The Boss
JF-Expert Member
- Aug 18, 2009
- 49,111
- 115,905
Sisi wengine tulikuwepo wakati Rais Mkapa (1995-2005)anatukanwa kila siku kuwa "anauza nchi Kwa makaburu".....ilifikia wakati hadi nyimbo zilitungwa zikimuimba naukumbuka wimbo mmoja .."Kama sio juhudi zako Nyerere, Mkapa angeuza nini"???..Mkapa alikuwa anatukanwa kisa ni kuleta wawekezaji wa kampuni zisizo zaidi tano kutoka Afrika Kusini..
Walikuja kuwekeza
1.TBL
2.. NBC
Zingine nimezisahau....Leo...
Uwekezaji wa NBC ulipelekea Serikali kuanzisha NMB ambayo nayo waliletwa Waholanzi kununua hisa zisizozidi asilimia 5..waka provide management baadae waholanzi wale wakashangaa jinsi soko lilivyo kubwa wakaomba kununua hisa zaidi now nasikia ni asilimia 25.
Mabadiliko ya sekta nzima ya Benki aliyoyasimamia Rais Mkapa kipindi kile Leo yamepelekea tuwe na sector ya bank kubwa inayofanya kazi Kwa ufanisi.
NMB Leo ni kubwa kuliko Zanzibar GDP..na bank zote 3 kubwa Tanzania.. NMB, NBC na Crdb ni kubwa kuliko Uchumi wa Burundi...
Haya yote yasingewekana kama Rais Mkapa angeogopa "kuitwa fisadi anaeuza nchi Kwa Makaburu"...kipindi kile usingeweza kumuelewa Mkapa ...since watu waliokuwa wanaompinga walikuwa Wana influence ya kutosha ..tukianzia na Mwl Nyerere.....Na Magazeti ya Jenerali Ulimwengu yaliyokuwa Yana influence kubwa Sana Kwa jamii ya wasomi na wakosoaji wakubwa. ungeweza fikiri nchi inauzwa kweli ukifatilia mijadala...
Leo hizo banks zote 3.. NMB na Crdb zinamilkiwa na watanzania asilimia 70 NBC pia Serikali bado ina hisa za kutosha na zote hizo serikali inapokea gawio la kutosha...wale waliokuwa wanasema Mkapa anauza nchi Kwa makaburu wamenyamaza kiimya na sasa wamehamia kwenye "Samia anauza nchi Kwa waarabu" as if nothing happened...wala hawajawi jiuliza walichokuwa wanapinga kipindi kile na Hali ikoje leo? Walikuwa sahihi??
Kama hawakuwa sahihi kwanini wasiombe hata radhi in public hapo hata waliokuwa washauri wa Mkapa ambao bado wako hai wafarijike??...kama Mkapa aliuza nchi Kwa makaburu, hii nchi wanayosema anauza Samia ni ipi tena?
Itoshe kusema TBL ilienda kuwa kampuni inayolipa Kodi kubwa kuliko kampuni zote Tanzania Kwa miaka mingi Sana kama sio mpaka Leo ninavyoandika hapa....lakini shukran pekee aliyoambulia Rais Mkapa ni kuitwa "fisadi anaeuza nchi Kwa makaburu"...
Na wale watukanaji wakubwa Hadi Leo hawajawi kusema "hatukuwa sahihi" tulikosea ...Sana Sana wamevamia basi jipya "la Samia anauza nchi Kwa waarabu" Kwa nguvu mpyaa kabisa ...wazungu wanasema "ignorance is bliss"..
Mtu mjinga ana faida ya kutojijua ujinga wake...anaweza ita hata watu werevu wajinga hadharani bila woga...'ignorance is bliss ".....ungemueleza nini Mtanzania wa kawaida kuwa Mwalimu Nyerere hayuko sahihi ..wakati CEO wa Crdb wakati ule anaenda Hadi Butiama kumuomba Nyerere anunue hata hisa kidogo za Crdb kama kushawishi jamii iamke na Ku embrace"mabadiliko ya uchumi "na Nyerere ananjibu waziwazi mbele ya Tv kuwa hakuna cha mabadiliko wala nini ..ni ubepari na wizi tu kubinafsisha mabenki"...
