Kama Wakenya wameweza, sisi tunashindwa kwenda kujifunza kwao?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,695
6,398
Inasemekana, kuna wakati Wakenya walikuwa wanakuja Tanzania, nafikiri Gairo, kununua viazi mviringo na kwenda kuvifsafisha, kuvigrade, na kuvifanyia packaging kisha kuvisafirisha kwenda sokoni Dubai.

Inasemekana, Wakenya hua wanavifuata vitunguu Tanzania, si kwa ajili ya kuviuza Kenya, bali nchi za nje hasa Dubai.

Inasemekana, hata Wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite, kwa miaka ya nyuma, walikuwa wanapendelea zaidi kuuza madini yao Kenya kuliko nchini. Inaonekana kulikuwa na cha ziada walichokuwa wanakipata huko, vinginevyo, wasingejihatarisha kiasi hicho kutorosha madini mpaka Kenya.

Inasemekana, miaka ya nyuma , Kenya ilikuwa ikisafirisha Tanzanite nyingi zaidi kuliko Tanzania, nchi pekee duniani Tanzanite inakopatikana.

Inasemekana, miaka ya nyuma, Wakenya walikuwa wakifuata parachichi nchini Tanzania. Kipindi hicho, parachichi zilikuwa na bei nzuri, lakini walipoacha kufanya hivyo, wakulima wa Tanzania wakaambulia maumivu. Na hayo maparachichi, Wakenya walikuwa wakienda kuyasafirisha kwenda "ng'ambo".

Inavyoonekana, Wakenya wako vizuri zaidi kwenye biashara za "Kimataifa" kuwazidi Watanzania.

Wakenya ni "ndugu" zetu, kama wao wameweza, kwa nini sisi tushindwe?

Haitakuwa jambo jema endapo tutaamua kwenda kujifunza kwao?

Binafsi ninafikiria nimtafute Mkenya aliye vizuri kwenye hilo eneo ili nimfanye "mentor" wangu.

Tanzania tuna fursa nyingi sana. Tunachohitaji ni IDEA EXPLOSION!
 
Sio inasemakana. Mpaka sasa hivi soko la mazao ya Tanzania liko Kenya. Pia hata soko lenye bei nzuri ya madini kuanzia Tanzanite mpaka dhahabu liko Kenya. Pia hata mafuta ya Alizet yananunuliwa kwa wingi na Kenya kisha kule yanafanyiwa pakeging na nembo za Kenya yanasafirishwa nje. Kwa ujumla Kenya wametuzidi ktk mambo mengi. Kikubwa hata elimu wametuzidi.
 
Sio inasemakana. Mpaka sasa hivi soko la mazao ya Tanzania liko Kenya. Pia hata soko lenye bei nzuri ya madini kuanzia Tanzanite mpaka dhahabu liko Kenya. Pia hata mafuta ya Alizet yananunuliwa kwa wingi na Kenya kisha kule yanafanyiwa pakeging na nembo za Kenya yanasafirishwa nje. Kwa ujumla Kenya wametuzidi ktk mambo mengi. Kikubwa hata elimu wametuzidi.
Wanasema mchawi mpe mwanao akulelee! Hatuwezi "kuwarubuni" Wakenya ili watupatie maujuzi yao?
 
Kenya wametuacha mbali Kwa vitu mbalimbali , hatuwezi kufanya vitu wanavyofanya kibiashara Maana wao tayari mazingira yanawasupport ,Sisi huku Ni uhuni ,ujuaji ,mlolongo mwingi kwenye kuhakikisha biashara inafika nje ....
Mkuu, naomba uuondoe huo msamiati wa "hatuwezi", tunataka na sisi tuweze kama wao, na zaidi.

Tufanyeje ili tuwe bora kuwazidi?
 
Wanasema mchawi mpe mwanao akulelee! Hatuwezi "kuwarubuni" Wakenya ili watupatie maujuzi yao?
Ni watu hatari sana hao, usithubutu kukaa na mkenya ukafanya nao makubariano nao kibiashara,watakupiga tu.
Pia kutafuta biashara za nje ni rahisi sana. Tatizo linakuja kwa nchi yetu,viongozi wa nchi hii ni kama hawataki Watanzania wainuke kiuchumi. Kwanza ukitaka tu kupeleka bidhaa kama hizo nje ukiritimba unaanzia hapa. Itatakiwa vibali vingi uvilipie. Kwa hiyo mwisho watu wanakata tamaa kufuatia ukiritimba uliopo.
Lakini huko nje soko ni kubwa sana la mazao,shida mpaka wewe kupata hivyo vibali vya export ndio pagumu. Wenzetu Wakenya wamerahisishiwa na wanasaidiwa na serikali mtu akijitokeza kutaka kufanya hivyo
 
