JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Ramadhan Kabwili amefunguka kuwa klabu yake ya Yanga iliamua kumpa likizo ya muda mrefu huku akiendelea kulipwa na Yanga kama kawaida
Anasema alipewa likizo ili akili yake itulie na atafute nafasi ya kuonana na mwanasaikolojia kutokana na kile ambacho kilitokea mitandaoni kumuhusu yeye.
Kabwili amekuwa nje kwa muda mrefu tangu mwaka jana, licha ya kuonyesha anaweza kuwa kipa mzuri siku zijazo wakati akichipukia klabuni hapo, ameshindwa kuonyesha uwezo mzuri huku tuhuma za kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja zilitawala.
“Nilikuwa napitia wakati mgumu lakini sasa hivi niko sawa na nimeanza mazoezi, namshukuru Mungu kwa maendeleo mazuri.
“Sina mtu wa kumlaumu, hata kilichotokea mimi mwenyewe sijakielewa, nilipagawa kiakili, ilifikia hatua wakawa wananitenga.
“Sasa hivi kidogo nina maendeleo mazuri na mwisho wa msimu huu mwezi wa saba mkataba wangu wa Yanga utaisha kisha nitajua mwelekeo wangu.
“Familia yangu ilikuwa katika wakati mgumu lakini baada ya yote tulikaa chini tukazungumza na kuna mwelekeo mzuri.
“Kilichotokea kiliniathiri kama mchezaji, hata malengo yangu kama kijana hayakutimia. Suala bado lipo Polisi siwezi kulizungumza kwa undani.
“Timu yoyote ikinihitaji mkataba wangu utakapomalizika tukiafikiana nitakuwa tayari kufanya kazi kwa moyo wote kwa kuwa soka ni kazi yangu,” anasema Kabwili.
Chanzo: TV3 TANZANIA
Anasema alipewa likizo ili akili yake itulie na atafute nafasi ya kuonana na mwanasaikolojia kutokana na kile ambacho kilitokea mitandaoni kumuhusu yeye.
Kabwili amekuwa nje kwa muda mrefu tangu mwaka jana, licha ya kuonyesha anaweza kuwa kipa mzuri siku zijazo wakati akichipukia klabuni hapo, ameshindwa kuonyesha uwezo mzuri huku tuhuma za kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja zilitawala.
“Nilikuwa napitia wakati mgumu lakini sasa hivi niko sawa na nimeanza mazoezi, namshukuru Mungu kwa maendeleo mazuri.
“Sina mtu wa kumlaumu, hata kilichotokea mimi mwenyewe sijakielewa, nilipagawa kiakili, ilifikia hatua wakawa wananitenga.
“Sasa hivi kidogo nina maendeleo mazuri na mwisho wa msimu huu mwezi wa saba mkataba wangu wa Yanga utaisha kisha nitajua mwelekeo wangu.
“Familia yangu ilikuwa katika wakati mgumu lakini baada ya yote tulikaa chini tukazungumza na kuna mwelekeo mzuri.
“Kilichotokea kiliniathiri kama mchezaji, hata malengo yangu kama kijana hayakutimia. Suala bado lipo Polisi siwezi kulizungumza kwa undani.
“Timu yoyote ikinihitaji mkataba wangu utakapomalizika tukiafikiana nitakuwa tayari kufanya kazi kwa moyo wote kwa kuwa soka ni kazi yangu,” anasema Kabwili.
Chanzo: TV3 TANZANIA