MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Hivi inakuingia Akilini kweli unamuacha Beki halisi namba Tatu Bench Mohammed Hussein Tshabalala na unamuanzisha Mtu mwenye uwezo wa Kucheza Beki namba Mbili Israel Patrick Mwenda?
Hivi inakuingia Akilini kweli ndani ya Mechi Tatu unaona kabisa Kiwango cha Beki Shomary Kapombe kinashuka halafu bado unalazimisha Kumpanga wakati unae Beki mpya tena huenda ana uwezo mkubwa kuliko Yeye Israel Patrick Mwenda?
Hivi inakuingia Akilini kweli Kocha mzima unajua kuwa 85% ya Mabeki ulionao Simba SC ni Wazee sasa halafu unaamua Kumtoa kwa Mkopo kwenda Mtibwa Sugar FC Beki mwenye Uwezo mkubwa na ana Kila Kitu Ibrahim Ame?
Hivi kweli inakuingia Akilini kwa Kocha kuamua Kumuingiza Uwanjani Mchezaji ambaye Kiuhalisia ni Beki Mbili Israel Patrick Mwenda akacheze Beki namba Tatu huku hapo hapo katika Bench ukiwa na Mchezaji mwenye hiyo namba na ndiyo anaimudu vyema Gadiel Michael Kamagi Mbaga?
Hivi kweli inaingia Akilini kwa Kocha kuamua Penati apige John Raphael Boko wakati 99.9999% ya Wachezaji wa Simba SC wanasema hata ukimuamsha tu Usingizini Mchezaji Kiraka ndani ya Kikosi Erasto Edward Nyoni anafunga / atafunga?
Hivi kweli inakuingia Akilini yaani Kocha ana Silaha Kali ya Mchezaji Pape Ousmane Sakho ambaye kila aliyemtizama kwa Jicho la Mpira anakubali kuwa Jamaa anajua, msumbufu na mpambanaji hasa na anaanzia tu Bench na hata akiingia anapewa wastani wa dakika 15 au 10 tu?
Mightier Jumapili Usiku nilianzisha Uzi hapa hapa JamiiForums nikisema na Kuahidi kuwa naenda Kuanika Upuuzi wote na Kuwataja Viongozi ambao ningesema Mapungufu yao ila kuna Mwandamizi Mmoja akanifuata PM na Kuniomba nisiharibu.
Na kwa Kumuheshimu kwakuwa namjua vyema pia lakini kwa hii Suluhu ( Goalless Draw ) ya Leo yenye Upuuzi kama siyo Upumbavu mwingi naweza Kuweka Mambo yote hadharani na Mgogoro mkubwa uibuke Klabuni Simba.
Na wengine kama akina Mightier tunaumia kwakuwa hatujaishia tu kuwa Wachambuzi wa Mpira ( hasa Soka la Tanzania ) ila hata huu Mpira wenyewe nao tumeucheza vyema, tukasifika na tunaujua vile vile hata kama hatujafikia Kiwango kile na bahati nzuri hata Wachezaji wa Timu hizi Kubwa nchini ni Washkaji na Wadogo zetu hivyo huwa wanatuambia mambo mengi, makubwa na mazito pia.
Tafadhalini Kocha Gomez atupishe SSC.
Hivi inakuingia Akilini kweli ndani ya Mechi Tatu unaona kabisa Kiwango cha Beki Shomary Kapombe kinashuka halafu bado unalazimisha Kumpanga wakati unae Beki mpya tena huenda ana uwezo mkubwa kuliko Yeye Israel Patrick Mwenda?
Hivi inakuingia Akilini kweli Kocha mzima unajua kuwa 85% ya Mabeki ulionao Simba SC ni Wazee sasa halafu unaamua Kumtoa kwa Mkopo kwenda Mtibwa Sugar FC Beki mwenye Uwezo mkubwa na ana Kila Kitu Ibrahim Ame?
Hivi kweli inakuingia Akilini kwa Kocha kuamua Kumuingiza Uwanjani Mchezaji ambaye Kiuhalisia ni Beki Mbili Israel Patrick Mwenda akacheze Beki namba Tatu huku hapo hapo katika Bench ukiwa na Mchezaji mwenye hiyo namba na ndiyo anaimudu vyema Gadiel Michael Kamagi Mbaga?
Hivi kweli inaingia Akilini kwa Kocha kuamua Penati apige John Raphael Boko wakati 99.9999% ya Wachezaji wa Simba SC wanasema hata ukimuamsha tu Usingizini Mchezaji Kiraka ndani ya Kikosi Erasto Edward Nyoni anafunga / atafunga?
Hivi kweli inakuingia Akilini yaani Kocha ana Silaha Kali ya Mchezaji Pape Ousmane Sakho ambaye kila aliyemtizama kwa Jicho la Mpira anakubali kuwa Jamaa anajua, msumbufu na mpambanaji hasa na anaanzia tu Bench na hata akiingia anapewa wastani wa dakika 15 au 10 tu?
Mightier Jumapili Usiku nilianzisha Uzi hapa hapa JamiiForums nikisema na Kuahidi kuwa naenda Kuanika Upuuzi wote na Kuwataja Viongozi ambao ningesema Mapungufu yao ila kuna Mwandamizi Mmoja akanifuata PM na Kuniomba nisiharibu.
Na kwa Kumuheshimu kwakuwa namjua vyema pia lakini kwa hii Suluhu ( Goalless Draw ) ya Leo yenye Upuuzi kama siyo Upumbavu mwingi naweza Kuweka Mambo yote hadharani na Mgogoro mkubwa uibuke Klabuni Simba.
Na wengine kama akina Mightier tunaumia kwakuwa hatujaishia tu kuwa Wachambuzi wa Mpira ( hasa Soka la Tanzania ) ila hata huu Mpira wenyewe nao tumeucheza vyema, tukasifika na tunaujua vile vile hata kama hatujafikia Kiwango kile na bahati nzuri hata Wachezaji wa Timu hizi Kubwa nchini ni Washkaji na Wadogo zetu hivyo huwa wanatuambia mambo mengi, makubwa na mazito pia.
Tafadhalini Kocha Gomez atupishe SSC.