UTAFITI: Watanzania Mungu wetu ni mmoja, tena mwenye nguvu na wa kweli, ila wenyewe hatujui tu

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,860
12,293
Habari za asubuhi wanaJF wenzangu?

Ndugu zangu.. binafsi nimekuwa msikilizaji, mfuatiliaji, mtafiti na mchunguzaji wa kila kilichopo au kinachotokea katika nchi yetu. Katika kusikiliza, kufuatilia, kutafiti na kuchunguza huko, nimeweza kugundua kwamba Tanzania tuna Mungu mmoja, mwenye nguvu na wa kweli (haijalishi utofauti wa dini zetu nk)

Najua hapa kuna watu wanaotaka kujua ni kwa nini mimi nimewaza na kuamini kwamba watanzania Mungu wetu ni mmoja. Sasa naomba usome chini ili uelewe zaidi vigezo nilivyotumia kugundua hili.

1. Kupewa nchi yenye kila aina ya resources ambazo nchi zingine hazina. Kumbuka au fahamu kwamba Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa resource nyingi katika East Africa Country au inaweza kuwa ya kwanza au ya pili Africa nzima. Hapa nikiwa na maana kuwa hata hiyo Kongo tunayoambiwa kuwa ina resource nyingi, bado haifikii zile tulizonazo sisi, mfano Congo hawana mlima wenye hadhi ya huu wa kwetu (mlima Kilimanjaro)ambao ndio mlima wa pili kwa ukubwa duniani, pili Congo hawana madini haya tulionayo sisi (Tanzanite) madini ambayo yanapatina Tanzania tu, na sio nchi nyingine yoyote hapa duniani.

Hapo bado sijazungumzia bahari, mito, milima mingine, mabonde na ardhi yenye rutuba nzuri hadi kupelekea baadhi ya nchi zilizopo jirani yetu kuitamani ardhi yetu (kumbuka vita ya Idi Amini kujaribu kuivamia na kuiteka ardhi yetu, mgogoro wa Tanzania na Malawi kuhusu mipaka yetu nk.

2. Ulinzi wa nchi ambao nchi nyingi hazina. I mean baada ya kupata uhuru Tanzania tuliingia katika migogoro mbali mbali ya ndani na nje ambayo ilikuwa ina nia au lengo la kuhatarisha usalama wa nchi yetu. Lakini kwa vile nchi yetu ina ulinzi wa Mungu wetu basi nia na malengo hayo yalishindwa vibaya sana.
Mfano kulikuwa na majaribio ya kumpindua raisi Nyerere mara mbili, lkn majaribio hayo ambayo pengine baadae yangetengeneza mgogoro na mgawanyiko mkubwa wa taifa ambao pengine ungeendelea hadi sasa yalishindwa.

Idi Amini nae alipojaribu kutuvamia Mungu wetu alimuadhibu vibaya na kuionesha dunia kwamba chini ya ulinzi wake sisi hatuwezi kuvamiwa na kushindwa na mtu au nchi yoyote.

Hata kipindi cha kuwasaidia ndugu zetu wa nchi za kusini kupigania uhuru wao. Makaburu waliweza kutuma mashushu, wanajeshi nk kuvamia na kuziadhibu nchi zote zilizojaribu kuwapa hifadhi wanasiasa weusi waliokuwa wamekimbia mateso katika nchi yao, lkn makaburu hao walipojaribu kutumia mbinu hizo kwa nchi yetu walishindwa na wale mashushu wao wote tuliwagundua na kuwatia nguvuni before ya kuleta madhara makubwa nchini kwetu, hivyo hivyo wareno tuliwachapa na kumuweka Samora Machel kitini kwa kutumia nguvu na ulinzi tuliopewa na Mungu wetu.

