa lipi?, kuna kosa mtu anaweza akawajibika, lakini kama huna kosa huwezi kuwajibika, haiwezekani watu waliofanya makosa wenyewe kwa kuandamana bila uhalali wasiwajibike halafu mimi niwajibike, haiwezekani.

Sisi tunapokuwa kazini, tunalinda raia na mali zao na ndiyo tulilofanya na mara zote tunasisitiza utii wa sheria bila kushurutishwa.

Kwa hiyo, hicho ndicho kilichokuwa kinafanyika, kilichofanyika ndiyo utii wa sheria bila shuruti, wangetii sheria bila shuruti yote yasingetokea, alisema.

Septemba 2 mwaka huu, Mwangosi aliuawa kwa kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu alipokuwa kazini katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa.

Baada ya kulipuliwa na kitu hicho, mwili wake ulisambaratika vipande vipande ingawa pia askari mmoja aliyekuwa jirani naye, pia alijeruhiwa mguu.

Baada ya tukio hilo, waandishi wa habari, wanaharakati na watu mbalimbali, walilaani tukio hilo na kutoa matamko yao wakitaka Kamanda Kamuhanda ajiuzulu, kutokana na mauaji hayo.

Septemba 12 mwaka huu, askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia mwenye namba G2573, Pasificus Simon, alipandikizwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Iringa, kwa kosa mauaji ya marehemu Mwangosi.

Mtuhumiwa huyo alipofikishwa mahakamani hapo, hakutakiwa kujibu lolote kutokana na kosa linalomkabili haliwezi kusikilizwa katika mahakama hiyo. Hadi sasa mshitakiwa yuko mahabusu.
Mkuu Mlyafinono,
Kila nikikuona nakumbuka ulivyoniliza...
Kisheria mtuhumiwa akikiri kosa kwa kufanya confession mbele ya mlinzi wa amani, then hakuna ushahidi wowote unaohitajika hivyo mahakama haitahitaji kuita shahidi yoyote!.

Kama ni hivyo, na ni kweli mtuhumiwa huyo amekiri kosa, mambo yafuatayo yatafanyika.
  1. Mtuhumiwa atapelekwa mahakamani na kusomewa shitaka la mauaji na hatatakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji (jurisdiction). Kesi za mauaji husikilizwa na mahakama kuu!.
  2. Kama polisi watathibitisha wamekamilisha uchunguzi, then jalada la kesi hiyo litapelekwa kwa DPP na hatimaye litahamishiwa mahakama kuu kupangiwa siku ya kusikilizwa by that time, kesi itakuwa imeishabadilishwa kutoka kesi ya mauaji (murder) hadi kesi ya kuua bila kukusudia (manslaughter)
  3. Kwenye ile confession, polisi wameshakaa na mwenzao na kumfundisha namna bora kabisa ya kukiri kosa ni kusema kuwa kutokana na vurugu na purukushani, bomu lilifyatuka kwa bahati mbaya na kumlipua marehemu!. Ili jinai ya mader itendeke, lazima kuwepo tendo la mauaji (actus reus) na nia ya mauaji (mens rea). Kwa vile jinai ya kifo imetokea hivyo actus reus imefanyika lakini kwa vile silaha ile ni bomu la machozi na sio ya risasi za moto, kazi ya bomu la machozi sio kuua, mahakama itakubali moja kwa moja kuwa mens rea ya kuua haikuwepo!.
  4. Siku ikifika, kesi hiyo itatajwa na kusikilizwa kwa siku moja tuu, ambapo mshitakiwa atasomewa kesi yake na mahakama itamuuliza kama analo la kujibu, wakili wake ataieleza mahakama kuwa mshtakiwa amekiri kosa, mahakama itathibitisha kwa kumsikiliza na kumsikiliza, kama hata kanusha kukiri kosa, then kesi hiyo itafungwa kwa kusikiliza final submission za mawakili wa pande zote, kisha mshtakiwa atapewa fursa ya kujitetea na kesi itakamilishwa na kupangiwa siku ya hukumu.
  5. Kwa vile hii ni public interest case, siku ya hukumu, mahakama itatoa adhabu kali ya zuga tuu ili kutuliza hasira za Watanzania ila mtuhumiwa hatatumikia adhabu hiyo!. Ila kisheria, maadamu hakuna mens rea, mshitakiwa angepaswa kuhukumiwa kwa adhabu ndogo tuu ya negligence kwenye matumizi ya silaha hivyo kusababisha kifo!. Kifo hicho kitahesabika kama kifo cha ajali kazini na kesi itakwisha.
  6. Akisha hukumiwa biashara ya kiserikali na jinai inakuwa imeishia hapo, jamaa atapelekwa gerezani siku mbili tatu na kuachiwa huru na kutafutiwa kazi nyingine ya kawaida na kendesha maisha yake ila sio eneo lile tena asije tambulika!.
  7. Familia ya marehemu wana uwezo wa kufungua kesi ya madai dhidi ya serikali kwa kifo cha mpendwa wao na serikali italipa fidia nono fasta fasta kupooza hasira za familia.
  8. Kihalisia, waziri wa mambo ya ndani na waziri wa usalama wa taifa na IGP walipaswa kujiuzulu kama ile kesi ya mauaji Mwanza, waziri wa mambo ya ndani Ali Hasaan Mwinyi na Waziri wa usalama Peter Siyovelwa na igp, Saimon Pundugu walijiuzulu!.
  9. RPC, RSO, OCD na DSO, walipaswa wote kuunganishwa kwenye kesi hiyo lakini polisi wametumia ujanja kumshauri mmoja tuu ajitolee kuwa mbuzi wa kafara ila wengine wote waokoke japo this time, hawatafanikiwa kirahisi kama wanavyodhani!.
  10. All and all, damu ya Daudi Mwangosi haikumwagika bure, things will never be same again kwa polisi kutumia nguvu kubwa kuliko inayohitajika katika maandamano yoyote na hili limethibitishwa na maandamano ya Waislamu yaliyofuatia kifo hiki!.

Pasco.
Naibu Kamishna Mstaafu wa Polisi (DCP) Michael Kamuhanda amefariki Januari 29, 2026 majira ya Asubuhi katika Hospitali ya Bugando Jijini Mwanza alikokuwa anapatiwa Matibabu.

Huyu jamaa ndo aliamuru Mwandishi wa Habari wa CHANNEL TEN, Daud Mwangosi apigwe Bomu huko Nyololo Iringa. Kiko wapi?

Alimtuhumu kuipendelea CHADEMA katika kutoa habari.


View attachment 3536781
Kamanda Kamuhanda, asante kwa utumishi wako dunia hii, kuna yule mwanahabari mwenzetu, Daudi Mwangosi, kwa vile yeye alitangulia, basi atakupokea, mtamalizana nae kwanza, ndipo ukamalizane na Sir God.

RIP Kamanda Polisi Michael Kamuhanda

RIP Kamanda Habari Daudi Mwangosi

Paskali
 
Kamanda Kamuhanda, asante kwa utumishi wako dunia hii, kuna yule mwanahabari mwenzetu, Daudi Mwangosi, kwa vile yeye alitangulia, basi atakupokea, mtamalizana nae kwanza, ndipo ukamalizane na Sir God.

RIP Kamanda Polisi Michael Kamuhanda

RIP Kamanda Habari Daudi Mwangosi

Paskali
Good riddance to bad rubbish.
 
Back
Top Bottom