Tatizo unaongelea watu waliooa wanawake makahaba. Kama mwanamke alieolewa anajiheshimu hawezi kufanya huo ujinga hata kidogo. Bahati mbaya sana taarifa mbaya siku hizi ni nyingi kuliko mambo mazuri yaliyotuzunguka. Tukiacha ubinafsi na kuona hawa wanawake tunaowazungumzia kwa namna hasi kuwa ni dada zetu, mama zetu, wadogo zetu, mashemeji zetu na hata ndugu/jamaa zetu ambao wanastahili heshima, tusingekuwa tanaanzia thread kama hizi.
Ngoja nikuulize mtoa mada, kama dada yako angekuwa ameolewa na mtu anaefanya kazi ya shift, ungemshauri amuache dada ako? kuna wakati tuache kufikiria kwa kutumia moyo huku ubongo uko idle.