Kwa watanzania Wengi Nyerere ni close to God ... hawezi kuwa hayuko sahihi..huwa najiuliza kama kipindi kile mwaka 1996 kama Babu yangu angekuwa na Uwezo mdogo Tu na akanunua hisa nyingi Crdb mwaka 1996 mfano hisa zenye thamani ya hata ya milioni 2 mwaka 1996 Leo ingekuwa ni utajiri kiasi gani?but watanzania Wengi hawakuwa na uelewa na waliokuwa wanaopinga mabadiliko ndo hao kina Nyerere na Rais anaeongoza mabadiliko anatukanwa kama "anauza nchi Kwa makaburu"...miaka 17 later ... tunamtukana Rais Kwa kuleta nchini moja ya kampuni 3 kubwa duniani Kwa shughuli za Bandari... Dpworld... kampuni imewekeza kuanzia China Hadi USA Kwa mabingwa wenyewe wa uwekezaji..Hadi Kwa wajerumani mabingwa wa ubaguzi duniani......
Kampuni CEO mmarekani lakini tunaambiwa inakuja "kueneza Uislam"... kampuni imewekeza UK lakini tunaambiwa huko kote imewekeza "fair " Ila kwetu ndo "imeuziwa nchi"...hata serikali inaposema mkataba wa uwekezaji bado kusainiwa hatutaki kuelewa...
Watu unao fikiri Wana uelewa wanatokwa na mapovu kuongea with certain "hatari kubwa Sana " iliyo mbele yetu akija "huyu mwarabu"...na wimbo mpya wa Samia anauza nchi Kwa waarabu ndo unazidi kupandishwa chati Kwa nguvu kubwa... maandamano uchwara yanachochewa na Viongozi wa dini ambao unajiuliza ni Bandari tu au kuna agenda ingine?
The more things change the more they stay the same....
Walio muita Mkapa fisadi anaeuza nchi Kwa makaburu..sasa wanafanya miamala banks zile zile na pengine kununua hisa na kunywa Safari lager huku washasahau "matusi " yote waliyomtwisha Mzee Mkapa...angalau wajitokeze waombe radhi japo hata washauri wa Mzee Mkapa wafarijike...kabla hawajapanda hili basi lingine la "Samia anauza nchi Kwa waarabu"...
Pengine wanaweza wasiwe hai ikitokea haya yote yanayozungumwa Leo yakathibitika kuwa ni uzushi , upumbavu na propaganda za wanasiasa wanaotaka Mama Samia "awapishe kwenye kiti mapema".....ili waombe radhi...Bora kwanza waombe radhi hili la Mkapa ambalo limethibitika bila Shaka kuwa "kelele za Mkapa kuuza nchi Kwa makaburu" ilikuwa uwongo, upumbavu,upeo mdogo kuhusu uchumi na uwekezaji na kudandia mabasi ya propaganda ambayo hujui dereva wake nani.
Walikuja kuwekeza
1.TBL
2.. NBC
Zingine nimezisahau....Leo...
Uwekezaji wa NBC ulipelekea Serikali kuanzisha NMB ambayo nayo waliletwa Waholanzi kununua hisa zisizozidi asilimia 5..waka provide management baadae waholanzi wale wakashangaa jinsi soko lilivyo kubwa wakaomba kununua hisa zaidi now nasikia ni asilimia 25.
Mabadiliko ya sekta nzima ya Benki aliyoyasimamia Rais Mkapa kipindi kile Leo yamepelekea tuwe na sector ya bank kubwa inayofanya kazi Kwa ufanisi.
NMB Leo ni kubwa kuliko Zanzibar GDP..na bank zote 3 kubwa Tanzania.. NMB, NBC na Crdb ni kubwa kuliko Uchumi wa Burundi...
Haya yote yasingewekana kama Rais Mkapa angeogopa "kuitwa fisadi anaeuza nchi Kwa Makaburu"...kipindi kile usingeweza kumuelewa Mkapa ...since watu waliokuwa wanaompinga walikuwa Wana influence ya kutosha ..tukianzia na Mwl Nyerere.....Na Magazeti ya Jenerali Ulimwengu yaliyokuwa Yana influence kubwa Sana Kwa jamii ya wasomi na wakosoaji wakubwa. ungeweza fikiri nchi inauzwa kweli ukifatilia mijadala...
Leo hizo banks zote 3.. NMB na Crdb zinamilkiwa na watanzania asilimia 70 NBC pia Serikali bado ina hisa za kutosha na zote hizo serikali inapokea gawio la kutosha...wale waliokuwa wanasema Mkapa anauza nchi Kwa makaburu wamenyamaza kiimya na sasa wamehamia kwenye "Samia anauza nchi Kwa waarabu" as if nothing happened...wala hawajawi jiuliza walichokuwa wanapinga kipindi kile na Hali ikoje leo? Walikuwa sahihi??