3. Umoja wetu na mshikamano wetu. Tanzania ni moja ya nchi chache ambazo raia wake tuna Umoja, Upendo na Mshikamano wenye nguvu sana. Ukienda Burundi Kuna matabaka mawili mawili nayo ni:
a) tabaka la wahutu na watusi.
b) tabaka la waongea kiswahili na kirundi.

Tabaka "A" kutokana nchi yao haina ulinzi wa Mungu kama tulio nao sisi ndio lililotumika kuleta vita kubwa nchini kwao, vita ambayo imeacha makovu mengi ndani ya mioyo yao. Pamoja na kwamba kwa sasa wanasema yale mambo ya ukabila yameisha na nchi umekuwa kitu kimoja, lkn unaona kabisa bado hakuna kuaminiana katika ya mtusi na mhutu (hiyo itakuwa hivyo hata ipite miaka 100)

Ukienda Kenya huko licha ya nchi yao kuwa na makabila zaidi ya kumi tofauti lkn bado ukabila umetamalaki kuanzia serikalini, masokoni, madukani nk. Japo Kenyata alijaribu kutaka kuwaunganisha wakenya kupitia lugha ya kiswahili baada ya kujifunza msingi huo kutoka kwa Nyerere, lkn alishindwa kutokana na swala la ukabila kupewa kipaumbele kuliko utaifa.

Ukienda Kenya maeneo ya sokoni utakuta kila mtu anaongea lugha yake na wengine hawaelewani kabisa.

Rwanda, Uganda, Congo nk ni vilevile tu Umoja wao ni wa kuunga unga na kuizuga dunia, lkn ndani ya mioyo yao imejaa mgawanyiko wa makabila, lugha nk.

4. Nguvu ya asili. Pia tumepewa nguvu ya asili ya kuweza kuwadhibiti au kuzidhibiti njia zote zinazoweza kutumika kujaribu kutuangusha. Kama nilivyotoa mfano kuhusu msumbiji na Kaburu kushindwa, lkn pia tumepewa nguvu ya kuweza kuleta Amani hata katika nchi zingine tulizoamua kwenda kuwasaidia kama Comoro nk.

Hata juzi kati Kagame alijaribu kutingisha kibiriti, za ndani kabisa zinasema kama isingekuwa mzee Mwinyi (mzee wa amani na hekima) kuzituliza zile jazba za kijana wa msoga basi leo Rwanda ingekuwa ishaonganishwa kuwa mmoja wa mikoa ya Tanzania, maana kijana wa msoga akishirikiana na mkuu wa jeshi wa kipindi hicho ambae alikuwa na hamu ya kuikamata Kigali usiku mmoja, hivyo akawa anamshawishi mkubwa wake atoe amri akamalize mechi na ubishi wa kijinga jinga wa bwana PK.

Nchi kwetu pia tulishuhudia wale wote waliojaribu kuteteresha amani yetu kupitia dini na siasa wakishindwa vibaya kabla hata ya kuanza.

Kwa resource tulizokuwa nazo na wema tulionao toka enzi za mwl Nyerere wa kukaribisha wakimbizi, na waafrika wenzetu kutoka nchi mbali mbali kama isingekuwa ulinzi wa Mungu basi leo hii nchi ingekuwa kama Congo au Msumbiji ambazo leo hii zipo kwenye vita isiyoisha.

Demokrasia imeshaleta machafuko almost Afrika nzima, lkn kwetu hiyo haijatokea na naamini hatatokea kamwe.

Kwahiyo nashauri viongozi wa serikali, dini na siasa waendelee kutuasa watanzania tupendane na tusibaguane kwa misingi ya dini, rangi, kabila, siasa, jinsia nk. Maana sisi wote Mungu wetu ni mmoja, mwenye Nguvu na Upendo wa kweli na sisi. Yeye anaangalia mioyo yetu tu, na sio dini zetu au rangi zetu.

Mungu ibariki Tanzania.
Ibariki serikali yetu na raisi wetu.
Bariki pia bara letu na dunia yetu kwa ujumla.

