Kahama VS Njombe/Mafinga

Hahahahaha,kwamba kama hakuna nini? Mi nimeongea kiushabiki kwa nachokijua, wachambuzi wazuri wenye takwimu watasaidia hapa kueleza vigezo vya kuipaisha.
Mkoa wa kuigopa kwenye Uchumi huko Kanda ya Ziwa ni Geita ndio inakuja Kwa kasi na imeingia top 10 ya Mikoa yenye GDP kubwa,hakuna Cha Kahama na Shinyanga yake Wala nini.
 
Hawa jamaa hawatembei ndo shida mfano makambako to njombe km 60 road full makazi na umetenganisha msitu wa tanwat tu miji ina kutana pia Kuna makambako ilembula km 30 na makambako igwachanya km 45 via mtwango mfano hi ni road ya makambako to njombe full daladala πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡ hii NI makambako to ilembula full makazi na daladala za kutosha
 


Wewe unaijua Kahama lakini πŸ€”?
Ukiwa unatoka mkoa wa Geita kwenda Kahama,ukivuka hifadhi ya Mkweni kuanzia wendele hadi Kahama ni makazi hadi kagongwa 41km hapo hiyo ni main road (East to West) hapo ni makazi tu
Kutoka Nyandekwa hadi Kahama mjini ni 14km , Kahama mjini hadi Igung'hwa ni 11km hiyo ni kusini hadi kaskazini mwa mji ( hapo ni 25km+)

Kahama ime-extend pande zote kwa kilometers za kutosha
Unazani kuingia top ten ya Miji mikubwa Tanzania ni swala la kitoto?πŸ–•
 
Narudia Tena muwe mnatembea ndo utajua miji mingi inakua unakuja na vi km 14 sijui 41 wakati wenzenu tayar wana zaidi ya km 50 zinajengeka tu kahama ongea idadiya watu tutakuelewa ila si kwa ujenz
 
Sawa Kahama na Lake zone Kwa ujumla Kuna watu wengi lakini je Kuna maendeleo mengi?

Je Kuna ubora mzuri wa Maisha?

Jibu ni hapana.Mkoa unaokuja Kwa kasi ni Geita na natamani kujua ukiacha Dhahabu Kuna nini tena?

On top of that Kuna Tarime nasikia ina Hali nzuri ya hewa kama Mikoa yetu ya Highlands.

Kahama siwezi ishi huko ni gulioni ,kwanza imeshapungua umaarufu wake hakuna pesa sawa na Morogoro Mjini tuu.

Mwisho Nimekukataza kwamba achana na hoja ya Linier settlement pattern Haina maana Kwa sababu Kila sehemu Nchi hii kukopa hivyo.Mfano Kwa Arusha kutoka Usariver Hadi Kisongo,majani ya Chai au kule Kwa Geodovie NJ zaidi ya km 60 kote Kuna makazi je Arusha Ina watu wengi kuliko Dodoma City?
 
Aliyekudanganya kwamba saivi Kahama hakuna hela ni nani πŸ€”?
Kahama inalishwa na migodi ya dhahabu ya Mwime na Mwakitolyo, na kakola, kilimo cha mpunga, na ni mji wa kibiashara, pia kuna viwanda vingi sana ukiacha vinavyojishughulisha na dhahabu,
Mpaka sasa ukiacha Mwanza kwa lake zone hakuna mji wa kuishinda Kahama kwa upande wa pesa πŸ˜„πŸ€—

Kwa upande wa Maghorofa sensa ya majengo 2022, Njombe ilikuwa inaizidi Kahama kwa idadi ya ghorofa 8 tu (Njombe 139, Kahama 131). Sasa unazani hii data ni valid mpaka sasa, kumbuka miaka ya 2022 kurudi nyuma ujenzi wa maghorofa Kahama haukua wa maana,
Hata huko nyanda za juu kusini data zinaonyesha Mbeya inaizidi Iringa mjini kwa idadi kubwa sana ya Maghorofa almost nusu nzima. Lakini sasa twende kwenye CBD Mbeya inakuwa kituko
 
Narudia Tena muwe mnatembea ndo utajua miji mingi inakua unakuja na vi km 14 sijui 41 wakati wenzenu tayar wana zaidi ya km 50 zinajengeka tu kahama ongea idadiya watu tutakuelewa ila si kwa ujenz
Unalazimisha watu kutembea πŸ€”wewe umetembea?πŸ˜‚πŸ˜‚
Ungekuwa umetembea na hizi data ungezielewa haraka sana, Kahama ni Mji mkubwa mno
 
Njombe inakuja kwa kasi hatari nilikuwepo kule 2015 nikicheki picha za sasa tofauti kubwa inaonekana haswaaa!
 
Ukiongelea mkoa kwa maendeleo mkoa wa Geita unauzidi mkoa wa shinyanga hilo halina ubishi, kwa sababu kwa upande wa Mkoa wa shinyanga sehemu zenye maendeleo ya maana ni wilaya tatu tu Shinyanga Mc, Kahama Mc at least Msalala DC nayo kwa sababu iko na migodi na ardhi nzuri ya kilimo,

tofauti na Geita ambayo kati ya wilaya zake 6 ni wilaya moja ndio iko nyuma kidogo ambayo ni wilaya ya Nyang'wale, hizi wilaya zingine ( mbogwe,bukombe,Chato, Geita DC na Geita Mc) zote zimepiga hatua nzuri kimaendeleo kutokana na uwepo wa migodi ya dhahabu na fursa zingine
 
Sasa wewe nikiangalia Mapato ya ndani miaka na miak Kahama Huwa haivuki bln 13,Sasa Kuna hela gani hapo wakati Geita MC ni bln 19?
 
Shinyanga ina kaupendeleo tu kisa iko barabara kuu, ila kwa speed ya sasa ya Kahama inapitwa mengi.
.
Njombe haipafikii Kahama japo inawekewa kauzibe sana.
Njombe haipafikii Kahama Kwa lipi? Watu wengi au?

Njombe ni Makao Makuu ya Mkoa lazima iwe vizuri kuliko huko vichochoroni.
 
Kwani Kahama na Katolo ipi kubwa? Teh teh teh teh teh. Japo Njombe ina wanawake watam kinoma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…