Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,265
- 17,135
Mwendesha mashitaka wa kesi hiyo alikuwa J.C.Summerfied na Mwalimu Nyerere alitetewa na mawakili watatu, D.N.Pritt aliyekuwa wakili kiongozi akisaidiwa na Wakili Mahamoud Rattansey na Wakili K.L.Jhavery.
Walalamikaji walikuwa wakoloni wa Kiingereza, Mkuu wa Wilaya ya Musoma na Geita F.B.Weeks na mwingine Mkuu wa Wilaya ya Songea G.T.Scotts. Ilidaiwa kuwa Mwalimu Nyerere aliwakashifu viongozi hao katika mikutano yake ya hadhara na kwa kuandika makala kwenye kigazeti kiitwacho Sauti ya Tanu.
Akiwa mahakamani mwendesha mashitaka ambaye pia alikuwa mkoloni wa Kiingereza alisema: "Julius Kambarage Nyerere unashitakiwa, kwanza kwa kumkashifu DC Weeks wa Musoma katika makala yako ya ''Sauti ya Tanu'' Namba 58 ya tarehe 27 Mei 1958. Pili, Katika gazeti hilohilo ulimkashifu pia DC Scotts wa Songea.
Mwendesha mashitaka akaendelea: "Tatu, unashitakiwa kwa kuwakashifu kwa pamoja maafisa hao wa serikali. Baada ya kusomewa mashitaka mambo yalikuwa hivi:
Mwendesha mashitaka: Ni kweli au hapana
Mwalimu Nyerere: Hapana.
Kesi iliahirishwa hadi Julai 16, 1958 ambapo siku hiyo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw.J.C.Cole alilazimika kufika mahakamani yeye binafsi. Shitaka la kwanza liliondolewa. Shitaka la pili lilifanyiwa marekebisho.
Katika utetezi wake, Mwalimu Nyerere alikiri kuwa yeye ndiye aliyechapisha gazeti la ''Sauti ya Tanu'' na kwamba maneno yaliyopo kwenye gazeti hilo yanayowahusu wakuu wa wilaya hao aliyaandika akiwa na lengo la kuitaka serikali ya kikoloni itupie macho malalamiko ya watu.
Alisisitiza kuwa chama cha Tanu kilikuwa na wanachama 300,000 na lengo lake lilikuwa ni kupatikana uhuru wa Tanganyika bila kusababisha vurugu.
Hukumu ya kesi hiyo ilitolewa Agosti 13, 1958 na Mwalimu Nyerere alipatikana na hatia ya makosa mawili ya uchochezi kwa kuwaita wakuu wa wilaya, mashetani na maharamia. Hakimu Davies alisema:
"Nimegundua kuwa Nyerere ni mtu mwenye busara nyingi. Ni mtu mwajibikaji katika jamii. Si jambo la kawaida kutoa adhabu ya kifungo kwa makosa kama haya… mimi sitaki kujitenga na desturi hiyo. Namtoza mshitakiwa faini ya shilingi 3,000 au kwenda jela miezi 6. Nampa mshitakiwa muda wa siku mbili kulipa faini hiyo.''
Baada ya hukumu hiyo kutolewa nyimbo na nderemo zilitawala mahakamani hapo, akina mama ambao walikuwa wamezoea kuzingira jengo hilo kufuatilia kesi hiyo kila ilipotajwa, walishangilia kwa msisimko wakiongozwa na Bibi Titi Mohammedi.
Baada ya kupeana mikono na mawakili wake, Nyerere aliingia katika gari kurejea nyumbani kwake Magomeni Mikumi akifuatana na makamu wake wa Tanu, John Rupia na viongozi wengine wa chama.
Walalamikaji walikuwa wakoloni wa Kiingereza, Mkuu wa Wilaya ya Musoma na Geita F.B.Weeks na mwingine Mkuu wa Wilaya ya Songea G.T.Scotts. Ilidaiwa kuwa Mwalimu Nyerere aliwakashifu viongozi hao katika mikutano yake ya hadhara na kwa kuandika makala kwenye kigazeti kiitwacho Sauti ya Tanu.
Akiwa mahakamani mwendesha mashitaka ambaye pia alikuwa mkoloni wa Kiingereza alisema: "Julius Kambarage Nyerere unashitakiwa, kwanza kwa kumkashifu DC Weeks wa Musoma katika makala yako ya ''Sauti ya Tanu'' Namba 58 ya tarehe 27 Mei 1958. Pili, Katika gazeti hilohilo ulimkashifu pia DC Scotts wa Songea.
Mwendesha mashitaka akaendelea: "Tatu, unashitakiwa kwa kuwakashifu kwa pamoja maafisa hao wa serikali. Baada ya kusomewa mashitaka mambo yalikuwa hivi:
Mwendesha mashitaka: Ni kweli au hapana
Mwalimu Nyerere: Hapana.
Kesi iliahirishwa hadi Julai 16, 1958 ambapo siku hiyo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw.J.C.Cole alilazimika kufika mahakamani yeye binafsi. Shitaka la kwanza liliondolewa. Shitaka la pili lilifanyiwa marekebisho.
Katika utetezi wake, Mwalimu Nyerere alikiri kuwa yeye ndiye aliyechapisha gazeti la ''Sauti ya Tanu'' na kwamba maneno yaliyopo kwenye gazeti hilo yanayowahusu wakuu wa wilaya hao aliyaandika akiwa na lengo la kuitaka serikali ya kikoloni itupie macho malalamiko ya watu.
Alisisitiza kuwa chama cha Tanu kilikuwa na wanachama 300,000 na lengo lake lilikuwa ni kupatikana uhuru wa Tanganyika bila kusababisha vurugu.
Hukumu ya kesi hiyo ilitolewa Agosti 13, 1958 na Mwalimu Nyerere alipatikana na hatia ya makosa mawili ya uchochezi kwa kuwaita wakuu wa wilaya, mashetani na maharamia. Hakimu Davies alisema:
"Nimegundua kuwa Nyerere ni mtu mwenye busara nyingi. Ni mtu mwajibikaji katika jamii. Si jambo la kawaida kutoa adhabu ya kifungo kwa makosa kama haya… mimi sitaki kujitenga na desturi hiyo. Namtoza mshitakiwa faini ya shilingi 3,000 au kwenda jela miezi 6. Nampa mshitakiwa muda wa siku mbili kulipa faini hiyo.''
Baada ya hukumu hiyo kutolewa nyimbo na nderemo zilitawala mahakamani hapo, akina mama ambao walikuwa wamezoea kuzingira jengo hilo kufuatilia kesi hiyo kila ilipotajwa, walishangilia kwa msisimko wakiongozwa na Bibi Titi Mohammedi.
Baada ya kupeana mikono na mawakili wake, Nyerere aliingia katika gari kurejea nyumbani kwake Magomeni Mikumi akifuatana na makamu wake wa Tanu, John Rupia na viongozi wengine wa chama.