Ameen 🤲
 
Kuna watu ni wafia mifumo iliyokuja kuwatawala na sio nchi yao na ndugu zao watanzania.

Wako tayari waibe na kupeleka kwa waleta ukoloni na hata kuwa vibaraka wao na kuwasaliti watanzania na Tanzania yao.
 
Mungu alitupendelea sana watanganyika. Mbali na rasilimali nyingi kuwepo, Tanganyika ni taifa lenye utajiri wa rasilimali watu(Ethnical Diversity). Tamaduni za watu tofauti zaidi ya 120 wanaoishi kwa amani kunaweza kuritajirisha mno taifa kiutamaduni. Culture, Arts, Sports, Laws, Spirituality and Medicine, owe their roots to Collective Ethnic Diversity.

Tatizo kubwa ni kwamba mbali na Mzee Nyerere kujenga msingi mzuri mwanzoni kuna, maeneo alikosea sana. Mojawapo ni muungano, na jingine ni kutaka kutumia siasa kuendesha kila nyanja ya maisha ya binadamu akitaka kumuiga Karl Marx. Hili liliingilia sana makuzi na maendeleo ya saikolojia ya jamii za kitanzania (It affected, thwarted and slowed down the growth of collective psychology).

Leo hii Tanzania imeingia kwenye mgogoro mkubwa na usio na kichwa wala miguu, kwasababu watanganyika tulipuuza utaifa wetu tukitaka kuchanganya mafuta na maji. Kiukweli Tanganyika na Zanzibar haziwezi kushikama na kuwa kitu kimoja hata siku. Tukiendelea kulazimisha hili kwa kuzingatia siasa, na kusahau kwamba hawa watu wawili hata kupendana hawapendani tutaendelea kulivuruga hili taifa.

Binafsi nadhani ni wakati muafaka wa kukaa chini na kuzungumza hatma ya huu muungano, ambao umekuwa kero na maumivu tangu siku ya kwanza ulipozaliwa. Tanganyika iende zake kiamani na Zanzibar iende zake kiamani, kila mtu ajenge kwake.
 
Kuna watu ni wafia mifumo iliyokuja kuwatawala na sio nchi yao na ndugu zao watanzania.

Wako tayari waibe na kupeleka kwa waleta ukoloni na hata kuwa vibaraka wao na kuwasaliti watanzania na Tanzania yao.
Umeandika ukweli ndugu yangu, lkn Mungu wetu ni mwenye nguvu na uwezo.

Najua kuna siku watashindwa tu kama walivyoshindwa hao waliotutawala kabla ya uhuru.
 
Mungu alitupendelea sana watanganyika. Mbali na rasilimali nyingi kuwepo, Tanganyika ni taifa lenye utajiri wa rasilimali watu(Ethnical Diversity). Tamaduni za watu tofauti zaidi ya 120 wanaoishi kwa amani kunaweza kuritajirisha mno taifa kiutamaduni. Culture, Arts, Sports, Laws, Spirituality and Medicine, owe their roots to Collective Ethnic Diversity.

Tatizo kubwa ni kwamba mbali na Mzee Nyerere kujenga msingi mzuri mwanzoni kuna, maeneo alikosea sana. Mojawapo ni muungano, na jingine ni kutaka kutumia siasa kuendesha kila nyanja ya maisha ya binadamu akitaka kumuiga Karl Marx. Hili liliingilia sana makuzi na maendeleo ya saikolojia ya jamii za kitanzania (It affected, thwarted and slowed down the growth of collective psychology).

Leo hii Tanzania imeingia kwenye mgogoro mkubwa na usio na kichwa wala miguu, kwasababu watanganyika tulipuuza utaifa wetu tukitaka kuchanganya mafuta na maji. Kiukweli Tanganyika na Zanzibar haziwezi kushikama na kuwa kitu kimoja hata siku. Tukiendelea kulazimisha hili kwa kuzingatia siasa, na kusahau kwamba hawa watu wawili hata kupendana hawapendani tutaendelea kulivuruga hili taifa.

