Kama Dr.Slaa ni 'babu', hawa wetu tuwaitaje?

Kama Dr.Slaa ni 'babu', hawa wetu tuwaitaje?

Muite Kikwete babu!!!!!!
Unajitoa fahamu mno!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kikwete hakuwahi kukataa kuitwa BABU, yeye ana wajukuu ambao wanamuita hivyo!

Ila huyu wa kwenu na umri ule badala atafute mke aoe, yeye kutwa kucha kukimbizana na vibinti vidogo!
 
Slaa ni mzinzi sana..hafai kuigwa na jamii
Msitupe mawe na mko nyumba ya vioo.Kuna gazeti limefungiwa juzi hapa likionyesha taswira kamili ya naniii.
Acheni jama,sipendi maneno haya yavuke mpaka jama.Please.
 
Dr.Slaa alishaandika huku na haimsumbui.Kuitwa babu ni ishara ya Busara na baraka.Wao wanadhani wanamuita hivyo kwa dhihaka kumbe wanatambua busara na baraka alizo nazo

Kwa mfano yule kijana aliyesema wanaounga mkono serikali tatu wanasubiri kufa kesho akimlenga Warioba unadhani kwa kufuru na laana hii itawaacha salama wafikie umri huo?
Leo nilikuwa nimekukumbuka kamanda wangu Saanane! Nimefurahi kukuona uko mtandaoni tena.
 
Busara za kutumikisha vijana kazi chafu ambazo yeye wala mtoto wake hawezi kuzifanya? Unadhani mwanae anaweza kubeba sumu kweli?l
Jifunzeni kujenga hoja mnaelekea kipindi cha u haguzi mkuu. Bado mnaleta vihoja
 
Babu Slaa ni mkubwa mpaka mzee Majuto anampa shikamoo....
 
Ni propaganda mfu. Imemezwa na kutamkwa bila ya utafiti. Dr.Wilbrod Slaa wa CHADEMA amezaliwa tarehe 29/10/1948. Eti anaitwa babu. Huku ni kuishiwa kwa hoja. CCM hatukufika hapo. Tazama baadhi ya waandamizi wa kwetu wa CCM ambao wengine wanatajwa kuwa wagombea Urais na uone Dr.Slaa alivyo kijana:

-Wasira (amezaliwa 1945. Ni miaka mitatu kabla ya Dr Slaa)

-Mangula (mwaka wake wa kuzaliwa hauko wazi lakini ni mkubwamnokwa Dr. Slaa)

- Sitta (amezaliwa tarehe 18/12/1942 miaka zaidi ya mitano kabla ya kuzaliwa kwa Dr. Slaa)

-Pinda (amezaliwa tarehe 12/8/1948 akimzidi miezi miwili Dr. Slaa)

-Kinana (mwaka wake wa kuzaliwa hauko wazi ingawa kuna habari kuwa amelitumikia Jeshi la Wananchi kwa miaka takribani 20 hadi alipong'atuka 1972. Kimahesabu, naye umri umekwenda)

Kuna orodha ndefu ya waandamizi chamani ambao ni wakubwa wa Dr. Slaa wa CHADEMA lakini hawaitwi 'babu'. Ni propaganda za kitoto sana. Niwaase wanachama wenzangu wa CCM na wakereketwa wetu kuachana na jina dhafu hilo kwa Dr.Slaa. Sisi tuna kaka na dada zake wengi tu ndani ya CCM. Nasi tuwaitaje?


Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
Huo ni ujinga wa Nape mkuu sio wana CCM wote. Unajua yule kijana ana tatizo la kujulikana familia yake sasa anadandia undugu kwa watu. Sasa mimi nashangaa anakwenda mbali wakati ndani ya chama chake kuna mababu na mabibi kibao. Mababu zake ndio hao uliowataja na wengine ni kina Kingunge, Lowassa, Kikwete, ... mabibi ni kama akina Makinda, Anna Abdalah, Sophia Simba, Mary Nagu, Rose Mtengeti nk. Kijana ana matatizo sana yule. Anaichafua CCM yetu. Makelele kibao utadhan kakwamwa na tonge kooni.
 
Leo nilikuwa nimekukumbuka kamanda wangu Saanane! Nimefurahi kukuona uko mtandaoni tena.

Rare asante sana sana kamanda.Nimepata nafuu.Soon nitarudi tena kwenye mapambano Rasmi
 
Last edited by a moderator:
- Anyways ina maana Dr. Silaa sasa ana miaka mingapi kama hujali mkuu

Le Mutuz

Ikija thread ya kujadili critical issues huonekani.Masuala ya kisera na kiitikadi haujadili

Vipi mkuu hujatuletea feedback ya kikao chako na top brass ya NBC

Bado tunakusubiri hapa

www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/662736-salute-kwa-wana-jf-nbc-imeomba-na-radhi-na-inataka-kikao-6.html
 
Warioba mbona kijana sana kichwani kuliko akina NAPE, Makonda waliozeeka akili?... Uzee mnaangalia katka muktadha ipi?...
 
Kwiro boy hana uwezo wa kujadili issues... yeye Nyalandu, January, Membe na Jerry Slaa wanapenda sana mambo ya vimodo ... Issue serious zenye maslahi mapana ya nchi hii huwezi kuwasikia hata siku moja...
Ikija thread ya kujadili critical issues huonekani.Masuala ya kisera na kiitikadi haujadili

Vipi mkuu hujatuletea feedback ya kikao chako na top brass ya NBC
 
- Ukitaka umri wangu fungua thread yake hii ni thread mliyoileta wenyewe naomba kujua Dr. Silaa ana miaka mingapi please?

Le Mutuz

Hatuitaji kufungua thread hapa,records zako za marekani zinaonesha una miaka 53,kama kuishi kisheria ingekuwa miaka 60,ungekuwa umebakiza miaka 7 tu udanje.
 
Back
Top Bottom