Kahama vs Geita Battle: Majiji Yajayo Kung'arisha Kanda ya Ziwa

Mgambilwa 04

Member
Oct 19, 2023
25
41
images (1).jpeg

Manispaa ya Kahama

Kanda ya Ziwa inajivunia kuwa na Jiji la Mwanza (City Council) tangu 2002 ambalo ni Jiji la pili kutangazwa baada ya Dsm. Katika miaka hiyo ya 2000s, Miji ya Musoma, Bukoba na Shinyanga ilipandishwa hadhi na kuwa Manispaa (Municipal Cluncil). Ilichukua tena miaka ipatayo 20 kwa Mji mwingine wa Kahama kupata hadhi ya Manispaa mwaka 2021.

Na kwa sasa, Miji yenye Mamlaka (Town Council) kamili ni Geita, Tarime, Bariadi na Bunda.

Hata hivyo, ukuaji wa kasi wa Miji ya Kahama na Geita, umesababisha kufunika Manispaa kongwe katika Kanda hiyo kutokana na ukuaji wa pole pole wa Manispaa hizo ambazo ni Bukoba, Musoma na Shinyanga.

Mathalani,
  • Manispaa ya Kahama ina wakazi 453,000 ikishika namba 07 kwa watu wengi nchini.
  • Mji wa Geita una wakazi 361,000 na unashika nafasi ya 09 kwa watu nchini.
  • Mji wa Shinyanga - watu 214,000, Musoma - watu 164,000 na Bukoba - watu 144,000.
Sababu kuu ya ukuaji wa kasi wa Manispaa ya Kahama ni:-
i) Uchimbaji wa dhahabu.
ii) Ipo Barabara Kuu ya kutoka Dar el Salaam kwenda Rwanda, Burundi, Uganda na Mikoa ya Kagera, Geita na Kigoma.
iii) Kuna biashara kubwa ya mazao mathalani mchele, pamba na tumbaku.

Kwa upande wa Geita, ni:-
i) Uchimbaji wa dhahabu
ii) Ni Makao Makuu ya Mkoa
iii) Upo kwenye Barabara inayotoka Mwanza kwenda Kagera, Kigoma, Rwanda, Burundi na Uganda.
iv) Ni tajiri kwa matunda hususani mananasi.
v) Mkoa unaojihusisha na uvuvi.
vi) Ipo umbali mfupi wa km 35 pekee kutoka Mji wa Katoro ambao ni maarufu kwa biashara ya uchuuzi na maduka kwa Kanda ya Ziwa.

Kutokana na mazingira hayo, dalili zinaonyesha kuwa Kahama na Geita itakuja kuwa mojawapo ya miji mikubwa hapa nchini.

Hata hivyo, Kahama iko katika 'strategic position' kwenye Barabara Kuu inayotoka Dar es Salaam kwenda Rwanda, hali inayoipa advantage kubwa dhidi ya Mji wa Geita.

Hata hivyo kwa idadi hiyo kubwa ya watu, ni suala la muda tu kwa Geita kuwa Manispaa.

images (3).jpeg

Mji wa Geita
 
Ni kweli miji hiyo inakua kwa kasi ila miundombinu haina hasa barabara za lami zenye urefu mjini na viunga vya miji hiyo maarufu kwa uchimbaji wa madini ya dhahabu kwa wingi.

Kahama kuna stendi kubwa ya mabasi yaendayo mikoani, ina mabasi mengi mithili ya stendi ya magufuli mbezi jijini dar kuliko ya arusha na moshi.

Hiyo miji ki miundombinu ya barabara na majengo marefu bado inajikongoja kiasi cha kupendeza kuwa na hadhi ya kuwa jiji
 
Ni kweli miji hiyo inakua kwa kasi ila miundombinu haina hasa barabara za lami zenye urefu mjini na viunga vya miji hiyo maarufu kwa uchimbaji wa madini ya dhahabu kwa wingi.

Kahama kuna stendi kubwa ya mabasi yaendayo mikoani, ina mabasi mengi mithili ya stendi ya magufuli mbezi jijini dar kuliko ya arusha na moshi.

Hiyo miji ki miundombinu ya barabara na majengo marefu bado inajikongoja kiasi cha kupendeza kuwa na hadhi ya kuwa jiji
True, kimiundombinu miji hiyo kama ilivyo miji mingine ya Kanda ya Ziwa bado ni duni sana licha ya ukubwa wake.
Kuna siku wataibuka Viongozi watakaotambua changamoto hizo na kuzifanyia kazi kwa ukubwa wake.
 