Binafsi nadhani ni wakati muafaka wa kukaa chini na kuzungumza hatma ya huu muungano, ambao umekuwa kero na maumivu tangu siku ya kwanza ulipozaliwa. Tanganyika iende zake kiamani na Zanzibar iende zake kiamani, kila mtu ajenge kwake.
Dah mkuu we acha tu...

Ulichoandika kinafikirisha sana.
 
Dah mkuu we acha tu...

Ulichoandika kinafikirisha sana.
Ni jambo la ajabu kuukataa utaifa wako, Mungu hakukosea kukuumba wewe Mtanganyika. Msingi wa huu muungano ni utaifa wa Tanganyika na Zanzibar ambayo ndiyo mataifa yaliyopata uhuru. Tanzania haijawahi kutawaliwa na mkoloni, wala haijawahi kupata uhuru. Tunapotaka kuukataa huu ukweli ndiyo matatizo huanza. Tanzania ni chombo cha kisiasa kilichotengenezwa kuyanganisha haya madola mawili, ya Tanganyika na Zanzibar.

Tanganyika ndiyo imebeba kumbukumbu za mababu zetu, siyo Tanzania. Tanganyika ndiyo ina makovu ya ukoloni, utumwa na ushahidi wa mapambano yetu dhidi ya watawala wa kigeni. Hii historia ndiyo inatuunganisha watanganyika wote. Historia ya Mkutano wa Berlin 1884-1885 ni ya Tanganyika, siyo Tanzania wala Zanzibar. Historia ya vita vya maji-maji ni ya Tanganyika, siyo Tanzania wala Zanzibar.

Wakati Tanganyika inagawanywa na wakolini kule Berlin, Zanzibari lilikuwa ni taifa tayari ambalo linatawaliwa na Sultan. Mbaya zaidi nalo lilitaka kushirikishwa kwenye ule mkutano likidai kwamba baadhi ya maeneo ya Tanganyika kama Arusha, Kilimanjaro, Mkondokwa na Usagara ni yake. Ushahidi upo unaonyesha Sultan wa Zanzibar akiandika barua kwa mfalme wa Ujerumani kwamba kwanini yeye hukushirikishwa kwenye mkutano wa Berlin.

Hivi unadhani ni jambo sahihi kusema kwamba siku ya uhuru wa Tanganyika ndiyo siku ya uhuru wa Tanzania, ilhali Zanzibari hajapitia mambo yale ambayo sisi watanganyika tumepitia, ??

Kutaka kulazimisha kwamba uhuru wa Tanganyika ndiyo uhuru wa Tanzania ni kukosa hekima na kuzitukana kumbukumbu za mababu zetu kwasababu za kisiasa. Zanzibar hawataki huu muungano kwasababu wamekuwa na utaifa wao kwa zaidi ya miaka 200. Sisi utaifa wetu umeanza mwaka 1961, bahati mbaya ukabakwa na wajamaa kwasababu wanazozijua wenyewe.
 
Habari za asubuhi wanaJF wenzangu?

Ndugu zangu.. binafsi nimekuwa msikilizaji, mfuatiliaji, mtafiti na mchunguzaji wa kila kilichopo au kinachotokea katika nchi yetu. Katika kusikiliza, kufuatilia, kutafiti na kuchunguza huko, nimeweza kugundua kwamba Tanzania tuna Mungu mmoja, mwenye nguvu na wa kweli (haijalishi utofauti wa dini zetu nk)

Najua hapa kuna watu wanaotaka kujua ni kwa nini mimi nimewaza na kuamini kwamba watanzania Mungu wetu ni mmoja. Sasa naomba usome chini ili uelewe zaidi vigezo nilivyotumia kugundua hili.

