Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi,
Wakati mchakato wa Bunge la Katiba unaendelea, kumezidi kuibuka mijadala mikali, kuhusu serikali 3 zilizopendekezwa na Tume ya Warioba au kushikilia serikali mbili ambayo ndio sera ya chama tawala, Chama cha Mapinduzi, na tayari wachunguzi wa hesabu za uwiano wa kuwianika wamedhibitisha pasi shaka kuwa endapo uamuzi wa idadi ya serikali utapitishwa kwa kura, then serikali mbili ndio zitapita.
Japo Mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba, amewasisitiza wajumbe wa Bunge la Katiba, kuheshimu matakwa ya Wananchi waliopendekeza serikali 3, hivyo kazi ya Bunge la Katiba iwe ni kuboresha tuu na ku rubber stamp matakwa ya Wananchi, lakini sio kuyabadili, kuyapindua au kuyafuta kabisa ili kuilinda hadhi ya Tume yake kuwa imewasikiliza wananchi na kuleta kile wananchi walichotaka, Bunge la Katiba, likipindua, kubadili au kufuta chochote, itakuwa ni kuwadharau wananchi na kuidhalilisha kazi nzuri ya tume yake!
Mwanasheria nguli nchini, Prof. Issa Shivji, amesema Bunge la Katiba ndio kila kitu!, ndio mwanzo mwisho kabla ya kura ya maoni, hivyo kazi ya Tume ilikuwa ni kupendekeza tuu na Bunge hili lina mamlaka kamili, kukubali mapendekezo ya tume, kuboresha, kukataa, kuyafuta na kuuleta kitu kingine chochote na sheria na kanuni za Bunge la Katiba zinaruhusu.
CCM kwa upande wake imeishatoa msimamo wa kushikilia serikali mbili kama ilivyo sera yake, hivyo kuhakikisha tunapata katiba mpya ya sera ya Chama cha Mapinduzi kwa kisingizio cha kuulinda muungano, hivyo kuutumia vizuri huo mwanya wa uwiano wa kuwianika wa waungaji mkono wake ndani ya Bunge la Katiba.
Mimi nashauri hivi, kama ni kweli CCM ina nia ya dhati ya kuulinda muungano, basi iwahamasishe wajumbe wa bunge la katiba, kuunga mkono hoja mpya kabisa ya Nchi Moja, Serikali Moja na Rais Mmoja!.
Najua hoja hii itapata upinzani mkali toka upande wa Zanzibar, lakini kama CCM iliweza kumshikisha adabu kwa kumuadabisha rais fulani wa Zanzibar, CCM ikaweza kuyaongeza yale mambo ya muungano kutoka 11 ya awali hadi sasa zaidi ya 20, bila kuishirikisha Zanzibar, CCM ikaweza kuvifumua vipengele muhimu sana vya makubaliano ya muungano kwa kumuengua rais wa Zanzibar asiwe Makamo wa Rais bila kuishirikisha Zanzibar, hivyo CCM inaweza kabisa kuamua twende kwenye serikali moja!, hata Zanzibar wapige kelele vipi, tukiamua tumeamua, na kukionekana dalili zozote za kutaka kuichafua hali ya hewa ya kisiasa, dawa ni kuwashikisha tuu adabu kama tulivyokwisha wahi kufanya kule nyuma walipotaka kuuchokoa Muungano wetu huu Adhimu uliosababishwa na yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Mwaka 1964.
Hili la serikali moja ndio Muarobaini pekee wa matatizo yote kabisa ya Muungano, na ili kuepuka kumeza Zanzibar, Tunaigeuza Tanzania kuwa ni Federal Union Republic of Tanzania, yenye majimbo mawili la Bara na Zanzibar, haya majimbo yataongozwa na Magavana! Tukiona hii nayo ni ngumu, then tutakuwa hatuna jinsi, Zanzibar igeuzwe tuu kuwa Mkoa mpya wenye wilaya mbili za Pemba na Uguja! Full Stop! Mwisho wa matatizo!
Na huku ndiko kutakuwa kumuunga mkono Baba Wa Taifa Mwalimu Nyerere aliposema.
By Mzee Mwanakijiji
Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.
Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.
Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!
SAY NO TO SERIKALI TATU!
Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
Asante Mkuu Mzee Mwanakijiji, nadhani now it's high time tuunde a pressure group ya serikali moja!. Kama rasimu inapendekeza serikali 3!, CCM imeamua kutupilia mbali maoni ya serikali mbili!, then kama nia ni kuulinda muungano, why not serikali moja?!.
Nchi Moja,
Rais Mmoja,
Serikali Moja!.
Mungu Ibariki Tanzania!.
Paskali
Wakati mchakato wa Bunge la Katiba unaendelea, kumezidi kuibuka mijadala mikali, kuhusu serikali 3 zilizopendekezwa na Tume ya Warioba au kushikilia serikali mbili ambayo ndio sera ya chama tawala, Chama cha Mapinduzi, na tayari wachunguzi wa hesabu za uwiano wa kuwianika wamedhibitisha pasi shaka kuwa endapo uamuzi wa idadi ya serikali utapitishwa kwa kura, then serikali mbili ndio zitapita.