Mji wa Katoro (kata za katoro, ludete na nyamigota) una watu wengi kuliko manispaa za bukoba na shinyanga.


Mji wa buseresere(kata za buseresere na butengorumasa) una watu karibu na manispaa ya bukoba.
 
Kahama na Geita ni largest slums zijazo...haikui ikifata itifaki zote za modern city au municipality..

Kahama ikikua sana itafanana mbeya tu

Hiv pale kahama, mjini ni wap? No planning at all

Miji ya zamani kama Musoma na Bukoba imepangiliwa na ina mionekano ya kimji so ikijengwa miundombinu kidogo tu basi itakuwa miji mzr sana na ya kisasa ikizingatiwa pia iko karibu na maji

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
View attachment 2816061
Manispaa ya Kahama

Kanda ya Ziwa inajivunia kuwa na Jiji la Mwanza (City Council) tangu 2002 ambalo ni Jiji la pili kutangazwa baada ya Dsm. Katika miaka hiyo ya 2000s, Miji ya Musoma, Bukoba na Shinyanga ilipandishwa hadhi na kuwa Manispaa (Municipal Cluncil). Ilichukua tena miaka ipatayo 20 kwa Mji mwingine wa Kahama kupata hadhi ya Manispaa mwaka 2021.

Na kwa sasa, Miji yenye Mamlaka (Town Council) kamili ni Geita, Tarime, Bariadi na Bunda.

Hata hivyo, ukuaji wa kasi wa Miji ya Kahama na Geita, umesababisha kufunika Manispaa kongwe katika Kanda hiyo kutokana na ukuaji wa pole pole wa Manispaa hizo ambazo ni Bukoba, Musoma na Shinyanga.

Mathalani,
  • Manispaa ya Kahama ina wakazi 453,000 ikishika namba 07 kwa watu wengi nchini.
  • Mji wa Geita una wakazi 361,000 na unashika nafasi ya 09 kwa watu nchini.
  • Mji wa Shinyanga - watu 214,000, Musoma - watu 164,000 na Bukoba - watu 144,000.
Sababu kuu ya ukuaji wa kasi wa Manispaa ya Kahama ni:-
i) Uchimbaji wa dhahabu.
ii) Ipo Barabara Kuu ya kutoka Dar el Salaam kwenda Rwanda, Burundi, Uganda na Mikoa ya Kagera, Geita na Kigoma.
iii) Kuna biashara kubwa ya mazao mathalani mchele, pamba na tumbaku.

Kwa upande wa Geita, ni:-
i) Uchimbaji wa dhahabu
ii) Ni Makao Makuu ya Mkoa
iii) Upo kwenye Barabara inayotoka Mwanza kwenda Kagera, Kigoma, Rwanda, Burundi na Uganda.
iv) Ni tajiri kwa matunda hususani mananasi.
v) Mkoa unaojihusisha na uvuvi.
vi) Ipo umbali mfupi wa km 35 pekee kutoka Mji wa Katoro ambao ni maarufu kwa biashara ya uchuuzi na maduka kwa Kanda ya Ziwa.

Kutokana na mazingira hayo, dalili zinaonyesha kuwa Kahama na Geita itakuja kuwa mojawapo ya miji mikubwa hapa nchini.

Hata hivyo, Kahama iko katika 'strategic position' kwenye Barabara Kuu inayotoka Dar es Salaam kwenda Rwanda, hali inayoipa advantage kubwa dhidi ya Mji wa Geita.

Hata hivyo kwa idadi hiyo kubwa ya watu, ni suala la muda tu kwa Geita kuwa Manispaa.

View attachment 2816060
Mji wa Geita
Vituko tupu.Kuwa Jiji ni zaidi ya kuwa na lundo la maskini mjini.

Kigezo Cha Idadi ya Watu pekee hakifanyi Mji kuwa Jiji achilia mbali Manispaa.
 
True, kimiundombinu miji hiyo kama ilivyo miji mingine ya Kanda ya Ziwa bado ni duni sana licha ya ukubwa wake.
Kuna siku wataibuka Viongozi watakaotambua changamoto hizo na kuzifanyia kazi kwa ukubwa wake.
Changamoto zipi zaidi ya umaskini uliotopea pande hiyo?
 
