da sophy kaja kishari.....au tuseme kaja ki-taarabu, na anaonekana anampa mtu ujumbe. lakini anaenda mbali zaidi na kusema huyo mwanaume amefika kwake, hasikii wala haoni...Hii ni jeuri ya hali ya juu kabisa!!!
Japo hajatwambia kama wamekutana na jamaa akiwa ameoa au bado kuoa, from the look of it ni kwamba, da sophy amekuwa na huyo mwanaume kabla ahajaoa na anaendelea kuwa nae mpaka sasa....nakumbuka alisema "yeye kakimbilia pete na harusi, amevipata, sasa atulie na mimi nipate vingine".
My take:
Now; ni wazi kuwa, hawa wanawake walikuwa wanajuana kabla ya ndoa, mmoja akabana kabali ili aolewe, kidume kwa kuwa hakijali ndoa (hakioni kama ndoa ni kitu cha maaana sana) kikaona isiwe tabu, ngoja nikuoe basi.......pasi kufikiri na kuweka nadhiri za kweli za ndoa, wala kuamua kumuacha yule mwingine. lakini na mwanamke aliye ng'ang'ania kuolewa, hakuwa na dhamiri ya kweli ya kuanza maisha ya ndoa bali kumuonyesha da sophy kuwa mimi ni zaidi na nina haki zaidi yako kwa mwanaume huyu.....(waswahili wanasema, atatembea huko, mwisho atarudi home tu!).
Nimalize kwa kusema, jamaa pamoja na hao wanawake wake wanapotezeana muda tu!! the guy, should consider his options as a man and devise an exit strategy........start all over.