Japo Mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba, amewasisitiza wajumbe wa Bunge la Katiba, kuheshimu matakwa ya Wananchi waliopendekeza serikali 3, hivyo kazi ya Bunge la Katiba iwe ni kuboresha tuu na ku rubber stamp matakwa ya Wananchi, lakini sio kuyabadili, kuyapindua au kuyafuta kabisa ili kuilinda hadhi ya Tume yake kuwa imewasikiliza wananchi na kuleta kile wananchi walichotaka, Bunge la Katiba, likipindua, kubadili au kufuta chochote, itakuwa ni kuwadharau wananchi na kuidhalilisha kazi nzuri ya tume yake!
Mwanasheria nguli nchini, Prof. Issa Shivji, amesema Bunge la Katiba ndio kila kitu!, ndio mwanzo mwisho kabla ya kura ya maoni, hivyo kazi ya Tume ilikuwa ni kupendekeza tuu na Bunge hili lina mamlaka kamili, kukubali mapendekezo ya tume, kuboresha, kukataa, kuyafuta na kuuleta kitu kingine chochote na sheria na kanuni za Bunge la Katiba zinaruhusu.
CCM kwa upande wake imeishatoa msimamo wa kushikilia serikali mbili kama ilivyo sera yake, hivyo kuhakikisha tunapata katiba mpya ya sera ya Chama cha Mapinduzi kwa kisingizio cha kuulinda muungano, hivyo kuutumia vizuri huo mwanya wa uwiano wa kuwianika wa waungaji mkono wake ndani ya Bunge la Katiba.
Mimi nashauri hivi, kama ni kweli CCM ina nia ya dhati ya kuulinda muungano, basi iwahamasishe wajumbe wa bunge la katiba, kuunga mkono hoja mpya kabisa ya Nchi Moja, Serikali Moja na Rais Mmoja!.
Najua hoja hii itapata upinzani mkali toka upande wa Zanzibar, lakini kama CCM iliweza kumshikisha adabu kwa kumuadabisha rais fulani wa Zanzibar, CCM ikaweza kuyaongeza yale mambo ya muungano kutoka 11 ya awali hadi sasa zaidi ya 20, bila kuishirikisha Zanzibar, CCM ikaweza kuvifumua vipengele muhimu sana vya makubaliano ya muungano kwa kumuengua rais wa Zanzibar asiwe Makamo wa Rais bila kuishirikisha Zanzibar, hivyo CCM inaweza kabisa kuamua twende kwenye serikali moja!, hata Zanzibar wapige kelele vipi, tukiamua tumeamua, na kukionekana dalili zozote za kutaka kuichafua hali ya hewa ya kisiasa, dawa ni kuwashikisha tuu adabu kama tulivyokwisha wahi kufanya kule nyuma walipotaka kuuchokoa Muungano wetu huu Adhimu uliosababishwa na yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Mwaka 1964.
Hili la serikali moja ndio Muarobaini pekee wa matatizo yote kabisa ya Muungano, na ili kuepuka kumeza Zanzibar, Tunaigeuza Tanzania kuwa ni Federal Union Republic of Tanzania, yenye majimbo mawili la Bara na Zanzibar, haya majimbo yataongozwa na Magavana! Tukiona hii nayo ni ngumu, then tutakuwa hatuna jinsi, Zanzibar igeuzwe tuu kuwa Mkoa mpya wenye wilaya mbili za Pemba na Uguja! Full Stop! Mwisho wa matatizo!
Na huku ndiko kutakuwa kumuunga mkono Baba Wa Taifa Mwalimu Nyerere aliposema.
Wanabodi, hii nimeikuta humu iliandikwa na Mkuu Mzee Mwanakijiji , miaka 2 iliyopita! Kumbe wakati sisi tunazungumza haya leo, wenzetu walizungumza kitambo!"CHAMA CHA MAPINDUZI kitakapobadili sera yake ya Muungano wa Serikali mbili, sera yake mpya itakuwa sera ya Muungano wa Serikali moja. Chama cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, katu hakiwezi kukubali sera ya serikali tatu, kikijua wazi wazi kwamba matokeo na shabaha ya sera hiyo ni kuiua, na kuizika Tanzania. Chama cha Mapinduzi kikiwa na msimamo huo, na wala kisiuonee haya, Tanzania itadumu." Mwalimu J. K. Nyerere, "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania," Uk. 61.
Tuchukue wosia wa Baba wa Taifa niliounukuu hapo juu kwa manufaa ya nchi yetu na vizazi vijavyo!
Nawasilisha kwa Mjadala zaidi!
Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.
Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.
Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!
SAY NO TO SERIKALI TATU!
Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
Asante Mkuu Mzee Mwanakijiji, nadhani now it's high time tuunde a pressure group ya serikali moja!. Kama rasimu inapendekeza serikali 3!, CCM imeamua kutupilia mbali maoni ya serikali mbili!, then kama nia ni kuulinda muungano, why not serikali moja?!.
Nchi Moja,
Rais Mmoja,
Serikali Moja!.
Mungu Ibariki Tanzania!.
Paskali