Kahama VS Njombe/Mafinga

Na huo uwekezaji unao sema ni ule wa uboreshaji miji kumi na nane ambapo kwa njombe wamejenga soko ,stendi taa za barabarani na baadhi ya lami za mitaa kumbuka miji Kama kahama makambako mafinga na tunduma haikuwemo kwenye huo mradi nasaiz imeingizwa na ndo miji ambayo itapewa kipaumbele zaidi kwa mujibu wa waziri ko hiyo lazima mkubali kuzidiwa Kama saiz ipo speed na bado mradi huo haujaanza
 
Na ukumbuke makambako haikuwepo kwenye mradi huo lakini Ina taa za barabarani za kiwango lamiza mitaa za kutosha na wamejenga masoko madogomadogo ya kutosha na ushindani wa kujenga gorofa unaendelea especially angalia songea road kinacho endelea ni mwendo wa shell na gorofa
 
Ni kweli kabisa hayo unayosema na jiografia ya Makambako ina support viwanda kwa sababu ni tambarare na iko junction.

Sasa baba unatakiwa ujue kwamba roho ya Mkoa na Mji wa Njombe ni kilimo anuwai na licha ya kuwa Mazao kuwa na ups and downs Kwenye bei ukweli unabakia pale pale kwamba wakulima wa Mazao wanapata kipato kikubwa kuliko vibarua wa viwandani.

Pili kiwanda kinaweza kuwa 1 kikalipa pesa moja tuu kwa mwaka.ya ushuru lakini Mazao ya kilimo na misitu ni mwaka mzima.Pili kilimo cha Njombe sio sawa na.Sumbawanga kwamba watu wanategemea kudra za Mungu.

Mkoa wa Njombe una watu wenye pesa naaggressive wa biashara na kilimo Chao ni kilimo cha kisasa kwa hiyo quality ya Mazao itaamua bei na kuzuia bei isiporomoke zaidi.

Makambako hadi mje kufikia mapato ya Njombe ni miaka mingi Sana ijayo,Kumbuka Njombe imetoka chini around 2.5 bln(2015) hadi kuwapita Tunduma,Mafinga (2019) na kwa mwaka huu (2020/21) biashara zimefunguka utaona mwenyewe mkuu,7bln zote zinaenda kutumika kwa wananchi wa Njombe TC.

Na uhakika by 2025 Njombe itafikisha mapato ya ndani 10 bln maana ndio kwanza take off ya investments ya Mazao ya Kilimo hasa parachichi,ufugaji wa kisasa na Vannila bado,na kufungua miundombinu kufungua miundombinu ya barabara inayoendelea aisee mambo yatanoga Sana.

Hapa kila mtu ashinde mechi zake mkuu.
 
Kwa sasa tumekidhi vigezo ni taratibu tuu za kiserikali kuitangaza rasmi kwa sababu hakuna kigezo ambacho bado.

Kilichoibeba Kahama ni nguvu ya mapato na idadi ya watu waliyokuwa nayo ambayo,Njombe Tulikuwa na mapato kiduchu kama hayo ya Makambako na idadi ya wakaazipungufu ya 150k lakini kwa sasa tayari tumekidhi vigezo vyote na natarajia kabla ya 2025 tutatangazwa rasmi kuwa Manispaa.Ndani ya miaka 3 ijayo watafanya tathmnini kama kutakuwa na consistency ya mapato ya 5bln consecutively.

Kama.Lindi na Mpanda ni Manispaa kwa nini Njombe isiwe?
 
Sasa idadi ya bajaj 2000 ni sifa?
Mji hauna town trip za daladala za hapo utajivunia kuwa ni mji mkubwa au ni kitongoji kilichochangamka?
 