Kama hawakuwa sahihi kwanini wasiombe hata radhi in public hapo hata waliokuwa washauri wa Mkapa ambao bado wako hai wafarijike??...kama Mkapa aliuza nchi Kwa makaburu, hii nchi wanayosema anauza Samia ni ipi tena?
Itoshe kusema TBL ilienda kuwa kampuni inayolipa Kodi kubwa kuliko kampuni zote Tanzania Kwa miaka mingi Sana kama sio mpaka Leo ninavyoandika hapa....lakini shukran pekee aliyoambulia Rais Mkapa ni kuitwa "fisadi anaeuza nchi Kwa makaburu"...
Na wale watukanaji wakubwa Hadi Leo hawajawi kusema "hatukuwa sahihi" tulikosea ...Sana Sana wamevamia basi jipya "la Samia anauza nchi Kwa waarabu" Kwa nguvu mpyaa kabisa ...wazungu wanasema "ignorance is bliss"..
Mtu mjinga ana faida ya kutojijua ujinga wake...anaweza ita hata watu werevu wajinga hadharani bila woga...'ignorance is bliss ".....ungemueleza nini Mtanzania wa kawaida kuwa Mwalimu Nyerere hayuko sahihi ..wakati CEO wa Crdb wakati ule anaenda Hadi Butiama kumuomba Nyerere anunue hata hisa kidogo za Crdb kama kushawishi jamii iamke na Ku embrace"mabadiliko ya uchumi "na Nyerere ananjibu waziwazi mbele ya Tv kuwa hakuna cha mabadiliko wala nini ..ni ubepari na wizi tu kubinafsisha mabenki"...
Kwa watanzania Wengi Nyerere ni close to God ... hawezi kuwa hayuko sahihi..huwa najiuliza kama kipindi kile mwaka 1996 kama Babu yangu angekuwa na Uwezo mdogo Tu na akanunua hisa nyingi Crdb mwaka 1996 mfano hisa zenye thamani ya hata ya milioni 2 mwaka 1996 Leo ingekuwa ni utajiri kiasi gani?but watanzania Wengi hawakuwa na uelewa na waliokuwa wanaopinga mabadiliko ndo hao kina Nyerere na Rais anaeongoza mabadiliko anatukanwa kama "anauza nchi Kwa makaburu"...miaka 17 later ... tunamtukana Rais Kwa kuleta nchini moja ya kampuni 3 kubwa duniani Kwa shughuli za Bandari... Dpworld... kampuni imewekeza kuanzia China Hadi USA Kwa mabingwa wenyewe wa uwekezaji..Hadi Kwa wajerumani mabingwa wa ubaguzi duniani......
Kampuni CEO mmarekani lakini tunaambiwa inakuja "kueneza Uislam"... kampuni imewekeza UK lakini tunaambiwa huko kote imewekeza "fair " Ila kwetu ndo "imeuziwa nchi"...hata serikali inaposema mkataba wa uwekezaji bado kusainiwa hatutaki kuelewa...
Watu unao fikiri Wana uelewa wanatokwa na mapovu kuongea with certain "hatari kubwa Sana " iliyo mbele yetu akija "huyu mwarabu"...na wimbo mpya wa Samia anauza nchi Kwa waarabu ndo unazidi kupandishwa chati Kwa nguvu kubwa... maandamano uchwara yanachochewa na Viongozi wa dini ambao unajiuliza ni Bandari tu au kuna agenda ingine?
The more things change the more they stay the same....
Walio muita Mkapa fisadi anaeuza nchi Kwa makaburu..sasa wanafanya miamala banks zile zile na pengine kununua hisa na kunywa Safari lager huku washasahau "matusi " yote waliyomtwisha Mzee Mkapa...angalau wajitokeze waombe radhi japo hata washauri wa Mzee Mkapa wafarijike...kabla hawajapanda hili basi lingine la "Samia anauza nchi Kwa waarabu"...
Pengine wanaweza wasiwe hai ikitokea haya yote yanayozungumwa Leo yakathibitika kuwa ni uzushi , upumbavu na propaganda za wanasiasa wanaotaka Mama Samia "awapishe kwenye kiti mapema".....ili waombe radhi...Bora kwanza waombe radhi hili la Mkapa ambalo limethibitika bila Shaka kuwa "kelele za Mkapa kuuza nchi Kwa makaburu" ilikuwa uwongo, upumbavu,upeo mdogo kuhusu uchumi na uwekezaji na kudandia mabasi ya propaganda ambayo hujui dereva wake nani.