zaratustra
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 848
- 225
Niko kikazi huku kanda ya ziwa, jana kulikuwa na kikao kikubwa kwenye hoteli moja jijini Mwanza!
Inasemekana kuwa Mheshimiwa EL, ameshaanza kampeni za uraisi 2015. Amekuwa na kikao kizito sana na baadhi ya makada wa CCM hotelini hapo! Niliowaona na kuwafahamu kuwepo ni pamoja na Hussein Bashe na mwenyekiti wa wazazi hapa Mwanza, Masota. Huyu ndo alikuwa kama organiser, alikuwa akiwapigia simu watu mbali mbali kuja kuhudhuria kikao na mara kwa mara alisikika akisema mtarajiwa yuko hapa. Walithubutu hata kutamka kuwa rais mtarajiwa ana kikao hapa.
Kilichoshangaza ni kuwa, kuna kijana alikuwa amewaletea magazeti, huyu Masota akamtoa baru akimwita mmbea kwamba amempigia simu Riz-One kuwa kuna kikao cha kampeni. Mwanzoni alivaa sare za CCM baadae akabadilisha na akawa anasema kuwa kikao hicho ni cha kujadili mambo ya harambee ya ujenzi wa kanisa la wakatoliki na yeye ni mwenyekiti wa kamati ya ujenzi huo na EL ni mgeni rasmi kwenye ibada ya harambee iliyotarajiwa kufanyika leo. Cha ajabu ni kuwa Bashe anahusika vipi na kikao cha ujenzi wa kanisa? Au ameshabatizwa?
Naambiwa EL alikuwa na kikao cha kampeni kama hicho mjini Shinyanga juzi. Hivi pamoja na maskendo yote hayo EL ameazimia kweli kugombea urais?
Nawasilisha!
Inasemekana kuwa Mheshimiwa EL, ameshaanza kampeni za uraisi 2015. Amekuwa na kikao kizito sana na baadhi ya makada wa CCM hotelini hapo! Niliowaona na kuwafahamu kuwepo ni pamoja na Hussein Bashe na mwenyekiti wa wazazi hapa Mwanza, Masota. Huyu ndo alikuwa kama organiser, alikuwa akiwapigia simu watu mbali mbali kuja kuhudhuria kikao na mara kwa mara alisikika akisema mtarajiwa yuko hapa. Walithubutu hata kutamka kuwa rais mtarajiwa ana kikao hapa.
Kilichoshangaza ni kuwa, kuna kijana alikuwa amewaletea magazeti, huyu Masota akamtoa baru akimwita mmbea kwamba amempigia simu Riz-One kuwa kuna kikao cha kampeni. Mwanzoni alivaa sare za CCM baadae akabadilisha na akawa anasema kuwa kikao hicho ni cha kujadili mambo ya harambee ya ujenzi wa kanisa la wakatoliki na yeye ni mwenyekiti wa kamati ya ujenzi huo na EL ni mgeni rasmi kwenye ibada ya harambee iliyotarajiwa kufanyika leo. Cha ajabu ni kuwa Bashe anahusika vipi na kikao cha ujenzi wa kanisa? Au ameshabatizwa?
Naambiwa EL alikuwa na kikao cha kampeni kama hicho mjini Shinyanga juzi. Hivi pamoja na maskendo yote hayo EL ameazimia kweli kugombea urais?
Nawasilisha!