Kama kipato chako ni chini ya milioni Tano kwa mwezi wewe ni Maskini

Wenye hela hawawezi weka avatar kama aliyoweka yeye.. hizo editing za picha zinapatikana infinix sijui 🤣
Ni maskini mwenzetu, aje tupeleke CV kwa Boss la DP World
Hakuna sehemu mtoa mada kasema yeye ni tajiri au kutaja kipato chake,ila kaandika anachoona yeye ni sawa haijalishi yeye anavyo au hana,shida yetu wabongo wengi ni masikini sana na tunapenda maneno ya faraja,mtu akituchana ukweli tu tunapaniki na lazima tumshambulie
 
Basi nyamaza mkuu, usilie 😘
Hakuna sehemu mtoa mada kasema yeye ni tajiri au kutaja kipato chake,ila kaandika anachoona yeye ni sawa haijalishi yeye anavyo au hana,shida yetu wabongo wengi ni masikini sana na tunapenda maneno ya faraja,mtu akituchana ukweli tu tunapaniki na lazima tumshambulie
 
View attachment 2922301
Takwimu za 2022.

Hiyo mishahara ni midogo mkuu. Hiyo wanalipwa vibarua, wafanyakazi wa kwenye viwanda, call center n.k.
Kwa mwaka ndio inarange usd 23k to 35k
 
Mkuu inawezekana tunatofautiana mitizamo. Ila kwa Tz yetu hii useme kwamba 5M ni masikini? Aisee inabidi wengine turudi shule kujifunza maana halisi ya umasikini.
Hebu jaribu kuangali mishahara ya public sector around the world. Utagundua Tz tunajitahidi.
Tuache utani 5M ni pesa ya kuishi.
 
Kwema Wakuu!

Kuna aina tatu za Maskini.
1. Maskini wa kutupwa (Fukara)
2. Maskini wa kawaida
3. Maskini aliyechangamka.

1. Maskini Fukara
Maskini Fukara hili kundi ni wale Watu ambào kula yao ni mshikeshike, hawana pakuishi, yaani hawa ndio huitwa hohehahe. Hawa kwa asilimia kubwa wamekata tamaa ya maisha. Na ukikutana nao moja kwa moja umaskini ndio utambulisho wao.

2. Maskini wa Kawaida.
Hili ni kundi ambalo wengi tupo hapa.
Hawa wanapata kiasi mahitaji yao ya msingi lakini sio Quality. Yaani atakula ndio chakula lakini sio mlo kamili.
Yaani yeye kila siku maugali na maharage sio shida. Kuvaa nguo za mtumba ni jambo la kawaida. Mpya ni mara mojamoja.

Makazi yao ni vibanda fulani ambavyo vinawastiri na baridi, jua na mvua. Ingawaje wao wenyewe huita nyumba lakini kimsingi sio nyumba.

3. Maskini waliochangamka.
Kundi hili ni lile la wenye vipato ambavyo ni kati ya milioni moja mpaka tano.
Kwa Tanzania kundi hili nalo hujiona limetoboa lakini kimsingi ni kundi maskini tuu kwani vipato vyao haviwezi kukidhi mahitaji ya msingi kwa kiwango kikubwa.

Mfano mtu mwenye kipato cha milioni moja mpaka tano hana uwezo wa kula milo mitatu kamili mwaka mzima pasipo kupasua matairi. Hapohapo hana uwezo wa kuishi kwenye makazi mazuri na kuvaa nguo Standard. Ni lazima kimoja atashindwa. Hapohapo awe anabima nzuri ya afya. Gari nzuri ambayo mafuta kwake sio tatizo, huku anasomesha watoto shule nzuri. Utagundua hicho kipato ni kidogo mno.

Kundi hili linanafasi ya kupambana na kuingia kundi la matajiri daraja la chini ambao kipato chao ni milioni 10 mpaka milioni mia moja.
Ishu inakuja pale ambapo Watanzania wengi tukishapata tumilioni mbili kwa mwezi ndio tunaona tumeshatoboa na tunaanza kubweteka ilhali kimsingi bado tupo tabaka la juu la maskini.

Unapoambiwa nchi yako ni maskini elewa kuwa robo tatu ya wananchi vipato vyao kwa mwezi havitoboi milioni tano.

Ukisikia mtu anakuita Maskini na unajiona una maisha mazuri. Sijui gari, nyumba na unapesa za kubadilisha mboga alafu muda huohuo kipato chako halifiki milioni tano jua anahaki ya kukuita hivyo.

Ingawaje umaskini kwa upande mwingine ni mtazamo. Mtu anaweza kuwa Maskini wa kipato lakini akawa anajiona tajiri(mental illness) alafu yupo mwenye kipato cha milioni 100 alafu anajiona maskini(hana shukrani).

Ijumaa Kareem
ila wewe jamaa una akili fupi sana, unajua maana ya umaskini?
 
Utajiri una definition kubwa na wealth it's Infinity, sijui kama ulishawahi tengeneza hata. 2ml Kwa Mwezi wewe out formal system,

Wakati Niko namaliza chuo wenye mawazo kama Yako walikuwa wengi, Tena wlisema mshahara wa million 3 Kwa Mwezi ni mdogo sana siwezi Fanya kazi ila 99 percentage now wana less than 1,000,000 Gross salary per month na wengine hata kazi wamekosa.
My take; Vijana tuamke tuache kuishi maisha ya kimtandao go and make money you stop talking this non sense,
Kama umeajiliwa tuanze na wewe weka slip attach one slip or kama ni inform sector returns zako hapa,

Nje na hapa ni mawazo ya watoto wanao kaa Kwa shemeji.
Ukisikia mgambo wanaruka na kukanyagana ndo huku sasa,mara wealth is infinity,mara milioni tano ni pesa nyingi ya utajiri? Mzee tukueleweje? Halafu muda huohuo unatuasa vijana tuamke tutafute hela,hela gani sasa kama milioni 3 kwako ni utajiri?
 
Mkuu kumbe yule binti kimoso ndio anamlea jamaa, maana posts zake nyingi za kitoto na zimejaa picha za binti kimoso, kweli usiamini kila kinachoandikwa jf
Hahaaaaa unamfahamu. Hana lolote anatishia watu tu humu JF, tunaomfahamu toka anajinyea na kunya minyoo kule Ugweno Upareni hatusumbui.
 
Back
Top Bottom