JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAOFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAAHALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
Toggle navigation
Kituo kikubwa cha ukaguzi wa magari kujengwa katika Halmashauri ya Mji Makambako
Tarehe Iliyowekwa: August 11th, 2022
Na. Lina Sanga
Kituo kikubwa cha ukaguzi wa magari kinatarajiwa kujengwa katika Halmashauri ya Mji Makambako,kitachotumika kufanya ukaguzi wa magari yote yanayoelekea mbeya na Songea.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi,Mhe. Makame Mbalawa alipokuwa akitoa salamu kwa wakazi wa Halmashauri ya Mji Makambako leo,waliofika kumsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Mhe. Mbalawa amesema kuwa eneo la ujenzi wa kituo hicho lenye ukubwa wa hekta 200 limechukuliwa na jumla ya mil. 870 zimelipwa fidia kwa wamiliki wa maeneo hayo na mil. 2.9 Wizara inajipanga kuwalipa wamiliki walio baki.
Ametoa wito kwa wamiliki wa maeneo hayo ambayo yamechukuliwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho,wanaostahili kulipwa fidia kwa mujibu wa sheria watalipwa kwani fedha zao zipo hawatadhulumiwa.
Ameongeza kuwa jumla jumla ya bil. 2.2 zimetolewa kwa ajili ya matengenezo ya barabara za mjini na Serikali itaendelea kuleta fedha hizo kadri inavyowezekana ili Mji wa Makambako uondokane na Vumbi kwa kujenga barabara za lami.
Video
TEHAMA ni Msingi wa Taifa Endelevu, Tuitumie kwa Usahihi na Uwajibikaji . Makambako TC, 2021
Video zaidi
Kurasa za Karibu
Tovuti Mashuhuri
Wasomaji mbalimbali duniani
Idadi ya Wasomaji
free HitCounter
Ramani ya Eneo
Wasiliana nasi
- Makambako Town Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako
Simu ya mezani: 026-2730044
Simu ya Kiganjani: 0785635383
Barua pepe: td@makambakotc.go.tz
Mawasiliano Mengine
Haki miliki Β©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa
Original text
Contribute a better translation