Tuliwacheka walipowakumbatia wazungu baada ya Uhuru, na sisi tukawafukuza kama paka mwizi na kuwaambia imetosha na uhuru mmetupa kwaherini kana kwamba tutaweza

Wenzetu mpaka leo kuna wazungu wenye mashamba huko na wao (wazungu) ndio waliowafundisha kila kitu kuanzia ukulima wa faida mpaka packaging na usafirishaji

Wao wamefanikiwa hata kwenye mashamba ya chai na ndio mpaka Ulaya tunakunywa chai yao na makampuni makubwa kama Unilever ni kubwa sana na ndio wanunuzi wao wakubwa wanatengeneza PG tips
Ukija kwenye soko la mboga na matunda kwa mfano Western International Market ya West London utakuta bidhaa nyingi zinatoka Kenya
Ila Tz hutaona hata nyanya moja lakini za Uganda pia zipo bidhaa nyingi tu na mimi ni mnunuzi mkubwa hapo

Wenzetu wametuzidi sana kwa sababu ya elimu na pia vibali kupata ni balaa kwa Tz ila bidhaa zetu nyingi zinaenda Kenya na mpaka South Africa ila zinaandikwa zimetoka huko
Sisi wakulima ni dhalili sana wakati wao mkulima ana nguvu haswa
 
Ni watu hatari sana hao, usithubutu kukaa na mkenya ukafanya nao makubariano nao kibiashara,watakupiga tu.
Pia kutafuta biashara za nje ni rahisi sana. Tatizo linakuja kwa nchi yetu,viongozi wa nchi hii ni kama hawataki Watanzania wainuke kiuchumi. Kwanza ukitaka tu kupeleka bidhaa kama hizo nje ukiritimba unaanzia hapa. Itatakiwa vibali vingi uvilipie. Kwa hiyo mwisho watu wanakata tamaa kufuatia ukiritimba uliopo.
Lakini huko nje soko ni kubwa sana la mazao,shida mpaka wewe kupata hivyo vibali vya export ndio pagumu. Wenzetu Wakenya wamerahisishiwa na wanasaidiwa na serikali mtu akijitokeza kutaka kufanya hivyo
Mkuu, mbona mimi nawaamini sana Wakenya?.

Siamini kama kuna mtu anyeweza "kunipiga"

Anipige mimi nikiwa wapi? Kika kitu tutaifanya kwa kuzingatia kanuni, taratibu, na vigezo.
 
Sidhani kama mtaji ni tatizo. Kuna Watanzania wengi wenye mamilioni yasiyo na "kazi" lakini hawataki hata kusikia suala la kulima.
Mkuu usiwaone wakenya wanakuja wale hawaji na lakisaba 🤣🤣🤣🤣. Wale wamejipanga ohoo! Ngoja nikuelezee. Kuna jamaa yangu alikuwa kwenye hizo ishu alinipaga ufafanuzi wakina. Ngoja nieleze kwa urefu, samahani kama nitakosea (spellings natype fastafasta).


1. Kwanza ili uweze kuexport vitu kwenda soko la Ulaya, Marekani, Uarabuni, UAE, Dubai, Saudi Arabia. Lazima uwe na vibali ambavyo vinalipiwa pesa, uwe na vibali vya ubora kama ISO standards,EU standards, Halal standards. Hapo pesa inahitajika

2. Uwe na mtaji wa kununua mazao na kusafirisha mazao mpaka sehemu husika. Hapo pesa inahitajika

3. Uwe na eneo ambalo linakidhi ubora wa kimataifa kwa ajili ya packing, wafanyakazi, mitambo ya packaging. Maana yake ama ujenge kiwanda au ukodi jengo lenye vigezo ndio uanze uzalishaji. Na ili upate certificate ya kimataifa inabidi jengo liwe lako sasa piga hesabu ya kununua kiwanja cha Light industry au heavy industry mpaka unapata hati ya kiwanja ushatoa rushwa mpaka umechoka 🤣🤣, kujenga jengo kwa designs,michoro na ubora wa kimataifa EU,USA, ISO standards ni pesa 🤣, kuvuta umeme hapo ni kuwapa rushwa tanesco mpaka wakuletee umeme umeshachoka 🤣🤣, kuweka mitambo hapo kutafuta mitambo inayotoa bidhaa yenye ubora wa kimataifa na mpaka uitoe mitambo bandarini ushatoa rushwa ya kutosha 🤣🤣, kulipa wafanyakazi ambao wana ujuzi wa kuzalisha bidhaa yenye ubora wa kimataifa sio kulipualipua🤣 , mpaka kufikisha ubora wa kimataifa umechoka🤣🤣🤣. Hapo ni pesa tu inahitajika

