Mwaka 2005 hapo Tarime Secondary kuna jomba mmoja alikuwa ni classmate Msukuma huyo kutoka Magu ndani huko aliitwa Kija Charles.
Hiyo siku tupo prep, kuna mdada mmoja alikuwa na majini, akapandisha bana siku hiyo, watu taharuki, sasa yalivyokuwa yanazungumza yakamtaja huyo mlozi na alichotaka kumfanyia akashindwa. Kumbe yule jomba alishatomber dorm moja zima, la pili alikuwa kafika nusu, wadada wakaandamana kumtafuta huku kelele zikiwa zimetamalaki madarasani. Hakuonekana shule karibia wiki nzima.
Kumbe jamaa alikuwa anawatomber kichawi
wote wanatumia nguvu za giza mkuu kuna waziri mmoja rafiki yangu nilikuta kwake kawafungia waganga kama 30 hivi anawalisha kila kitu wamtengeneze mambo yake yawe mazuri na kweli amefanikiwa jiwe anamsikiliza hatari japokua jamaa ni bogus tu
Nisaidie mawasiliano yake boss
Hapo Kunduchi kuna ng'ombe zipo zinajifuga zenyewe na kuna siku nimetoka zangu kwenye mishe zangu saa nane kasoro ivi napishana na ng'ombe inaenda home aisee. Na hizo ng'ombe mtu hazigusi maana zinahusishwa na kusomewa albadiri kwa sababu inasemekana ziliibiwa kumbe zilipotea zenyewe kwa hiyo atakayezichukua cha moto kitampata.Nakumbuka miaka flani maeneo ya Pale kunduchi mtongani kuliku na mzee flani anaitwa x alikuwa anafuga mbuzi basi siku moja mbuzi wake alipotea maeneo ya benaco kule akaanza kulia kwa kuliita jina la yule mzee x mpk wananchi wanampeleka kwa yule mzee
Mimi nilishangaa pale mtakuja hizo ng'ombe zinavuka kwenye zebra na zenyewe zinaangalia kulia na kushoto kama kuna gari au hamna.hao mbuzi wanaojichunga huwa wabaya sana, usiwaguse, mbuzi anafunguliwa kwenye banda tu anajua mwenyewe pa kwenda, mbuzi kabla hajavuka barabara kwanza anageuka kulia na kushoto, ukiwaona waache!.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa Mtongani watoto tuliokulia pale tunakijua kile kijiji ni nomaMimi nilishangaa pale mtakuja hizo ng'ombe zinavuka kwenye zebra na zenyewe zinaangalia kulia na kushoto kama kuna gari au hamna.
Haahah,kuna kisa cha mpemba Mafia, alikua ameanika samaki wake baada ya kuwavua, ikafika mda akatoa mkeka akawa anapiga rakaa(Anaswali).Amemaliza kuswali kugeuka hamadi samaki wake wawili hawapo, akauliza kuna ntuu kachukua samaki zangu arudishee kila mtu akakakana akasema mi natoa dakika kumi tuu msiporudisha Walah! atakufa mtuu hapa na si masiharaa... Ebanaeee baaada ya dakika 10 zikaanguka kunguru mbili(hawa ndege Weusi) zimeshakaukaa zamani mdomoni wanamabaki ya samaki....
Sent using Jamii Forums mobile app
Jomba hiyo siku prep madem waliwaka hatari!
Ipo nyingine hujaamua kuionaGamboshi iko mpakani mwa magu na bariadi ila kiutawala iko bariadi,hiyo ya sengerema sijawahi isikia
Sent using Jamii Forums mobile app
mi nawaona sehemu nyingine, hao wa magomeni siwajui!Ilikua zamani wakati wachaga bado walikua wanashika dini. Wale wa Magomeni mwembe chai unewaona siku hizi?