1. Kupewa nchi yenye kila aina ya resources ambazo nchi zingine hazina. Kumbuka au fahamu kwamba Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa resource nyingi katika East Africa Country au inaweza kuwa ya kwanza au ya pili Africa nzima. Hapa nikiwa na maana kuwa hata hiyo Kongo tunayoambiwa kuwa ina resource nyingi, bado haifikii zile tulizonazo sisi, mfano Congo hawana mlima wenye hadhi ya huu wa kwetu (mlima Kilimanjaro)ambao ndio mlima wa pili kwa ukubwa duniani, pili Congo hawana madini haya tulionayo sisi (Tanzanite) madini ambayo yanapatina Tanzania tu, na sio nchi nyingine yoyote hapa duniani.

Hapo bado sijazungumzia bahari, mito, milima mingine, mabonde na ardhi yenye rutuba nzuri hadi kupelekea baadhi ya nchi zilizopo jirani yetu kuitamani ardhi yetu (kumbuka vita ya Idi Amini kujaribu kuivamia na kuiteka ardhi yetu, mgogoro wa Tanzania na Malawi kuhusu mipaka yetu nk.

2. Ulinzi wa nchi ambao nchi nyingi hazina. I mean baada ya kupata uhuru Tanzania tuliingia katika migogoro mbali mbali ya ndani na nje ambayo ilikuwa ina nia au lengo la kuhatarisha usalama wa nchi yetu. Lakini kwa vile nchi yetu ina ulinzi wa Mungu wetu basi nia na malengo hayo yalishindwa vibaya sana.
Mfano kulikuwa na majaribio ya kumpindua raisi Nyerere mara mbili, lkn majaribio hayo ambayo pengine baadae yangetengeneza mgogoro na mgawanyiko mkubwa wa taifa ambao pengine ungeendelea hadi sasa yalishindwa.

Idi Amini nae alipojaribu kutuvamia Mungu wetu alimuadhibu vibaya na kuionesha dunia kwamba chini ya ulinzi wake sisi hatuwezi kuvamiwa na kushindwa na mtu au nchi yoyote.

Hata kipindi cha kuwasaidia ndugu zetu wa nchi za kusini kupigania uhuru wao. Makaburu waliweza kutuma mashushu, wanajeshi nk kuvamia na kuziadhibu nchi zote zilizojaribu kuwapa hifadhi wanasiasa weusi waliokuwa wamekimbia mateso katika nchi yao, lkn makaburu hao walipojaribu kutumia mbinu hizo kwa nchi yetu walishindwa na wale mashushu wao wote tuliwagundua na kuwatia nguvuni before ya kuleta madhara makubwa nchini kwetu, hivyo hivyo wareno tuliwachapa na kumuweka Samora Machel kitini kwa kutumia nguvu na ulinzi tuliopewa na Mungu wetu.

3. Umoja wetu na mshikamano wetu. Tanzania ni moja ya nchi chache ambazo raia wake tuna Umoja, Upendo na Mshikamano wenye nguvu sana. Ukienda Burundi Kuna matabaka mawili mawili nayo ni:
a) tabaka la wahutu na watusi.
b) tabaka la waongea kiswahili na kirundi.

Tabaka "A" kutokana nchi yao haina ulinzi wa Mungu kama tulio nao sisi ndio lililotumika kuleta vita kubwa nchini kwao, vita ambayo imeacha makovu mengi ndani ya mioyo yao. Pamoja na kwamba kwa sasa wanasema yale mambo ya ukabila yameisha na nchi umekuwa kitu kimoja, lkn unaona kabisa bado hakuna kuaminiana katika ya mtusi na mhutu (hiyo itakuwa hivyo hata ipite miaka 100)

Ukienda Kenya huko licha ya nchi yao kuwa na makabila zaidi ya kumi tofauti lkn bado ukabila umetamalaki kuanzia serikalini, masokoni, madukani nk. Japo Kenyata alijaribu kutaka kuwaunganisha wakenya kupitia lugha ya kiswahili baada ya kujifunza msingi huo kutoka kwa Nyerere, lkn alishindwa kutokana na swala la ukabila kupewa kipaumbele kuliko utaifa.

