Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,176
- 25,919
Hakuna wakati nime-appreciate uwezo wa kuona mbali wa Julius Nyerere kama wakati huu. Huko nyuma nchi kama USA na Russia waliomba waweke vituo vya kijeshi Tanzania na Nyerere alikataa katakata, sababu mojawapo akitambua kuwa katika sias nchi rafiki leo inaweza kuwa nchi adui kesho. Sasa fikiria kama nchi rafiki leo anaweka kituo kikubwa cha kijeshi nchini kwako na kesho anakuwa nchi adui!
Sasa hilo ndio linaendelea huko Denamark, ambapo uhusiano wa Greenland na Denmak ni karibu sawa na uhusiano wa Tanzania na Zanzibar. Watu wa Greenland ni raia wa Denmark lakini wanajitegemea katika mambo fulani fulani pamoja na kuwa na "raisi" wao na wizara kama 17 ambazo ni za ndani ya Greenland. Kuna kituo kikubwa cha kijeshi cha USA ndani ya Greenland, kiasi kwamba Rais wa USA anaweza kwenda Greenland hata kama Denmark wasipende.
Sasa Trump anaenda mbali, anasema lazima aifanye Greenland kuwa sehemu ya USA, kama ambavyo siku moja anaweza kuamka na kusema nataka Zanzibar iwe sehemu ya USA,kwa sababu ya huu mfumo legevu kati ya Tanzania na Zanzibar.
Nadhani huu mfumo wa uhusiano kati ya Zanzibar na Tanzania unatakiwa ubadilike ili jambo kama hilo isiwe rahisi kutokea. Ni rahisi kwa sasa kwa Trump au kiongozi yeyeote mwenye wazimu na nguvu za kijeshi wa taifa jingine kusema nataka Zanzibar iwe sehemu ya USA au China kwa mfano, kuliko yeye kusema nataka Arusha iwe sehemu ya USA au China au Russia nk.
Sasa hilo ndio linaendelea huko Denamark, ambapo uhusiano wa Greenland na Denmak ni karibu sawa na uhusiano wa Tanzania na Zanzibar. Watu wa Greenland ni raia wa Denmark lakini wanajitegemea katika mambo fulani fulani pamoja na kuwa na "raisi" wao na wizara kama 17 ambazo ni za ndani ya Greenland. Kuna kituo kikubwa cha kijeshi cha USA ndani ya Greenland, kiasi kwamba Rais wa USA anaweza kwenda Greenland hata kama Denmark wasipende.
Sasa Trump anaenda mbali, anasema lazima aifanye Greenland kuwa sehemu ya USA, kama ambavyo siku moja anaweza kuamka na kusema nataka Zanzibar iwe sehemu ya USA,kwa sababu ya huu mfumo legevu kati ya Tanzania na Zanzibar.
Nadhani huu mfumo wa uhusiano kati ya Zanzibar na Tanzania unatakiwa ubadilike ili jambo kama hilo isiwe rahisi kutokea. Ni rahisi kwa sasa kwa Trump au kiongozi yeyeote mwenye wazimu na nguvu za kijeshi wa taifa jingine kusema nataka Zanzibar iwe sehemu ya USA au China kwa mfano, kuliko yeye kusema nataka Arusha iwe sehemu ya USA au China au Russia nk.