aaah shabash! Facebook kuna wahuni kule, jamaa wameweka sana akaunt za viongozi wengi wengi ambazo ni hewa.EL kuwa mtarajiwa hiyo ipo wazi; kule facebook anajiita Edward Lowasa the next president of united republic of Tanzania.
na amewahi kuanzisha mada iliyokuwa ikisema, 'siwezi kuahidi mengi kama ilivyo kwa serikali iliyopo madarakani hivi sasa ila nipe kura yako na hutajutia.'
Hayo ndo maneno yenye busara. Hata Richmond jamaa wamembebesha zigo tu. Kwani hata jk anahusika, kujiuzulu kwake u PM nilichukulia kama jazba na hasira tu.Mi sioni tatizo kama EL atakuwa rais, kwa kuwa kashfa ananazopewa
ni za kisiasa na zina maslahi kwa kundi la kina Sitta mambo ambayo
sisi hayatusaidii. Ufisadi ni mfumo uliopo ndani ya CCM na Sofia Simba
alithibitisha kuwa ukiongelea ufisadi ndani ya CCM hakuna anayesalimika.
Kwa nini EL peke yake? Tuache bias na tuangalie mustakabali wa nchi
hii; hasa Katiba mpya, Tume Huru ya Uchaguzi, Jeshi lisilotumika kisiasa
na mengineyo, kwani bila vitu hivi hata angekuja nani bado hali itakuwa
ileile, na si kumsakama Lowassa tu. Huu ni mtazamo wangu...
Inaelekea Lowassa anawanyima baadhi ya watu usingizi kweli kweli!
Ama kweli EL ana roho ya paka.
Nilikuwa siamini hata kidogo kama EL atapata urais 2015 lakini sasa kwa mbaali naanza kuiivuta picha.
EL for CCM 2015.Niko kikazi huku kanda ya ziwa, jana kulikuwa na kikao kikubwa kwenye hoteli moja jijini Mwanza!
Inasemekana kuwa Mheshimiwa EL, ameshaanza kampeni za uraisi 2015. Amekuwa na kikao kizito sana na baadhi ya makada wa CCM hotelini hapo! Niliowaona na kuwafahamu kuwepo ni pamoja na Hussein Bashe na mwenyekiti wa wazazi hapa Mwanza, Masota. Huyu ndo alikuwa kama organiser, alikuwa akiwapigia simu watu mbali mbali kuja kuhudhuria kikao na mara kwa mara alisikika akisema mtarajiwa yuko hapa. Walithubutu hata kutamka kuwa rais mtarajiwa ana kikao hapa.
Kilichoshangaza ni kuwa, kuna kijana alikuwa amewaletea magazeti, huyu Masota akamtoa baru akimwita mmbea kwamba amempigia simu Riz-One kuwa kuna kikao cha kampeni. Mwanzoni alivaa sare za CCM baadae akabadilisha na akawa anasema kuwa kikao hicho ni cha kujadili mambo ya harambee ya ujenzi wa kanisa la wakatoliki na yeye ni mwenyekiti wa kamati ya ujenzi huo na EL ni mgeni rasmi kwenye ibada ya harambee iliyotarajiwa kufanyika leo. Cha ajabu ni kuwa Bashe anahusika vipi na kikao cha ujenzi wa kanisa? Au ameshabatizwa?
Naambiwa EL alikuwa na kikao cha kampeni kama hicho mjini Shinyanga juzi. Hivi pamoja na maskendo yote hayo EL ameazimia kweli kugombea urais?
Nawasilisha!
Ni kweli, hasa wale wanaousaka urais kwa nguvu zote lakini wanajifanya hawautaki
kwa kuwa wanakwenda kimyakimya huku mioyo yao ikiwa imejaa unafiki mtupu.
Hawakai wakajadili mambo muhimu ya kitaifa bali wao wanang'ang'ana na Lowassa tu.
Mbona hata wao wanaalikwa mpaka kwenye mahafali ya wanafunzi na wanafanya
kampeni zao lakini hakuna anayewafuatilia? Au kunya anye kuku akinya bata kaharisha?...
"Ikulu si mahali pa kupakimbilia.... Mtu huyo mwogopeni kama ukoma" -J K Nyerere.
Inawezekana akawa mtendaji mzuri kama unavyodai, lakini kwanini anang'ang'ania sana, why why why why?
Kwa uchu alionao Kwanini tusimhofie?
"Ikulu si mahali pa kupakimbilia.... Mtu huyo mwogopeni kama ukoma" -J K Nyerere.
Inawezekana akawa mtendaji mzuri kama unavyodai, lakini kwanini anang'ang'ania sana, why why why why?
Kwa uchu alionao Kwanini tusimhofie?
EL namkubali anaweza kutukomboa watz.