Ilitokea miaka ya 2000 mwanzoni. Tulikuwa tunaishi karibu na shamba la miti ya kupandwa...sasa kuna kichochoro fulani hukatiza katikati ya shamba hilo. Tukiwa nje mida ya saa mbili kasoro nikisikiliza habari za michezo kutoka RTD tulishuhudia kama kijinga cha moto kikipita katika kile kijia...mwanzo tulijua mtu..ila kwa kasi ya ajabu kikakwea mtini huku kikitoa cheche. Sikumbuki kilichoendelea maana breki ya kwanza ilikuwa uvunguni.Wakuu habari zenu, ni matumaini yangu kuwa hamjambo.
Leo nataka kuweka ushuhuda wangu kwa niliyoyashuhudia live juu ya nguvu za giza, kwa wasioamini nadhani uzi huu hautakuwa na thamani kwao, kama na wewe unao ushuhuda usisahau kushea nasi.
1. Ushuhuda wangu unaanzia mwaka 1992 nikiwa nafundisha shule X wilaya ya Sengerema, kuna mwalimu nilikuwa nafundisha naye kituo kimoja.
Siku hiyo kuna kamvua kalinyesha sana, baada ya kupungua mwalimu mwenzangu alimuagiza mtoto wake wa kiume aliyekuwa akisoma darasa la kwanza kwenda kuchuma maharage shambani.
Bahati mbaya mtoto akiwa shambani aligongwa/aliumwa na nyoka na kupeleka kifo, tulifanya taratibu za mazishi na kumsitiri mtoto huyo.
Cha kushangaza mwaka 2008 mtoto huyo alionekana akiwa uchi na nywele ndefu sana alikuja moja kwa moja nyumbani na kupitiliza ndani nyumbani kwao, alikuwa ameshakuwa baba mzima, nywele zilikuwa ndefu sana pamoja na mikono iliyofikia usawa wa magoti.
Watu walistaajabu sana lakini hakudumu sana alifariki baada ya kukaa uraiani kwa wiki mbili.
2. Ushuhuda wangu bado unabaki huko huko Sengerema katika kijiji cha Bubandwamhela.
Nikiwa nafundisha shule X, kuna binti kijijini aliyekuwa akisoma darasa la saba aliugua ghafla baada ya kutoka shuleni.
Wazazi wake walipompeleka hospitali daktari aliwaambia mtoto hana ugonjwa, wazazi waliamua kujiongeza na kumpeleka kwa mganga wa jadi.
Cha kushangaza kesho yake shangazi ya binti alikutwa kwa mganga akiwa uchi, huku akiweweseka na akili zimemruka, shangazi mtu alikamatwa na kupelekwa kituo cha polisi lakini kwa kuwa serikali haiamini ushirikina aliachiwa huru, lakini hadi leo hii alishakuwa chizi. Binti yeye alipona kabisa.
3. Kisa cha tatu na mwisho ni hiki kilichotokea Liwale shule ya sekondari X nikiwa na walimu wenzangu ambao tulikuwa tunasoma chuo cha SAUT-Mtwara.
Tulipangiwa field katika wilaya ya Liwale ilikuwa mwaka 2009, mwanachuo mwenzetu akiwa zamu siku hiyo alikumbana na mtoto ambaye kwao iliaminika kuwa bibi yake alikuwa mtaalamu wa mambo ya giza.
Mwanafunzi huyo alichelewa kufika shule, mwalimu alipotaka kumuadhibu aligoma, wakasumbuana sana mwisho wa siku akamuadhibu yakaisha, jioni tukiwa uwanjani tunafanya mazoezi yule mwanachuo mwenzangu alianguka na kupoteza fahamu, ikawa jumla hadi kifo.
Kama na wewe umewahi kukutana/kushuhudia live ushirikina share nasi kisa chako watu tupate ilimu.
