Watakuelewa basiiii!!! Geita sijakaa sana,itakuwa inaizidi Kahama ukubwa tu. Lakini pia,wasisahau. Miaka kama 10 nyuma,watu kujenga Kahama ilikuwa kama kujilipua tu. Ujenzi ulikuwa wa mashaka sana,maana watu waliambiwaga hawaruhusiwi kujenga. Waliporuhusiwa, sasa hivi nadhani kutoka Kahama senta,kuna sehemu unaweza tembea zaidi ya km 20 ukiwa mjini kati,ukiachana na ile unakuta kuna uwazi mkubwa. Halafu,kitu watu wanasahau. Kahama si mji uliotegemea migodi. Kahama ni mji ambao watu wa Uganda, Rwanda,Congo na Burundi huijia mali. Kwenye swala la mazao, asikwambie mtu. Kahama, ipo main Road kuelekea Uganda, Rwanda,Burundi, DRC. Na hapo pamekuwa kama kituo kikubwa kwa waendesha magari makubwa. Mchanganyiko wa hivyo vitu,hupanua mji zaidi. Huko kwingine sijui