Ni jambo la kusikitisha sana kuona viongozi wa dini wa Kikristo, hasa Wakatoliki, wakikataa katakata Tanzania kujiunga na OIC. Sababu wanayoitoa ni kwamba Tanzania sio nchi ya kidini hivyo haiwezi kujiunga na OIC ambacho ni chombo cha Waisalamu. Wakati wanaendelea kushushumalia Tanzania isijiunge na OIC, wao wana vyombo mbalimbali vya Kikatoliki hapa Tanzania vinavyowaunganisha na Wakatoliki dunia nzima. Kwa mfano, Balozi wa Vatican ambaye ni Mwakilishi wa Papa yupo hapa Tanzania. Isitoshe, wana chombo chao cha kimataifa kuhusu masuala ya elimu hapa Tanzania kiitwacho Tanzania Episcopal Conference ambacho kimetapakaa dunia nzima. Kwa nini wao waruhusiwe kuwa na vyombo vya kidini vya kimataifa wakati Waislamu wakataliwe? Kibaya zaidi ni kwamba wakati Tanzania inakataliwa kujiunga na OIC, nchi zingine kama Uganda, Cameroon, Nigeria na Mozambique, Ivory Coast ni wanachama wa OIC na wanafaidika na misaada wanayopata kutoka OIC. Huu ni ubeberu uliopindukia. Hali hii haikubaliki hata kidogo na waislamu wataendelea kupigania haki yao hii mpaka waipate au Wakristo wa Tanzania na wao wasiruhusiwe kujiunga na vyombo vya kidini vya kimataifa. Mods muwe wavumilivu na mawazo tofauti ya members ili mradi hayavunji kanuni za JF na sheria za nchi. Mjitahidi kuzuia unazi wenu. Aluta Continua.