Mungu ni mwema siku zote.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu utakua umechanganya majina ya kituo kdg sbb majina km yanaendana..Kisa cha kwanza ambacho kinanivutia hadi leo ilikua mwaka 1998, Niko na jamaa yangu, Tunatokea Shule ya Wasichana Kifungilo tunarudi shuleni kwetu Magamba Secondary (now Sebastian Kolowa University)! Usafiri miaka ile usafiri ulikua wa shida sana, tukawa tunasubiri usafiri pale Lukozi, SAA Tisa au kumi hivi jioni. Mvua ikaanza kunyesha, wenyeji wakasema kuwa Mvua haitanyesha kwa kuwa Mzee Fulani yuko shambani kwake anauza mapeasi yake.
Ghafla yule Mzee akawa anapita, aiseee seriously kwa Mara ya kwanza tangu nizaliwe sijawahi kuona MTU hanyeshewi na mvua! Yaani mvua inanyesha lakini yeye hanyeshewi kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
Mwaka 1987 alikuja mtu mmoja kutoka Kasulu kwa lengo la kufanya kibarua cha kulima hapo kwenye familia yetu. Hicho kipindi kulikuwa na misiba sana nyumbani pale. Kulikuwa tayari wadogo zangu 5 wameshafariki kwa interval ya mwaka hadi miaka 2,3. Yule jamaa akawa anakwenda kulala kwa shangazi yangu, shangazi alikuwa jirani yetu sana.
Siku moja yule jamaa akamwambia mzee wetu kuwa ameshafikisha mara kadhaa anakutana na shangazi akitoka kuroga hapo nyumbani kwetu akiwa uchi. Mzee wetu alikasirika sana. Mzee alitoweka kwa kutoroka hadi miezi 2 au 3 hivi. Nakumbuka siku ametoroka tulimaliza kuzika mdogo wangu wa kike. Siku ya kurudi alirudi na mganga wa kike, alitoka sehemu moja inaitwa Kanadi huko Bariadi. Nakumbuka siku ya pili yake yule mganga alisema familia nzima wawepo nyumbani na asitoke mtu ikifikia saa 12 jioni
Mimi nikawa nawaza nini kitatokea. Alichukua yai la kuku (alikuja nalo nadhani) akazunguka nalo kwenye mpaka wa eneo la familia kisha akampa kaka yetu (mtoto wa baba mkubwa) akamwelekeza aende akalitupe lile yao kwenye familia ya shangazi na alifanya vile
Mungu wangu, usiku tu kabla ya saa 7 usiku huo. Pale nyumbani walikamatwa mbweha wengi, wale mbweha wanalia kama binadam (wanalia kama wanawake). Yule mganga alielekeza hakuna mtu kutoka. Kesho yake asubuhi, wale mbweha walikuwa wamekufa na wamevutwa wakawekwa kwenye shimo la choo kilichokuwa hakijajengelewa.
Siku chache baadae shangazi akajitokeza kama mwehu hivi akatembea kitongoji kwa kitongoji akisema yote ambayo huwa anayafanya, washirika wake wote humo mtaani, alisema pia mipango yake yote ambayo anatarajia kuyafanya.
Siku chache pia washirika wote wale nao wakaanza kufanya kama alivofanya mwenzao. Hakika, wale wote walikufa wakiwa wehu na kaburi zao huwa zinaota vichuguu hadi leo licha ya kujengelewa kokoto, huwa zinapasuka na kuota vichuguu vikubwa
Nilishaogopa sana, Nilishaogopa waganga na wachawi tangu hicho kipindi. Nilisha kataa habari zote za waganga maana nao ni wale wale tu.
Hawa watu ni shida wewe,kuna kicheche moja ilitusumbua kwenye familia tangu ina miaka 16 yaani ilifika mahali tulikuwa tunaombea afe tu ili tupumzike ikakumbana na mpemba ikaolewa yaani kama haipo ilivyotulia hata kukiwa na tatizo haiji mpaka mumewe aizingue nje kwenyewe nasikia haichunguliiHaahah,kuna kisa cha mpemba Mafia, alikua ameanika samaki wake baada ya kuwavua, ikafika mda akatoa mkeka akawa anapiga rakaa(Anaswali).Amemaliza kuswali kugeuka hamadi samaki wake wawili hawapo, akauliza kuna ntuu kachukua samaki zangu arudishee kila mtu akakakana akasema mi natoa dakika kumi tuu msiporudisha Walah! atakufa mtuu hapa na si masiharaa... Ebanaeee baaada ya dakika 10 zikaanguka kunguru mbili(hawa ndege Weusi) zimeshakaukaa zamani mdomoni wanamabaki ya samaki....