Mji wa Katoro (kata za katoro, ludete na nyamigota) una watu wengi kuliko manispaa za bukoba na shinyanga.


Mji wa buseresere(kata za buseresere na butengorumasa) una watu karibu na manispaa ya bukoba.
Huu ni uongo ,utakuwa ukweli mpaka hapo ambapo kutakuwa na mipangilio mipya ya kimaeneo ikiwepo hadhi za Mji.

Katoro haipo kwenye kundi lolote la Miji yaani sio Halmashauri ya Mji hivyo unachoongea ni uongo.
 
Mji wa Katoro (kata za katoro, ludete na nyamigota) una watu wengi kuliko manispaa za bukoba na shinyanga.


Mji wa buseresere(kata za buseresere na butengorumasa) una watu karibu na manispaa ya bukoba.
Kwa hiyo ulitaka kumaanisha kuwa mkusanyiko wa waendesha baiskeli unalingana na bukoba au mimi ndo sielewi
 
View attachment 2816061
Manispaa ya Kahama

Kanda ya Ziwa inajivunia kuwa na Jiji la Mwanza (City Council) tangu 2002 ambalo ni Jiji la pili kutangazwa baada ya Dsm. Katika miaka hiyo ya 2000s, Miji ya Musoma, Bukoba na Shinyanga ilipandishwa hadhi na kuwa Manispaa (Municipal Cluncil). Ilichukua tena miaka ipatayo 20 kwa Mji mwingine wa Kahama kupata hadhi ya Manispaa mwaka 2021.

Na kwa sasa, Miji yenye Mamlaka (Town Council) kamili ni Geita, Tarime, Bariadi na Bunda.

Hata hivyo, ukuaji wa kasi wa Miji ya Kahama na Geita, umesababisha kufunika Manispaa kongwe katika Kanda hiyo kutokana na ukuaji wa pole pole wa Manispaa hizo ambazo ni Bukoba, Musoma na Shinyanga.

Mathalani,
  • Manispaa ya Kahama ina wakazi 453,000 ikishika namba 07 kwa watu wengi nchini.
  • Mji wa Geita una wakazi 361,000 na unashika nafasi ya 09 kwa watu nchini.
  • Mji wa Shinyanga - watu 214,000, Musoma - watu 164,000 na Bukoba - watu 144,000.
Sababu kuu ya ukuaji wa kasi wa Manispaa ya Kahama ni:-
i) Uchimbaji wa dhahabu.
ii) Ipo Barabara Kuu ya kutoka Dar el Salaam kwenda Rwanda, Burundi, Uganda na Mikoa ya Kagera, Geita na Kigoma.
iii) Kuna biashara kubwa ya mazao mathalani mchele, pamba na tumbaku.

Kwa upande wa Geita, ni:-
i) Uchimbaji wa dhahabu
ii) Ni Makao Makuu ya Mkoa
iii) Upo kwenye Barabara inayotoka Mwanza kwenda Kagera, Kigoma, Rwanda, Burundi na Uganda.
iv) Ni tajiri kwa matunda hususani mananasi.
v) Mkoa unaojihusisha na uvuvi.
vi) Ipo umbali mfupi wa km 35 pekee kutoka Mji wa Katoro ambao ni maarufu kwa biashara ya uchuuzi na maduka kwa Kanda ya Ziwa.

Kutokana na mazingira hayo, dalili zinaonyesha kuwa Kahama na Geita itakuja kuwa mojawapo ya miji mikubwa hapa nchini.

Hata hivyo, Kahama iko katika 'strategic position' kwenye Barabara Kuu inayotoka Dar es Salaam kwenda Rwanda, hali inayoipa advantage kubwa dhidi ya Mji wa Geita.

Hata hivyo kwa idadi hiyo kubwa ya watu, ni suala la muda tu kwa Geita kuwa Manispaa.

View attachment 2816060
Mji wa Geita
Nakusahihisha Mwanza ilipewa hadhi ya jiji mwaka 2000.
 
kahama sawa, ila geitq pakichovu sana.
Ni kweli bado pa kichovu but ni Mji ambao una future kubwa sana baadaye. Ni Mji umezungukwa na una owe za kuhudumia centre kubwa zinazouzunguka Mji huo ambazo ni Katoro, Sengerema, Nyehunge, Nyarugusu, Bwanga na Lyamgasa.
 
Back
Top Bottom