Kwa hali ilivyo:
Kuna raia wanamtuhumu Mkuu wetu wa Mkoa kuwa ameiba utambulisho wa mtu mwingine kupitia vyeti.
Sisi wenye Imani na mkuu wetu wa mkoa. tunamuomba, ajitokeze, azivunje tuhuma hizi, aonyeshe vyeti vyake, ili awaonyeshe hawa vizabizabina kuwa yeye ni mtu safi na elimu yake haina chembe ya shaka!
Kitendo cha kukaa kimya bila kujibu tuhuma, ni kuonyesha kuwa tacitly anakubaliana na tuhuma hizo!.
Kitendo cha mke wake kufuta post ya Instagram aliyoipost zamani kabisa akijitambulisha kama mama Daudi inaonyesha kuwa kuna kitu kinafichwa, kwa nini afute?- Kikawaida, kwa nchi za Ulaya/marekani ukiwa na tuhuma za post fulani kwenye mitandao ya jamii halafu ukaifuta, inapelekea kuaminika kwamba unaficha kitu, Tena basi ukiwa raisi ndo kabisaaaa huruhusiwi kufuta kile ulichokwisha posti.
Tumeona kwa mujibu wa taarifa mpya, Makonda ana ndugu wa kuzaliwa naye, lakini wazazi wake wanadai wana mtoto mmoja, Je wanaficha hizi information kwa nini?
Ni dhahiri Makonda hana namna, ni lazima aje clean katika hili suala ili kurudisha imani ya wakazi wa mkoa wa DSM kwake!