Kuna ujinga fulani wa utegemezi unaenea sana.
Hakuna namna nzuri ya kuweza kuendelea kama ile ya kutengwa na ndugu zako.
Kutengwa na ndugu ni bahati ya mtende ambayo wajaaliwa wachache tu dunia hii wanaweza kuipata.
Namuonea donge mleta mada kwa kupata bahati hii iliyoje ya kutengwa na ndugu, wengine hatujaipata vilivyo bahati hii.
Sasa ni muda wake wa ku prove kwamba anaweza kufanya mambo bila ya msaada wa ndugu.
Mimi moja ya sababu iliyonifanya niondoke Tanzania ni kukataa habari ya kuendesha baskeli yenye "training wheels" za kuwa karibu na macho ya ndugu yanayoweza kumfanya mtu abweteke, nimejikita huku mbaaaali na ndugu, ni mwendo wa discipline tu, one mistake ten goals. Having said that, nina keep in touch na nyumbani na kusaidia kadiri ninavyoweza. Why not? Kipato cha wiki mbili kinamlipia mtu mwaka mzima wa chuo.
Tukirudi kwa huyu mtoa mada, anatakiwa agangamale aitoe halafu ajue kwamba anaweza bila msaada wa ndugu.
Waswahili walisema "Mtegemea cha ndugu, hufa masikini"
Na pia "Mtaka nyingi nasaba, hupata mwingi msiba".
Kujitegemea ndio mpango mzima.