Hizo hatuiti daladala, tunaziita ni gari za shamba. Daladala zinazozungumzwa ni kama kutoka Makambako mizani kwenda stendi au sokoni au au angalau Mtwango, kiuhalisia Makambako ni kimji kilichochangamka,lakini kina mambo mengi ya kukosa kupewa sifa kuwa urban proper
 
Ni daladala hata ukienda latra ndivo zilivo sajiliwa na ndo rut za daladala
Basi maana halisi ya daladala utakua huijui. Kwa mfano, kutoka Kihonda kwenda Msamvu ni daladala, kutoka Msamvu kwenda mjini kati ni daladala. Ila kutoka Morogoro kwenda Bwawani au Bigwa au Kisaki au Dumila au hata Mikese, inaweza kuonekana ni daladala kwa maana hiyo ya LATRA lakini siyo town trip, hivyo kwa maisha ya mjini, siyo daladala
 
Uwe mkweli, Makambako haiwez kuizidi Njombe never. Takwimu za Tamisemi zimeonesha kwa miaka yote mumegalagazwa. Ni kimji kinachojitahidi as long siyo makao makuu ya mkoa, hivyo sahau kuizidi Njombe TC, ukweli lazima usemwe.
 
Sasa idadi ya bajaj 2000 ni sifa?
Mji hauna town trip za daladala za hapo utajivunia kuwa ni mji mkubwa au ni kitongoji kilichochangamka?
Yan we ndo umevurugwa kabisa miji mingi saiz bajaji ndo zimeshika chati ko amka usingizini ndoo maana unaona migomo ya daladala inazidi na jiografia ya mji wa makambako bajaji zimeruhusiwa kuingia kila Kona tofaut na njombe zinaanzia masasi zinaishia hagafilo na zinanyooka main road kitu ambacho kwa makambako road za mitaa ni za kutosha na TARURA wanaendelea kuweka lami
 
Uwe mkweli, Makambako haiwez kuizidi Njombe never. Takwimu za Tamisemi zimeonesha kwa miaka yote mumegalagazwa. Ni kimji kinachojitahidi as long siyo makao makuu ya mkoa, hivyo sahau kuizidi Njombe TC, ukweli lazima usemwe.
Huo ni ukweli wa mawazo yko Sio uhalisia wa maeneo husika yalivyo kwa sasa
 
Sasa idadi ya bajaj 2000 ni sifa?
Mji hauna town trip za daladala za hapo utajivunia kuwa ni mji mkubwa au ni kitongoji kilichochangamka?
Kila siku nawaambia Makambako ni kijiji cha wachuuzi tuu hamna kitu hapo.Mabajaji yanavyoleta uchafu na usumbufu mjini ndio mtu eti anajisifia.

Makambako fikeni level ya Tunduma kwanza ndio uje kushindana na Njombe TC
 
Uwe mkweli, Makambako haiwez kuizidi Njombe never. Takwimu za Tamisemi zimeonesha kwa miaka yote mumegalagazwa. Ni kimji kinachojitahidi as long siyo makao makuu ya mkoa, hivyo sahau kuizidi Njombe TC, ukweli lazima usemwe.
Labda inaizidi kwa idadi ya watu napo sina hakika tutasubilia sensa lakini kwa vigezo vingine hicho kijiji hakina kitu si huduma za jamii wala miundombinu bora,si uchumi wala kilimo
 
Tuwekee picha na vigezo ulivyotumia kuchagua na kupambanisha miji hii.
Wakati naanzisha mada Kahama ilikuwa TC kama Njombe lakini kwa sasa Kahama ni MC ,ulinganisho hautokuwa sawa kwa sababu Mji unapopanda hadhi kuna previlages unazipata kulingana na hadhi yake.mf Ukiwa MC kila mwaka Unapata bajeti ya kujenga angalau 1km ya lami.

Japo kwenye vigezo vya quality of life Njombe iko vizuri zaidi kuliko Kahama.
 
Weka picha waone wenyewe
 
Bata linaliwa Kahama weweeee, Media tour kubwa nchini (Wasafi/ Clouds) Baada ya Dar/ Mwz / Arusha inakuja Manispaa mpyaa
 
Bata linaliwa Kahama weweeee, Media tour kubwa nchini (Wasafi/ Clouds) Baada ya Dar/ Mwz / Arusha inakuja Manispaa mpyaa
Kwa sababu kuna washamba huko,,usitegemee kuweka tamasha kwa watu wenye kipato cha Kati ,itakumala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…