Ukienda Kenya maeneo ya sokoni utakuta kila mtu anaongea lugha yake na wengine hawaelewani kabisa.

Rwanda, Uganda, Congo nk ni vilevile tu Umoja wao ni wa kuunga unga na kuizuga dunia, lkn ndani ya mioyo yao imejaa mgawanyiko wa makabila, lugha nk.

4. Nguvu ya asili. Pia tumepewa nguvu ya asili ya kuweza kuwadhibiti au kuzidhibiti njia zote zinazoweza kutumika kujaribu kutuangusha. Kama nilivyotoa mfano kuhusu msumbiji na Kaburu kushindwa, lkn pia tumepewa nguvu ya kuweza kuleta Amani hata katika nchi zingine tulizoamua kwenda kuwasaidia kama Comoro nk.

Hata juzi kati Kagame alijaribu kutingisha kibiriti, za ndani kabisa zinasema kama isingekuwa mzee Mwinyi (mzee wa amani na hekima) kuzituliza zile jazba za kijana wa msoga basi leo Rwanda ingekuwa ishaonganishwa kuwa mmoja wa mikoa ya Tanzania, maana kijana wa msoga akishirikiana na mkuu wa jeshi wa kipindi hicho ambae alikuwa na hamu ya kuikamata Kigali usiku mmoja, hivyo akawa anamshawishi mkubwa wake atoe amri akamalize mechi na ubishi wa kijinga jinga wa bwana PK.

Nchi kwetu pia tulishuhudia wale wote waliojaribu kuteteresha amani yetu kupitia dini na siasa wakishindwa vibaya kabla hata ya kuanza.

Kwa resource tulizokuwa nazo na wema tulionao toka enzi za mwl Nyerere wa kukaribisha wakimbizi, na waafrika wenzetu kutoka nchi mbali mbali kama isingekuwa ulinzi wa Mungu basi leo hii nchi ingekuwa kama Congo au Msumbiji ambazo leo hii zipo kwenye vita isiyoisha.

Demokrasia imeshaleta machafuko almost Afrika nzima, lkn kwetu hiyo haijatokea na naamini hatatokea kamwe.

Kwahiyo nashauri viongozi wa serikali, dini na siasa waendelee kutuasa watanzania tupendane na tusibaguane kwa misingi ya dini, rangi, kabila, siasa, jinsia nk. Maana sisi wote Mungu wetu ni mmoja, mwenye Nguvu na Upendo wa kweli na sisi. Yeye anaangalia mioyo yetu tu, na sio dini zetu au rangi zetu.

Mungu ibariki Tanzania.
Ibariki serikali yetu na raisi wetu.
Bariki pia bara letu na dunia yetu kwa ujumla.

Ameen
Tunahitaji tu bandari zetu

Siasa ni dini na Dini ni siasa lazima vichangameni

Tuepuke matapeli wa siasa
 
Tunahitaji tu bandari zetu

Siasa ni dini na Dini ni siasa lazima vichangameni

Tuepuke matapeli wa siasa
Nimeamini kuwa sio kila mlevi anaziweza pombe. Kuna wengine wanapenda pombe, lkn pombe haziwapendi.

Alieandika kuwa siasa sio dini na dini sio siasa ni nani?
Ni nani katika thread hii kaandika kuwa siasa na dini visichangamane.

Najua umekurupuka kuandika uharo wako kwenye thread yangu kwa lengo la kuokota viji "like" kutoka kwa walevi wenzako. Bahati nzuri walevi hao wamekupuuza baada ya kuona umekimbilia kuandika yalio nje ya kile nilichokiandika.
 
Back
Top Bottom