Sent using Jamii Forums mobile app
Dah ndio na Mimi nagundua sasa hivi, sijui kwanini muda sana nashindwa kutofautisha Mkuzi na Lukozi! Mzuka alishafariki miaka mingi akamuacha yule Mama, alikua na Mabinti wawili sijui wako wapi siku hizi. Walifungua hotel yao jirani na Makazi ya Mzee Mkapa! Nasikia Mzee ....... Usiku mwemaMkuu utakua umechanganya majina ya kituo kdg...
Kituo kitakua either ni mkuzi au kwemakame...
Nimeishi kule kiasi maana mzee alikua meneja misitu pale magamba forest(hope unapajua ni katikati ya msitu, ipo isolated na wanakijiji, japo huduma zote zipo) kabla hajahamishwa..
Lukozi ni Juu ya Magamba km unaenda Mtae huko na kifungiro n km unaenda mlola..
Yote kwa yotee yale maeneo yana mapicha picha sanaaaa...
Huko huko mkuzi kuna mzungu mmoja maarufu sana alikua anaitwa mzuka,
Kisa cha kupewa hili jina ni kwamba alikua na shamba akaambiwa popote utakapoona huu mti usiukate ni makazi ya majini/shetani..
Akapuuza siku akaukata...
Alikula bonge ya banzi kuanzia pale akawa amepita shingo kichwa kimelalia upande mmoja...
Maisha yake yote yaliobaki alikua akitembea na kikapu kilichojaa mawe upande mmoja ili ku balance mwili maana ulikua umelala upande mmoja...
Pia tushawahi pita sehemu usiku miti ikalala yoteee.....
Pia mzee alishawahi salimiwa na vibwengo usiku akitoka magamba coast akipita ule uchocholo wa magamba sec...
Akavitukana sana....
alifika nyumbn hana kiatu kimoja.....
Kuna mapicha mengi sanaa kulee....
Nimepamisss long time sanaaaa..
Hata humu watu wanathibitisha kuwa uchawi upo ingawa wewe unapinga kwa vigezo vyako.Kuthibitisha unakokutaka unataka kukidhi vigezo gani?
Maana naweza kuthibitisha usikubali uthibitisho wangu kwa vigezo vyako.
Nipe vigezo vyako unavyotaka nivitumie kuthibitisha, ili nijue uthibitisho wangu unakidhi vigezo.
Kama mtakimbuka ile mvua ya mawe kahama march 2015 ngoja niwape kisa chake.
Mvua zilikuwa adimu sana basi wananzengo wakamfuata mganga mmoja alokuwa ana tuhma za kuzuia mvua
Basi watu wakamuhoji akakataa tuhuma hizo. Jamaa hawajaelewa wakampiga hadi kumuua.
Wakati anakufa alisema nakuta lkn mtaona.
Waloelewa walianza kuhama walokaza shingo wakakomaa .....
Mvua ilipoanza wakasema tumemuua yule alikuwa anazuia mvua....lkn ikaja kuzidi....na mawe juu. Iliua watu na mifugo na uharibifu mkubwa ulotokea.
Kiranga usi comment hapa
Kabla ya kwenda kote huko, uchawi ni nini?Hata humu watu wanathibitisha kuwa uchawi upo ingawa wewe unapinga kwa vigezo vyako.
Kuthibitisha (uchawi) unakokutaka unataka kukidhi vigezo gani?
Sent using Jamii Forums mobile app
Kabla ya kupewa jibu, orbit ni niniKabla ya kwenda kote huko, uchawi ni nini?