Kwanini ndizi mshare hazipatikani Kanda ya Ziwa?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,695
6,398
Mwanza, Shinyanga, Kahama, Geita, Kagera, na Kigoma! Kote huko sijawahi kukutana na ndizi mshare. Ndizi zinazopikwa maeneo tajwa ni ndizi ambazo kwa Arusha na Kilimanjaro, ukikuta mtu kazipika, ujue ni amekosa kabisa cha kupika. Si matumizi yake.

Nilikula ndizi kwa mara ya kwanza jijini Mwanza mwaka 2010. Nilishangaa nilipokuta ni ndizi ambazo kwa Arusha na Kilimanjaro zinatumika kwa kupikia mtori au kuvundikwa kwa ajili ya kutengenezea pombe. Nilikula kwa kuwa sikuwa na namna, isitoshe, nilikuwa ugenini na ziliandaliwa kwa ajili yangu.

Tokea nikiwa mdogo, nilikuwa nikijua kuwa ndizi zinazotumika kupikia "ndizi" ni NDIZI MSHARE, KIMALINDI, n.k., lakini si ndizi ng'ombe.

Ni kwa nini hizo ndizi hazipatikani Kanda ya Ziwa?
 
Tembea uone.

Mimi mpaka leo nashangaa hao wa rugaruga wana kula je hizo ndizi ngumu kama miogo, mwanzoni ni lidhani na kwa ajili ya walevi kukatia hungerover zao za pombe, mpaka nilivo ona mama mjamzito naye anazila ndo ni kajifunza kwamba.

Hujafa hujaumbika
 
Zipo lakini huku hazilimwi maana zinahitaji mazingira ya baridi ili kustawi vizuri.

Kwaio kuna wachache hua wanazileta sema bei yake inakua juu kidogo hivyo wanaoweza ku afford ni wachache.
Another thing ni kua, most people ambao ni natives wa lake zone, ni heavy feeders, so quantity matters more than quality, i think unanielewa.

Ni kama zile ndizi sukari original, unakuta bei yake kwa ndizi moja ni almost sawa na hizi ndizi kubwa, so most people opt for hizo ndizi kubwa kama njoge n.k, but few people who like ndizi sukari hawawazi kulipa that ammount.
 
Nimezaliwa kanda ya ziwa,, naishi kanda ya ziwa na huenda nitafia kanda ya ziwa ama kuzikwa ziwani kabisa,, ngoja niseme ukweli wangu ndizi kama ndizi ni chakula rasmi kwa watu wa Kagera tu, huku Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Kahama, Musoma ni kitafunwa cha asubuhi kwa chai ama supu, huwa nawashangaa sana jamaa zangu wa kichaga kazini eti wanashindia ndizi,,
 
Uchagani haswa kwa warombo kila ndizi kule ina matumizi yake kwenye kupika. Matoke, mlali ,mshare ,kinairobi, nyoro, kitarasa ni favorite kwa mlo wa kawaida au machalari.

Halafu kunayo inaitwa mkonosi hii ni special kwa mtori/kiburu/kibulu na pia kuchoma au ku fry zikiwa mbivu na pia kutengeneza mbege.

Halafu kuna wanaziita kimulia na zenyewe ni suitable kwa mtori. Pia kuna ndizi mtotoo ambazo nadhani ni ng'ombe hizi ni best katika kutengeneza mbege . Doh nimepakumbuka huko.
 
Tembea uone...... mimi mpaka leo nashangaa hao wa rugaruga wana kula je hizo ndizi ngumu kama miogo, mwanzoni ni lidhani na kwa ajili ya walevi kukatia hungerover zao za pombe, mpaka nilivo ona mama mjamzito naye anazila ndo ni kajifunza kwamba........ hujafa hujaumbika
hizo kule zina hadhi yake
 
Usiwe mbishi, ni mshale sio mshare!.
Mkuu, sina tatizo la R na L, ujue!

🏹 Huo ni Mshale kama siyo mfano wa mshale

Na hapo chini ni ndizi MSHARE.

Ukienda kule yanakolimwa kwa wingi, ukisema ndizi mshale, watakuelewa kuwa unamaanisha NDIZI MSHARE, lakini watajua wewe ni wa kutoka Kanda fulani ndiyo maana unashindwa kutamka kwa ufasaha. Hata hivyo hawatakucheka. Ni wastaarabu!

Kwa hiyo:
NDIZI MSHARE ✅👏👏👏

NDIZI MSHALE ❎😀😀😀
 

Attachments

  • Mshale.jpeg
    Mshale.jpeg
    15.1 KB · Views: 2
mshare ni adimu kote nchini
Hiyo inaweza ikawa ni fursa nyingine iliyojificha!

Miaka ya nyuma, hasa kwa Arusha na Kilimanjaro, ilikuwa ni nadra sana ndizi kutokujumuishwa kwenye MLO wa sherehe. Wazee wengi chakula chao pendwa ni ndizi nyama. Ukimpa pilau au wali mnaweza "kugombana!"
 
Mkuu, sina tatizo la R na L, ujue!

🏹 Huo ni Mshale kama siyo mfano wa mshale

Na hapo chini ni ndizi MSHARE.

Ukienda kule yanakolimwa kwa wingi, ukisema ndizi mshale, watakuelewa kuwa unamaanisha NDIZI MSHARE, lakini watajua wewe ni wa kutoka Kanda fulani ndiyo maana unashindwa kutamka kwa ufasaha. Hata hivyo hawatakucheka. Ni wastaarabu!

Kwa hiyo:
NDIZI MSHARE ✅👏👏👏

NDIZI MSHALE ❎😀😀😀
Kwa hiyo hata baraza la kiswahili tanzania (BAKITA) huliamini
 
Kwa hiyo hata baraza la kiswahili tanzania (BAKITA) huliamini
Na wenyewe wanaiita NDIZI MASHALE?

Mkuu, kama unao ushahidi utuwekee hapa. Isije ikawa mababu zetu ndiyo waliokosea katika matamshi.

Nikikuta kuna utofauti wa matamshi kati ya mababu zetu na BAKITA, basi, nitafanya utafiti wa kunisaidia kuamua wa kuwaamini kati ya BAKITA au MABABU zetu.
 
Back
Top Bottom