Kaka anataka kuvunja ndoa kisa mdomo wa mkewe!

Liverpool VPN

JF-Expert Member
Aug 29, 2020
5,795
13,035
Habarini Wana JF..

Ni yuleyule Mr. Liverpool A.K.A YANGA BINGWA.

Sasa story iko hivi..
Juzi nilisafiri kwenda Mbeya (hata navyoandika huu Uzi nipo Tunduma@Songwe) kufatilia bidhaa fulani hivi.

Safari yangu ilianzia Morogoro.
Nilivyopanda basi la NEW FORCE ndani ya basi nikakutana na baba mdogo.

Huyu jamaa mi sinaga story nae kabisaa, mara ya mwisho tulipigaga story 2016 tulipokutana msibani Kijiji kwetu huko.

Hata namba yake sina na nilisikiaga tu story za walimwengu kuwa anaishi Morogoro.

Sasa bana tulipofika Mafinga abiria jirani angu alishuka na baba mdogo akahamia kwangu na kuanza maswali yake yakiwaki na story za maisha.

Maswali sijui, "Nasikia mpaka leo hujaoa", "Una Kazi serikalini lakini hutaki kuoa" na mengine kama hayo.

Aliendelea kunihoji mpaka Kuna muda nikasikia "Ila kweli kwa vijana wa sasa ninaposikia hujaoa huwa sikulaumu"..!!

Nikabaki namshangaa ""Kwanini?""

Mara akafunguka anayopitia mwanae wa kiume.

Mwanae wa kiume (tumuite John) ni "age mate" wangu (32 Yrs).

Wakati mama yangu yupo hai nilishawahi kuishi nae na kusoma Shule moja.
Baada ya mama kufariki aliondokaga na mawasiliano yakaishia hapo.

Mimi na John mawasiliano yalirudi 2017 ila yalikuja kutoweka tena 2018 baada ya kuoa.

Maana baada ya kuoa alianza uduwanzi wa kuniita "Dogo utaoa lini?" "Dogo huna mke, majukumu upate wapi"

Nikaona huyu sasa ni WA kumpotezea.

Sasa bana jana baba ake John tukiwa safari anasema NDOA YA JOHN INAENDA KUVUNJIKA sababu ya MDOMO WA MKEWE.

Baba mdogo anasema "Mke wa John anamdomo Sana Tena usio na staha"

Yaani John anaweza kukosea Chumbani mkewe akamezea halafu akaja "kumchamba" John hadharani.

Mdomo wa mke wa John haujui hapa wapi, Kuna kina nani, wapi natakiwa kumpayukia mume wangu na wapi natakiwa kuwa na staha, yeye ni KUMPAYUKIA TU JOHN.

Kwa Maelezo ya baba mdogo, mke wa John kufoka na kupayuka ni staili yake ya kuongea na mumewe.

Tena John alihojiwa akasema "Mbona wengine hawafokei ila ni Mimi tu mumewe?""

John alivyoona mdomo wa mkewe umezidi na maongezi na maonyo ya mdomo hayabadilishi tabia ya mkewe basi John alianza kutumia force/kipigo.

Leo anampiga mkewe, mara mkewe anakimbilia kwao, halafu akifika kwao ni full kutetewa, kwahiyo John huonekana mkosefu kila wakati.

Baba mdogo anasema kwa jinsi alivyomsoma mkwewe ni "Mwanamke anayependa/taka ku-control mwanaume" na John kagoma kuwa controlled.
Sasa hapo ndio vita inaanza.

Baba anasema John, kaongea weee, kampiga sanaa mikanda mkewe ila HABADILIKI na SASA SHAURI LIPO MAHAKAMANI huko Dar NDOA INATAKA KUVUNJWA.

Mdomo tu umemshinda..!!!

Turudi kwenu:-
Nikiwaambia "MSIOE" Utasikia "Wanaume wenye akili ndio waoe" Sasa cha kujiuliza huyo anayetakiwa kuolewa kwani akili nae sio kigezo chake?

Nyie mabaharia Ma-feminism watawaua.

Yaani unasutwa na mkeo halafu unatoa kipigo, mke anakimbilia kwao na kwao wanakurudi wewe na vichambo..!!!

Baba mdogo anasema John kanusurika mara 3 kulala lock up sababu ya kumpiga mkewe na kidomo chake.
Na mara mbili yeye baba ndio alibembeleza John asilazwe lockup na mkwewe.

Bila yeye baba kuingilia kati John ilikuwa aue huyo mkewe maana ni full kusemwa na maneno.

Mdomo tu UNAACHANISHA NDOA.

ANYWAY:-
Tuendelee kutafuta hela, If you think money can't buy happiness then go and ask the Homeless and Jobless.

Wale wa Songwe tuonane Mpemba ile "underground club" kama unaelekea Mbeya ipo upande wa kulia tule vyomboooo.

Kuoa waachieni Wazee wenu ndio walioa, nyie mnasogeza matatizo na stress tu za maisha.

USIOE
USIOE
USIOE

#YNWA
 
Habarini Wana JF..

Ni yuleyule Mr. Liverpool A.K.A YANGA BINGWA.

Sasa story iko hivi..
Juzi nilisafiri kwenda Mbeya (hata navyoandika huu Uzi nipo Tunduma@Songwe) kufatilia bidhaa fulani hivi.
Wewe kama hutaki kuoa waache wanaotaka kuoa wafanye hvyo usitumie JF kupinga mambo ya ndoa everyday hizi ndizo ishu zako unaboa
 
Kwa imani yangu inasema mwanamme atamuacha mwanamke kwa dhambi ya usaliti tu, mimi mdomo hauwezi kunifanya nimuache mwanamke, masimango, kiburi n.k LAKINI hakifanya uasherati hakuna mjadala wala kuhoji


1. Ulishawahi kukutana na mwanamke mwenye mdomo kweli wewe?
2. Njoo kazini nikuonyeshe PS asiye na staha na mdomo halafu jiulize ""Hivi mumewe ana hali gani kwa huu mdomo huko nyumbani?""

#YNWA
 
Back
Top Bottom