FairPlayer
JF-Expert Member
- Feb 27, 2006
- 4,145
- 731
Samahani jamani,
Kama huwawezi basi jiunge nao. Ndio mbinu yangu ya "kutoka" hiyo!
Kama huwawezi basi jiunge nao. Ndio mbinu yangu ya "kutoka" hiyo!
Zalendo halisi,
Samahani mkuu, hii ya kusomea Nigeria una uhakika nalo?
Maana mimi nafikiria kuwa fisadi mkuu hapa nchini na jamaa yangu mmoja anasema ukitaka kuwa fisadi either uibe BOT, Richmonduli, Ndege, IPTL, Kiwira etc, au uwe jambazi sugu na kuibia mabenki na kuuwa watu au uwe MCHAWI.
Sasa mimi nataka niwe MCHAWI ili mafisadi wakishaiba wawe wanakuja kwangu kuwafanyia mambo flani flani kisha nawadhulumu hela zote!
Halafu naanzisha miradi ya kuwasaidia wananchi!
Unaonaje hilo? nipe chuo na mahali huko Nigeria. Nitumie kwenye PM ikiwezekana.
hapo ndo mwisho au inaendelea?
Ndio Viongozi wote wa Dini tulionao Tanzania. Hivyo Sisi Wananchi ndio wenye kuwalea watu hawaNimesoma katika mtandao kuwa Kakobe kamkemea Kikwete kuwa ni mpole mno kwa kutokemea nyaraka za Katoliki na waislamu kuwa waziache.
Namshangaa Kakobe kweli ni mnafiki.Mbona hakumkemea Kikwete na serikali yake ilipopeleka mjadala wa kadhi bungeni? Kwa nini hakumuuliza kIngunge kwa nini hakukemea suala la KAdhi kuingia bungeni na mchakato wake kuingizwa serikalini wizara ya mambo ya sheria na katiba? Mnafiki mkubwa.
Nilichogundua ni kuwa anajikomba kwa serikali na kingunge Ikumbukwe kuwa ASkofu hutu alikuwa mwanasiasa mkubwa aliyetelekeza dini na kuwa mpiga debe wa Mrema aliyetoa unabii wa uongo kuwa Mrema angemshinda Mkapa.Huo unabii wake ukawa wa Uongo mkubwa Mkapa akashinda na mwamawe Mrema aliyempigia madogoli ya unabii wa uganga wa kienyeji wa uongo uwa angeshinda uchaguzi wa 1995 akashindwa vibaya na Mkapa.
Serikali wakati ule ilimlaaani ajkajifanya kichwa maji na unabii wake wa uongo.
Kingunge kampongeza kwa Sababu mwaka wa Uchaguzi 1995 mwenyekiti wa vijana wakati ulle NCHIMBI ambaye sasa ni naibu waziri wa Ulinzi aliamua kumkabili Kakobe na kubishana na Kakobe kuwa ni MWONGO na atashangaa mgombea wake Mrema Hatatashinda Kingunge akaingilia kati akamkemea Nchimbi akamwambia Nchimbi acha kubishana na Kakobe.Nchimbi akanyamaza.Sasa Kakobe analipa fadhili kwa Kingunge kwa kumsifia na kujifanya rafiki kwa Kikwete ili serikali imwone kama katubu mnafiki mkubwa.Kachagua kumpongeza Kingunge kwani Kingunge aliamua kumkemea mshabiki Nchimbi aliyekuwa kaamua kumvalia njuga Kakobe.Mashambulizi ya NChimbi yalikuwa makali kiasi kuwa kosa Kingunge kuingilia kati kumyamazisha nchimbi KAKOBE angekiona cha mtema kuni.Hata hivyo Mashambulizi ya Nchimbi yalikuwa makali kuwa pamoja na Kingunge kumnyamazisha Kakobe aliumia akakimbilia mafichoni akijifanya eti yuko katika maombi ya nguvu ya kumuomba huyo mungu wake kama yupo kweli aliyempa unabii wa uongo kuwa Mrema ATASHINDA UCHAGUZI lakini ukweli wa mambo ni kuwa aliingia mafichoni kwa aibu kwa kuwa unabii wake wa uongo kuwa Mrema angeshinda haukutimia.
Alikuwa wapi kuikemea serikali kuwa iachane na suala la kadhi kuwa suala lile ni hatarri kwa usalama wa nchi?alikaa kimya huyu.
NABII uongo aliyetabiri Mrema kushinda na hakushinda eti anaibuka kuwakemea wale waliokemea Suala la Kadhi hivi huyu kama si mnafiki ni nini? Asiye upande wetu kwa suala la kukemea mambo ya Kadhi yu kinyume chetu.MUNGU NA SHETANI UNAOWATAJA KILA SIKU KAMA WAPO NA WAKULAANI MNAFIKI NA MWOGA WEWE KAKOBE.
Kakobe umechelewa ulikuwa wapi suala la kukemea kadhi? Hatuna cha kukuheshimu you are too late ndio maana waumini wengi wamekukimbia unabaki unajikomba kwa wapagani akina KIngunge kwa kuwasifu kwa sifa wasiokuwa nazo.
Mimi ni mpagani na huwa nawalaani sana wakatoliki hata kwenye maandiko yangu nikipata mwanya lakini kwa suala la Kukataa suala la kadhi kulikataa mlikuwa sahihi na mlionyesha ujasiri mkubwa kusema wazi tofauti na Kakobe aliyejifanya hana cha kusema.Kwa suala la kukemea suala la kadhi kuingizwa bungeni na katika serikali wakatoliki nawapa hoyeeee Kakobe nampa Ziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
kuna mtu alimuuliza msimamo wake kuhusu Kikwete kabla ya uchaguzi wa 2005 na baadaye... watu wanakumbuka.. Kama ni unafiki ni ule nilioandika kwenye "Barua kwa wachungaji".. baada ya kondoo kutawanyika kama wasio na mchungaji leo wanasimama na kujifanya wananyosha fimbo ya uongozi!!? Ashindwe na kulegea....
Mtu asiye wa Mungu huongea kiwafurahichasho wanadamu ili apewe ujira wake hapa hapa. I meandikwa, mtawatambua kwa matunda yao, Naam!
Mimi nakubaliana na Kakobe kwa kiasi fulani. Ni kweli tumeshindwa kufanya lolote wakati CCM wanaiba waziwazi. Lakini kuandamana kuhusu Kenya siyo jambo baya maana inawezekana ndiyo ukawa mwanzo wa waTZ kuamka hivyo 2010 wakiibiwa CCM wajue wanategemea nini. Vilevile CCM kutokumtambua Kibaki wanajipalia makaa, kwani 2010 Kibaki atajibu mapigo, unafikiri M7 mjinga mpaka kajitanguliza kumpongeza? Anajua wizi ndiyo deal la viongozi wote Africa wakiongozwa na CCM nambari wani (No. 1)
Mkuu,
Napenda kutokubariana na wewe hapa.
Nadhani Mchungaji yupo right kwa hili,ingawa sikatai nini anaweza kua alifanya na kunena huko nyuma.Kutokana na siasa za kitanzania mabadiliko kama haya ni ya kuyategemea kwa yoyote (mfano Tambwe Hiza wa Cuf aliyeenda CCM).