4. Uwe na uwezo wakutafuta container special la kusafirisha mazao na kulipakiaa ama kwenye meli au ndege. Hapo ni pesa inahitajika

5. Uwe na connection ya upande wa pili wa unakopeleka na hao unakoexport lazima uwalipe. Na mzigo kufika mpaka kwa mteja lazima ulipe. Hapo pesa inahitajika

6. Uwe na pesa ya marketing ya bidhaa unayozalisha, na kuhudhuria international exhibition mara kwa mara ili kupata wateja wakubwa. Hapo hela inahitajika.

7. Bado kuna kulipa kodi na usafiri wa pande zote mbili, nchi unayotoa mzigo na unakopeleka, hapo kwa Tanzania mpaka uzungushwe na kusumbuliwa kweli kweli 🤣. Na Hapo hela inahitajika.



Baada ya harakati zote hizo ndio sasa unaanza kuingiza hela.

Huo mchakato wa kuzalisha bidhaa za kuexport unataka hela na ubora wa kimataifa. Ukifanya kosa moja TU umekula hasara. Mzigo kama hauna ubora wa kimataifa unatupwa. Huko wenzetu wako very serious, sio huku ukitoa rushwa mzigo feki unavuka 🤣

Ndio maana matajiri wa kibongo hawapo kwenye viwanda vya kuexport vitu kwenda soko la kimataifa. Wao wapo kwenye biashara za kuagiza vitu dubai,china, uturuki. Weka kwenye stoo na madukani unauza unapata hela bila usumbufu. Au wanajenga mahoteli na mabar mkalewe humo na kuzagamuana humo wao waingize hela. Au wanajenga sheli, mkaweke mafuta waingize hela fasta. Au wanajenga shule, mlipie ada watoto wao waingize hela. Au wananunua malori na macontena na mafuta, yapige safari za Congo, Zambia, Rwanda, Burundi, waingize hela. Au wanaweka viwanda vya unga wa ngano, juisi, energy drinks, pombe, mnunue mnywe/mle waingize hela. Au wananunua mabasi ya mkoani, weka nauli pandeni safirini, wao wanaigiza hela.

Sekta ya kuexport vitu sio rahisi kama unavyofikiria. Hao wakenya wamejipanga na ni wazoefu. Msiwachukulie poa.
 
Tuliwacheka walipowakumbatia wazungu baada ya Uhuru, na sisi tukawafukuza kama paka mwizi na kuwaambia imetosha na uhuru mmetupa kwaherini kana kwamba tutaweza

Wenzetu mpaka leo kuna wazungu wenye mashamba huko na wao (wazungu) ndio waliowafundisha kila kitu kuanzia ukulima wa faida mpaka packaging na usafirishaji

Wao wamefanikiwa hata kwenye mashamba ya chai na ndio mpaka Ulaya tunakunywa chai yao na makampuni makubwa kama Unilever ni kubwa sana na ndio wanunuzi wao wakubwa wanatengeneza PG tips
Ukija kwenye soko la mboga na matunda kwa mfano Western International Market ya West London utakuta bidhaa nyingi zinatoka Kenya
Ila Tz hutaona hata nyanya moja lakini za Uganda pia zipo bidhaa nyingi tu na mimi ni mnunuzi mkubwa hapo

Wenzetu wametuzidi sana kwa sababu ya elimu na pia vibali kupata ni balaa kwa Tz ila bidhaa zetu nyingi zinaenda Kenya na mpaka South Africa ila zinaandikwa zimetoka huko
Sisi wakulima ni dhalili sana wakati wao mkulima ana nguvu haswa
Bora mkuu uko huko! Hutafuti kufikiri "nje" ya boksi, bali unaishi nje ya boksi.

Tushauri tuliopo huku nyumbani, tunawezaje na sisi kufikisha huko mboga na matunda tunayolima?
 
Mkuu usiwaone wakenya wanakuja wale hawaji na lakisaba 🤣🤣🤣🤣. Wale wamejipanga ohoo! Ngoja nikuelezee. Kuna jamaa yangu alikuwa kwenye hizo ishu alinipaga ufafanuzi wakina. Ngoja nieleze kwa urefu, samahani kama nitakosea (spellings natype fastafasta).


1. Kwanza ili uweze kuexport vitu kwenda soko la Ulaya, Marekani, Uarabuni, UAE, Dubai, Saudi Arabia. Lazima uwe na vibali ambavyo vinalipiwa pesa, uwe na vibali vya ubora kama ISO standards,EU standards, Halal standards. Hapo pesa inahitajika

2. Uwe na mtaji wa kununua mazao na kusafirisha mazao mpaka sehemu husika. Hapo pesa inahitajika

3. Uwe na eneo ambalo linakidhi ubora wa kimataifa kwa ajili ya packing, wafanyakazi, mitambo ya packaging. Maana yake ama ujenge kiwanda au ukodi jengo lenye vigezo ndio uanze uzalishaji. Na ili upate certificate ya kimataifa inabidi jengo liwe lako sasa piga hesabu ya kununua kiwanja cha Light industry au heavy industry mpaka unapata hati ya kiwanja ushatoa rushwa mpaka umechoka 🤣🤣, kujenga jengo, kuvuta umeme hapo ni kuwapa rushwa tanesco mpaka wakuletee umeme umeshachoka 🤣🤣, kuweka mitambo hapo kutafuta mitambo inayotoa bidhaa yenye ubora wa kimataifa na mpaka uitoe mitambo bandarini ushatoa rushwa ya kutosha 🤣🤣, kulipa wafanyakazi ambao wana ujuzi wa kuzalisha bidhaa yenye ubora wa kimataifa sio kulipualipua🤣 , mpaka kufikisha ubora wa kimataifa umechoka🤣🤣🤣. Hapo ni pesa tu inahitajika

4. Uwe na uwezo wakutafuta container special la kusafirisha mazao na kulipakiaa ama kwenye meli au ndege. Hapo ni pesa inahitajika

5. Uwe na connection ya upande wa pili wa unakopeleka na hao unakoexport lazima uwalipe. Na mzigo kufika mpaka kwa mteja lazima ulipe. Hapo pesa inahitajika

6. Uwe na pesa ya marketing ya bidhaa unayozalisha, na kuhudhuria international exhibition mara kwa mara ili kupata wateja wakubwa. Hapo hela inahitajika.

7. Bado kuna kulipa kodi na usafiri wa pande zote mbili, nchi unayotoa mzigo na unakopeleka, hapo mpaka uzungushwe na kusumbuliwa kweli kweli 🤣. Na Hapo hela inahitajika.



Baada ya harakati zote hizo ndio sasa unaanza kuingiza hela.

Huo mchakato wa kuzalisha bidhaa za kuexport unataka hela na ubora wa kimataifa. Ukifanya kosa moja TU umekula hasara. Mzigo kama hauna ubora wa kimataifa unatupwa. Huko wenzetu wako very serious, sio huku ukitoa rushwa mzigo feki unavuka 🤣

Ndio maana matajiri wa kibongo hawapo kwenye viwanda vya kuexport vitu kwenda soko la kimataifa. Wao wapo kwenye biashara za kuagiza vitu dubai,china, uturuki. Weka kwenye stoo na madukani unauza unapata hela bila usumbufu. Au wanajenga mahoteli na mabar mkalewe humo na kuzagamuana humo wao waingize hela. Au wanajenga sheli, mkaweke mafuta waingize hela fasta. Au wanajenga shule, mlipie ada watoto wao waingize hela. Au wananunua malori na macontena na mafuta, yapige safari za Congo, Zambia, Rwanda, Burundi, waingize hela. Au wanaweka viwanda vya unga wa ngano, juisi, energy drinks, pombe, mnunue mnywe/mle waingize hela. Au wananunua mabasi ya mkoani, weka nauli pandeni safirini, wao wanaigiza hela.

Sekta ya kuexport vitu sio rahisi kama unavyofikiria. Hao wakenya wamejipanga na ni wazoefu. Msiwachukulie poa.
Mkuu, unataka kusema hatuwezi kuwafikia?

Kwani wao walizaliwa na hayo mafanikio?
 
Mfumo wenyewe unatupiga kichwani, ukionyesha kutaka kutoboa serikali hiyo hapo na makodi kibao.

Hata kuonyesha support ili upasue njia mbele huko wao utawaona 'unadaiwa kodi ya miaka 6'.

Wenzetu wanapeana support plus serikali kuweka mazingira rafiki, mfano kupata passport au Visa hadi hapo unakata tamaa.
 
Back
Top Bottom